Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/95 uku. 1
  • Kristo Akiwa Kigezo kwa Vijana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kristo Akiwa Kigezo kwa Vijana
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Je, Waweza Kujitolea?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Je, Hii Yaweza Kuwa Kazi-Maisha Inayokufaa Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 6/95 uku. 1

Kristo Akiwa Kigezo kwa Vijana

1 Baada ya mazungumzo marefu ya Biblia, kijana mmoja alisema: “Nilivutiwa na utu wenye nguvu wa Yesu Kristo. Huyu ndiye kiongozi ambaye ningeweza kuamini.” Haiwezekani kusemwa hivyo juu ya wanasiasa au mabingwa wa michezo na vitumbuizo. Wakristo wa kweli hawawaoni kuwa vigezo wale wanaokubali waziwazi viwango vya kilimwengu na mitindo-maisha isiyo ya Kikristo.—Zab. 146:3, 4.

2 Vijana waweza kuhakikishiwa kwamba wanapojizoeza imani katika Yesu Kristo, wao wanajiweka kuwa kondoo wa Mungu nao wajulikana na Yesu. Mchungaji Mwema anawajali. (Yn. 10:14, 15, 27) Vijana wanaofuata Kristo kuwa Kigezo chao wanabarikiwa.

3 Ndugu mmoja anayetumika katika Betheli ya Brooklyn wakati huu alikuwa na mradi wa pendeleo hili la utumishi tangu alipokuwa na umri wa miaka minane. Alitiwa moyo kuona utumishi wa Betheli kuwa njia inayofaa ya kufuata kielelezo cha Kristo akiwa mkubwa. Wazazi wake, na vilevile waangalizi wasafirio, waliweka mradi huu mbele yake. Ili kumsaidia kujitayarisha, walimtia moyo ajitumikishe kwa bidii kama mshiriki wa familia ya Betheli, akifanya kazi ndogo-ndogo nyumbani, kusaidia kutunza Jumba la Ufalme, na kusitawisha stadi katika huduma. Baada ya kufurahia utumishi wa Betheli kwa miaka kadhaa sasa, yeye anashukuru kwamba alipokuwa akikua, alifanya jitihada ya kuiga kielelezo cha Kristo.

4 Yesu hakufuatia kazi-maisha ya kilimwengu; alichagua huduma. Dada mmoja mchanga alitaka kupainia alipohitimu kutoka shule lakini akasita kwa sababu hakuwa na kazi ya kuajiriwa ya muda-muda. Aliendelea kufikiri hivi: ‘Kwanza nitatafuta kazi, kisha nitaijaza fomu yangu ya upainia.’ Mzee mmoja alimdokezea kwamba kadiri alivyokuwa akingoja, ndivyo kazi ya wakati wote ingevutia, kwa kuwa hangekuwa na kitu cha kumzuia kuikubali. Yeye alieleza: “Nilisali kwa Yehova anipe roho yake takatifu iniongoze.” Mara moja akajiandikisha kuwa painia msaidizi na baadaye akawa painia wa kawaida. Muda mfupi baada ya hapo, alipata kazi ya kuajiriwa inayofaa iliyopatana na ratiba yake ya painia.

5 Yesu alitangazia kila mtu ujumbe wa Ufalme kwa ujasiri. (Mt. 4:23) Vijana Wakristo pia wanaweza kujifunza kuwa wenye ujasiri katika kuhubiri, si kuogofywa na wengine. Shahidi mmoja mwenye umri wa miaka 14 aliripoti hivi: “Kila mtu shuleni ajua msimamo wangu nikiwa Mkristo. . . . Wanaujua vizuri sana hivi kwamba nikikutana na mwanadarasa mwenzangu katika huduma, sioni haya. Kwa kawaida wanafunzi wenzangu husikiliza, na nyakati nyingi wao hupokea vichapo.”

6 Kufikiria kielelezo cha Kristo kwaweza kusaidia vijana wafanye maamuzi yenye hekima juu ya wakati wao ujao. Badala ya kuwa wenye shughuli nyingi za ufuatiaji wa kilimwengu, wao ‘humkumbuka Muumba wao Mtukufu’ kwa kuonyesha bidii katika utumishi wa Yehova. (Mhu. 12:1, NW) Kama vile Kristo Yesu, wao wanasitawisha “kumpenda Baba,” ambako huleta baraka zenye kutamanika zaidi kuliko chochote kitolewacho na ulimwengu. Badala ya ‘kupitilia mbali’ pamoja na ulimwengu, wanaweza kutazamia ‘kubaki milele.’—1 Yoh. 2:15-17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki