Neno la Ufalme—Kupata Maana Yalo
1 Katika kielezi chake cha mpanzi, Yesu alisema kwamba mbegu iliyoanguka juu ya “udongo mzuri” ilifananisha yule “alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo [“kupata maana yalo,” NW].” (Mt. 13:23) Baada ya kusikia juu ya Ufalme, je, sisi ‘tumepata maana yalo’? Huo huathiri maisha zetu kadiri gani? Je, tumetanguliza masilahi ya Ufalme, hivyo tukifunua kwamba tulipata maana ya ujumbe huo?
2 Uelewevu sahihi wa ujumbe wa Ufalme wataka funzo la kibinafsi. Twahitaji kuchukua wakati kutafakari juu ya chakula cha kiroho kiandaliwacho. Kusoma upesi-upesi Mnara wa Mlinzi ni kama kumeza upesi mlo mtamu wenye lishe nzuri. Je, wewe huchukua wakati wa kutolea chakula cha kiroho ufikirio kamili? Ili kupata manufaa zaidi, lazima kuwe na kichocheo na hamu yenye afya ya kiroho. Ikiwa mambo hayo yakosekana, utendaji mwingine waweza kupunguza manufaa za funzo la kibinafsi au kutumia wakati wote tunaohitaji kwa ajili yalo. Si rahisi kushikamana na ratiba nzuri ya funzo. Ingawa kufanya hivyo kwataka kusawazisha kwa uangalifu mambo ya kutangulizwa, utajiri wa kiroho utakaopatikana ni wenye thamani kubwa sana.—Mit. 3:13-18; Kol. 1:27.
3 Kuyachunguza Maandiko hutusaidia kila siku kuwa na fikira chanya, zenye kujenga juu ya Ufalme. Wale “wenye kutambua uhitaji wao wa kiroho” hupanga kuchukua dakika chache kila siku kusoma andiko na maelezo. (Mt. 5:3, NW) Maandiko mengi hueleza pande mbalimbali za Ufalme. Kwa kielelezo, mnamo Novemba 22, 1994, andiko lililokaziwa lilikuwa Mathayo 13:4. Elezo lilizungumzia tumaini la Ufalme na kutukumbusha juu ya hatari za ushirika usiofaa pamoja na watu wa ukoo na majirani. Jambo la kwamba katika makao ya Betheli kotekote ulimwenguni, kuna mazungumzo ya dakika 15 juu ya andiko la kila siku kila asubuhi ya siku ya kazi hukazia manufaa na uzito wa kuzungumzia andiko la siku pamoja. Je, familia yako hutia ndani mazungumzo kama hayo katika kawaida yenu ya kila siku?
4 Kadiri uthamini wako kuelekea Ufalme uongezekavyo, kutakuwa na kichocheo kikubwa zaidi cha kushiriki ujumbe wa Ufalme pamoja na wengine. Mnara wa Mlinzi na Amkeni! huandaa kile kiwezacho kufananishwa na kuni za akilini zinazopatia akili zetu habari mpya, za kisasa. Hayo hutusaidia tudumishe ufahamu mwingi wa jinsi ulimwengu unavyohitaji sana Ufalme wa Mungu. Hutusaidia tuwe watu wa kiroho, walio na “nia ya Kristo.” (1 Kor 2:15, 16) Yote hayo yaweza kuimarisha tumaini letu na kuongeza bidii yetu ya kushiriki tumaini la Ufalme na wengine.—1 Pet. 3:15.
5 Ni muhimu kwamba sisi binafsi tupate maana ya ujumbe wa Ufalme. Ufalme ndiyo njia ambayo Mungu atatumia kutegemeza enzi kuu yake, kukomesha uovu, na kuleta ulimwengu mpya—paradiso. Yesu alituamuru tuutangulize maishani mwetu. Lazima tuwe raia wenye mfano wa kondoo ili kuishi chini ya utawala wa huo. (Mt. 6:10, 33) Tumia fursa yako kikamili ili kufurahia baraka za huo.