Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/95 uku. 1
  • Vingi Vinapewa—Vingi Vinatakwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vingi Vinapewa—Vingi Vinatakwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Zawadi Inayotoka kwa Yehova Mwenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Sifa za Kimungu za Upendo na Chuki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kujitolea Wenyewe kwa Hiari kwa Kila Kazi Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Yanayohitajiwa Ili Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 3/95 uku. 1

Vingi Vinapewa—Vingi Vinatakwa

1 Tumependelewa kama nini kuwa na kweli! Kwa sababu ya wakfu wetu kwa Yehova, ‘tumekabidhiwa habari njema.’ (1 The. 2:4, NW) Hilo latuweka chini ya daraka kubwa zaidi. Yesu alisema hivi: “Kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi.”—Luka 12:48b.

2 Maneno hayo ni ya kweli kama nini! Kwa kuwa sisi sote tumebarikiwa na ujuzi wa Neno la Mungu, ushirika wa ajabu wa akina ndugu, na tumaini zuri ajabu, yaweza kusemwa kwa kweli kwamba tumepewa vingi. Kwa kufaa, vingi vinatazamiwa kwetu.

3 Dumisha Maoni Yafaayo Kuelekea Matakwa: Wengine wamekata maneno kwamba vingi mno vinatazamiwa kwetu. Akiwa Kichwa cha kutaniko la Kikristo, Yesu Kristo huamua “kihitajiwacho” ili lifanye kazi ifaavyo. (Efe. 4:15, 16, NW) Yeye atuhakikishia kwamba ‘nira yake ni laini, na mzigo wake ni mwepesi.’ (Mt. 11:28-30) Yeye huwapa nafasi kwa upendo wale walio na mapungukio. (Luka 21:1-4) Tukitoa kiasi tuwezacho kabisa, haidhuru ni kiasi gani, tutabarikiwa.—Kol. 3:23, 24.

4 Jiulize mwenyewe, ‘Je, masilahi ya Ufalme hutangulizwa maishani mwangu? Je, ninatumia wakati wangu na mali zangu kwa njia inayotokeza sifa kwa jina la Mungu na manufaa kwa wengine? Je, mimi huona kwamba furaha yangu kubwa zaidi hutokana na kumtumikia Yehova badala ya kutokana na kufurahia kwa ubinafsi vitu vya kimwili?’ Majibu yetu ya haki kwa maswali hayo yatafunua madhumuni yaliyomo mioyoni mwetu.—Luka 6:45.

5 Epuka Kushawishiwa Kufanya Yaliyo Mabaya: Hakujawa kamwe na vishawishi na mibano ya jinsi hii kuelekea kujipendeza, pupa, na upendo wa raha ya kiashiki. Kila siku tunakabiliwa na magumu ya kiadili, na vishawishi vya kuacha imani. Ili kukabiliana na magumu haya kwa mafanikio, ni lazima tumwombe Yehova atusaidie. (Mt. 26:41) Kupitia roho yake, yeye aweza kutuimarisha. (Isa. 40:29) Kusoma Neno la Mungu kila siku ni msaada mkubwa. (Zab. 1:2, 3) Kujitia nidhamu na kujidhibiti kuna daraka kubwa pia.—1 Kor. 9:27.

6 Hakutoshi kupenda yaliyo mema—lazima pia tuchukie yaliyo mabaya. (Zab. 97:10) Hilo lamaanisha kutokuza tamaa kwa ajili ya yale mambo yaliyo mabaya. Mithali 6:16-19 yaorodhesha mambo saba ambayo Yehova huchukia. Kwa wazi, mtu anayetaka kumpendeza Yehova lazima achukie mambo ya jinsi hiyo. Tukiwa tumebarikiwa na ujuzi sahihi kuhusu kweli, twapaswa kutaka kutenda kwa kupatana na ujuzi huo, tukiendelea kukaza akili zetu juu ya mambo mazuri.

7 Yafaa kuomba kuwa na hali zilizo zenye kupendeleka za ‘kuwa sikuzote na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.’ (1 Kor. 15:58, NW) Wengi wameona kwamba ratiba yenye shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova ni ulinzi kwa sababu hairuhusu wakati mwingi kwa ajili ya ufuatiaji wa mambo yasiyofaa kitu.

8 Baada ya yote hayo, yale ambayo Yehova ataka kwetu ni yenye kufaa. (Mika 6:8) Tuna kila sababu ya kushukuru kwa ajili ya pendeleo moja-moja la utumishi. (Efe. 5:20) Kwa hiyo twaendelea ‘kufanya kazi kwa bidii na kujikakamua,’ tukiwa na hakika kwamba thawabu yetu itakuwa kubwa zaidi sana kuliko lolote lile linalotakwa kwetu.—1 Tim. 4:10, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki