Sanduku La Swali
◼ Ni vifaa gani tunavyopaswa kutwaa mikutanoni?
Kila juma tunapokea mafundisho yenye manufaa na kitia-moyo kwenye mikutano ya kutaniko. (Isa. 48:17; Ebr. 10:24, 25) Hata hivyo, kadiri tunavyonufaika, yategemea sana kama twaja tukiwa tumejitayarisha au la.
Itakuwa vizuri kwa kila mshiriki wa familia kuwa na habari ya funzo yake mwenyewe na vifaa vingine vinavyohitajiwa kwa ajili ya mikutano. Hivi vitatia ndani Biblia, kitabu cha wimbo, kichapo cha funzo, kitabu cha kuandikia mambo, na kalamu au penseli.
Kwa ajili ya Shule ya Kitheokrasi, Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na kitabu Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi vyahitajiwa. Vifaa hivi hutusaidia tuweke akilini kichwa cha hotuba za wanafunzi zinazotolewa na kuweka akili zetu kwa kiongozi wa shule anapotoa shauri. Twaweza kutumia kibinafsi shauri na madokezo ili kuboresha hotuba zetu wenyewe na utoaji wa utumishi wa shambani. Kuanzia Januari, hotuba nyingi za maagizo katika makutaniko fulani zategemea kitabu Jehovah’s Witnesses—Proclaimers of God’s Kingdom. Huenda lisiwe jambo la busara kwa kila mshiriki wa familia kutwaa nakala yake mwenyewe; labda buku moja lingeletwa ili kwamba familia iwe nalo kwa ajili ya marejezo. Katika makutaniko mengine hotuba za maagizo zategemea kitabu Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli na ingekuwa vizuri kwa kila mshiriki wa familia kuwa na nakala yake mwenyewe.
Kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi, twahitaji kuwa na Huduma ya Ufalme Yetu ya wakati huo na kitabu Kutoa Sababu. Twaa kichapo chochote kitakachorejezewa wakati wa mkutano huo, kama vile vifaa vya fasihi ambavyo vitatumiwa katika utoaji wa kutolewa onyesho. Wazee wapaswa kuwa na nakala ya kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu.
Wazazi wapaswa kujitahidi kufanya watoto wao wakae kimya na kusikiliza kwa uangalifu kwenye mikutano ya kutaniko. Kuwapa nakala za kibinafsi za Mnara wa Mlinzi na vichapo vinginevyo, hata kabla hawajaanza kusoma, huwatia moyo wawe na upendezi. Wachanga wanapofunzwa kuheshimu vichapo vya kitheokrasi na kuvitumia, tabia zinazofaa za kiroho hufanyizwa maishani.
Shangwe na utoshelezo tunaopata kutoka mikutano ya kutaniko huongezwa zaidi tunapokuja tukiwa tumejitayarisha kikamili. (2 Tim. 3:17) Hii ndiyo njia bora zaidi ya kuhakikisha kwamba ‘tunajazwa ujuzi sahihi wa mapenzi ya [Mungu] katika hekima yote na ufahamivu wa kiroho.’—Kol. 1:9, NW.