Habari Za Kitheokrasi
Afrika Mashariki: Hudhurio kamili la Ukumbusho wa 1994 ni kama ifuatavyo: Kenya: 26,588; Rwanda: 9,834; Sudan: 3,660; Tanzania: 15,896; Uganda: 4,810.
Kamerun: Ofisi mpya ilianzishwa katika Julai, ikilingana na kilele kipya cha wahubiri 21,323.
Kenya: Wakati wa mwaka wa utumishi wa 1994, makutaniko mapya 11 yaliundwa, karibu kutaniko moja jipya kila mwezi!
Rwanda: Hivi karibuni ndugu zetu kutoka Rwanda katika kambi za wakimbizi katika Mashariki mwa Zaire walikuwa na makusanyiko ya mzunguko mahali patatu na 86 walibatizwa. Kati ya 54 waliobatizwa katika Goma, Zaire, 31 walijaza utumishi wa upainia-msaidizi mara moja.
Tanzania: Hivi karibuni Jumba la Ufalme la Kigoma liliwekwa wakfu kukiwa na 150 waliohudhuria programu ya kuwekwa wakfu.
Zaire: Hata kujapokabiliwa na msiba mkuu wa mamia ya maelfu ya wakimbizi wakiingia Zaire, kilele kipya cha wahubiri 83,442 kilifikiwa katika Julai. Akina ndugu wamefanya jitihada bora zaidi kusaidiana, nao wasema kwamba mipango ya msaada kutoka nje yathaminiwa sana.