Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/95 uku. 1
  • Kuhubiri—Pendeleo Lenye Heshima

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri—Pendeleo Lenye Heshima
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Thamini Pendeleo Lako la Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kuhubiri Kuhusu Ufalme Ni Pendeleo la Pekee
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Tunahitaji Kudumisha Bidii Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 2/95 uku. 1

Kuhubiri—Pendeleo Lenye Heshima

1 Huduma ya habari njema ni pendeleo lenye heshima ambalo Yehova ametupa sisi. (Rum. 15:16; 1 Tim. 1:12) Je, wewe huiona kwa njia hiyo? Wala kupita kwa wakati wala kudhihaki kwa wengine hakupasi kuruhusiwa kupunguze umaana wayo machoni petu. Kuchukua jina la Mungu ni heshima inayopewa wachache tu. Twaweza kufanyaje uthamini wetu kuelekea pendeleo hili uongezeke?

2 Kuhubiri ujumbe wa Ufalme hakutuletei upendeleo wa ulimwengu. Wengi huona kazi yetu kwa ubaridi au kwa kutojali. Wengine hudhihaki na kuipinga. Upinzani huo waweza kutoka kwa wafanyakazi wenzetu, majirani, au hata washiriki wa familia. Machoni pao huenda tukaonekana kuwa wenye kuongozwa vibaya na kuwa wapumbavu. (Yn. 15:19; 1 Kor. 1:18, 21; 2 Tim. 3:12) Maneno yao ya kuvunja moyo yana kusudi la kupunguza bidii yetu na kutufanya tupunguze mwendo au tuache pendeleo letu lenye heshima. Maoni hasi yanaendelezwa na Shetani, ambaye “amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu.” (2 Kor. 4:4) Wewe huitikiaje?

3 Ni jambo la maana kukumbuka kwamba kuhubiri kwetu juu ya Ufalme ni kazi iliyo ya maana zaidi ambayo yeyote wetu angeweza kuwa akifanya leo. Tuna ujumbe wenye kuokoa uhai usiopatikana kwa njia nyingine yoyote. (Rum. 10:13-15) Kuwa na kibali cha Mungu, si cha mwanadamu, ndilo jambo la maana. Maoni hasi ya ulimwengu juu ya utendaji wetu wa kuhubiri hayatuzuii tusitangaze habari njema kwa ujasiri.—Mdo. 4:29.

4 Yesu alithamini sana pendeleo lake la kufanya mapenzi ya Baba yake. (Yn. 4:34) Alijitoa kabisa kwenye huduma naye hakuruhusu wala vikengeusha-fikira wala wapinzani wamfanye apunguze mwendo. Sikuzote kuhubiri ujumbe wa Ufalme kulichukua mahali pa kwanza maishani mwake. (Luka 4:43) Tunaamriwa tuige kielelezo chake. (1 Pet. 2:21) Kwa kufanya hivyo, twatumika tukiwa “wafanya kazi pamoja na Mungu.” (1 Kor. 3:9) Je, tunatumia kwa faida kamili pendeleo hili? Je, sisi hutafuta pindi za kushiriki habari njema pamoja na wengine kwa njia rasmi na kivivi-hivi pia? Tukiwa Mashahidi wa Yehova, twapaswa sikuzote kuwa tayari ‘kulifanyia jina lake tangazo la hadharani.’—Ebr. 13:15, NW.

5 Ushiriki wetu katika huduma wategemea sana mtazamo wetu. Je, twathamini kwa kina kirefu yale yote ambayo Yehova ametufanyia? Je, tumekuza mioyoni mwetu upendo kwa Yehova unaotuchochea kufanya yote tuwezavyo katika utumishi wake? Kutafakari juu ya baraka tunazofurahia sasa na pia yale ambayo Yehova ameahidi kwa wakati ujao kwatusaidia tumpende Muumba wetu sana. Upendo huo hutuchochea kwenye utendaji—udumifu na ukawaida katika kazi ya kuhubiri Ufalme kwa kadiri hali zetu ziruhusuvyo. Bidii yetu itatoa uthibitisho wa upendo wetu kwa Yehova na kwa jirani yetu.—Mk. 12:30, 31.

6 Twaonyesha jinsi tunavyothamini kitu sana kwa yale tufanyayo nacho na kusema juu yacho. Je, sisi huthamini kikweli pendeleo letu la kuhubiri juu ya Ufalme? Je, sisi hutukuza huduma yetu? Je, tumeazimia kudumu katika kazi hii muhimu ujapokuwa upinzani? Tukithamini sana pendeleo hili la ajabu, kwa hakika tutakuwa wenye bidii na wenye moyo wote.—2 Kor. 4:1, 7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki