Mikutano Ya Utumishi Kwa Machi
Juma Linaloanza Machi 6
Dak 13: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.” Ikiwa yajulikana, tangaza tarehe ya siku ya kusanyiko la pekee inayofuata, na utie moyo wote wafanye mipango ya kuhudhuria.
Dak 15: “Vingi Vinapewa—Vingi Vinatakwa.” Maswali na majibu. Tia moyo wale wanaostahili wafikirie kujiandikisha kuwa mapainia-wasaidizi wakati wa Aprili.
Dak 17: “Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii.’” Pitia mambo makuu. Karibisha wasikilizaji wasimulie maono waliyofurahia kwa kutumia au kuangusha kitabu Upeo wa Ufunuo. Himiza wote wawe na mtazamo chanya katika kutoa kitabu hicho, kwa kuwa chashughulikia matukio ya karibuni yanayohangaisha kila mtu. Fanyia wonyesho utoaji mmoja au miwili.
Wimbo 31 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 13
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Toa elezo fupi linaloelekeza fikira kwenye sanduku “Kikumbusha kwa Mwandishi na Mwangalizi wa Utumishi.” Ripoti ya hesabu.
Dak 15: “Trakti Habari za Ufalme ya Wakati Ufaao Kugawanywa Ulimwenguni Pote.” Hotuba ikitolewa na mzee. Kazia umaana wa utendaji huu unaokuja ulio wa pekee wakati wa Aprili na Mei. Himiza wote, kutia na wapya, wapange kushiriki kikamili.
Dak 15: “Onyesha Wengine Ufikirio—Sehemu ya 2.” Hotuba na mazungumzo yakishughulikiwa na mzee. Eleza matatizo yoyote ambayo yameonwa kwenu na utoe onyo la upole linalofaa.
Wimbo 36 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 20
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Uwe na wonyesho wa familia ikitumia Kitabu-Mwaka cha 1995 (katika Kiingereza). Kikundi cha familia chaeleza uthamini kwa ajili ya kitabu hicho; baba apitia kwa ufupi mambo makuu ya habari ya utangulizi kwenye kurasa 3-11. Wanazungumzia jinsi watakavyojaribu kusoma kurasa chache za Kitabu-Mwaka wakiwa pamoja kila juma na kuhakikisha kwamba kila siku wataelekeza fikira kwenye andiko la Biblia lililochaguliwa katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku.
Dak 15: Mahitaji ya kwenu. Au toa hotuba juu ya makala “Mkiwiwa Kodi, Lipeni Kodi,” katika Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 1994, kurasa 26-28.
Dak 15: “Saidia Wengine ‘Kuyashika Yaliyoandikwa.’” Pitia mambo makuu, kisha ufanyie wonyesho ziara moja au mbili za kurudia.
Wimbo 52 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 27
Dak 8: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: “Tukio la Maana Zaidi Katika Historia ya Binadamu.” Zungumzia makala pamoja na wasikilizaji. Pitia mipango ya kwenu kwa ajili ya Ukumbusho. Eleza kwa nini twahitaji kualika wenye kupendezwa na kuwasaidia wahudhurie.
Dak 12: Zungumzia Sanduku la Swali.
Dak 10: Kutoa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! wakati wa Aprili. Pitia kifupi miongozo kwa habari ya kujaza karatasi za andikisho. Tia moyo kuwa na mtazamo chanya. Mahali toleo la andikisho linakataliwa hakikisha unatoa magazeti ya karibuni zaidi. Weka rekodi ya kupendezwa kote na maangusho yote.
Wimbo 176 na sala ya kumalizia.