Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti
Juma Linaloanza Agosti 7
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak 15: “Mwapaswa Kuwa Watu wa Namna Gani?” Maswali na majibu.
Dak 20: “Iweni Wafundishaji wa Neno la Mungu—Mkitumia Broshua.” Ndugu aliyegawiwa sehemu hii atazungumza na wahubiri wengine wawili au watatu juu ya sehemu mbalimbali za broshua. Kisha watajizoeza utoaji wao kwa wao.
Wimbo 137 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 14
Dak 5: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak 10: Tumia Shule kwa Manufaa. Mzee atoa wonyesho wa jinsi mzazi anavyoweza kuongea na mwana au binti tineja kuhusu kuteua mafunzo ya masomo shuleni. Zungumzia uhitaji wa kuchagua mada ambazo zitasaidia kufuatia kazi-maisha katika huduma.—Ona Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 1992, kurasa 16-18, mafungu 3-11.
Dak 15: “Wazazi Walio na Shangwe!” Hotuba ikitolewa na mzee. Tia ndani maelezo ya ziada kutoka Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1987, kurasa 13-15, mafungu 14-23.
Dak 15: “Mwenendo wa Kikristo Shuleni.” Maswali na majibu. Tia moyo wazazi wapitie Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1991, kurasa 23-26, pamoja na watoto wao, hasa sehemu zinazoshughulika na masuala ambayo watoto wanaelekea kukabili.
Wimbo 157 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 21
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Zungumza juu ya “Kunufaika na Hotuba za Watu Wote Zilizosahihishwa.”
Dak 15: “Kujitolea Wenyewe kwa Hiari kwa Kila Kazi Njema.” Hotuba yenye idili ikitolewa na mzee kuhusu mafungu 1-9.
Dak 20: “Kujitolea Wenyewe kwa Hiari kwa Kila Kazi Njema.” Maswali na majibu kuhusu mafungu 10-15. Kazia mahitaji ya kwenu na njia ambazo wote wanaweza kutoa usaidizi.
Wimbo 156 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 28
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Kazia matoleo ya magazeti ya karibuni ambayo yanaweza kutolewa katika utoaji.
Dak 15: “Ziara za Kurudia Zenye Mafanikio Zahitaji Kufundisha Kwenye Matokeo.” Pitia mambo makuu na upange uwe na wonyesho mmoja au mawili ya kuonyesha jinsi utoaji waweza kutumiwa.
Dak 20: Toa Kitabu Kuishi Milele Wakati wa Septemba. Eleza jinsi kitabu hiki kinatimiza daraka la maana katika kutoa ujumbe wa hukumu wa Yehova. (Ona Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 1988, kurasa 25-26, mafungu 17-18.) Elezea jambo lililoonwa katika mafungu 3-4 kwenye ukurasa 15 wa Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 1992. Toa uangalifu kwa vielezi vyenye kuvutia vinavyoonekana kwenye kurasa 3, 11-13, na 156-158 za hicho kitabu. Zungumzia njia ambazo vielezi hivi vyaweza kutumiwa ili kuanzisha mazungumzo. Panga uwe na mhubiri anayestahili atoe utoaji mfupi akitumia mojapo Maandiko yaliyoonyeshwa kwenye kurasa 156-158. Kazia mradi wa kujaribu kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kumbusha wote watwae nakala za kutumia mwisho-juma huu.
Wimbo 178 na sala ya kumalizia.