Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/95 uku. 2
  • Kunufaika na Hotuba za Watu Wote Zilizosahihishwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kunufaika na Hotuba za Watu Wote Zilizosahihishwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Sababu Gani Wewe Unataka Kutoa Hotuba ya Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Endelea Kufanya Maendelio
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 8/95 uku. 2

Kunufaika na Hotuba za Watu Wote Zilizosahihishwa

1 Historia ya kisasa ya Mashahidi wa Yehova inafafanuliwa kwa usahihi katika maneno ya Mithali 4:18: “Njia ya wenye haki ni kama nuru ing’aayo, ikizidi kung’aa hata mchana mkamilifu.”

2 Kwa kupatana na hilo, kutaniko la Kikristo huendelea kupokea maelezo ya wazi zaidi ya wakati unaofaa na ya kisasa juu ya mafundisho ya Biblia. (Mt. 24:45-47) Yaelekea kwamba wewe waweza kusimulia vielelezo vya jambo hilo ambavyo umeona tangu uanze kushirikiana na Mashahidi wa Yehova. Mikutano ya kutaniko, kutia ndani hotuba za watu wote, hutusaidia tuendelee kuwa sambamba na nuru ya kweli inayoongezeka.

3 Mihtasari Iliyosahihishwa: Hivi karibuni, Sosaiti imefanya mihtasari ya hotuba za watu wote iwe ya kisasa. Habari mpya imetiwa ndani yazo, na mambo ya maana yameeleweshwa wazi. Ikiwa kutaniko litapokea manufaa kamili kutokana na maelezo haya ya kisasa, akina ndugu wanaotoa hotuba za watu wote wapaswa watumie tu mihtasari ya karibuni zaidi.

4 Ili kupata faida zaidi kutokana na hotuba za watu wote, fikiria vichwa vya hotuba zitakazotolewa. Kabla ya kuhudhuria Mkutano wa Watu Wote, jaribu kukumbuka maelezo ya karibuni zaidi kutoka kwa vyanzo vya kitheokrasi juu ya habari hiyo. Kisha, unaposikiliza, tazamia kukuzwa kwa maelezo hayo. Andika njia zozote mpya za kutokeza kweli hizo kwa matumizi ya wakati ujao. Hilo lahakikisha kwamba wewe utapata manufaa mengi zaidi kutokana na hotuba za watu wote zilizosahihishwa.

5 Hotuba za Watu Wote Zapasa Kuwa Zenye Kuarifu na pia Zenye Kuhamasisha Wasikilizaji: Yesu aliposema, yeye alifikia mioyo ya wasikilizaji wake. Kwenye umalizio wa Mahubiri ya Mlimani ya Yesu, iliyokuwa hotuba maarufu zaidi ya watu wote iliyopata kutolewa, kama vile Mathayo 7:28 liripotivyo: “Makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake.”

6 Yakiwa yanakumbuka kielelezo cha Yesu, mabaraza ya wazee yapasa kutumia busara katika kuidhinisha wasemaji wapya wa hotuba za watu wote, yakiwapa migawo wale ndugu tu walio walimu wazuri, wale ambao watashikamana kwa ukaribu na mihtasari ya Sosaiti, na wanaoweza kudumisha uangalifu wa wasikilizaji. Akina ndugu wanaogawiwa pendeleo la kutoa hotuba za watu wote wapaswa kujitahidi kwa kuendelea kuboresha uwezo wao wa kusema, wakikubali shauri na madokezo yoyote yanayopokewa kutoka kwa wazee.

7 Kama ilivyotabiriwa kwenye Isaya 65:13, 14, ufanisi wa kiroho wa watu wa Mungu waendelea kuwa wazi zaidi. Mpango wa hotuba za watu wote ni mojapo njia nyingi ambazo ‘tunafundishwa na Yehova.’—Isa. 54:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki