Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
Juma Linaloanza Juni 5
Dak 12: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak 15: “Yehova Hutoa Nguvu.” Maswali na majibu. Simulia yaliyoonwa katika Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 1992, ukurasa 32.
Dak 18: “Yehova Ndiye Muumba Wetu.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Panga uwe na maonyesho mawili yakionyesha jinsi ya kutumia utoaji uliodokezwa. Tia ndani madokezo mafupi juu ya jinsi ya kufanya ziara za kurudia, kufuatia maangusho ya trakti Habari za Ufalme zilizogawanywa wakati wa Aprili na Mei.
Wimbo 17 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 12
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak 17: “Kristo Akiwa Kigezo kwa Vijana.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo kutoka Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1986, kurasa 4-6.
Dak 18: “Wasaidie Wale Wasiokuwa na Imani.” Kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko apitia makala pamoja na wahubiri wawili au watatu kisha azungumza jinsi ya kutumia habari. Wanajizoeza kwa kutoa onyesho la utoaji kwa mmoja na mwenzake.
Wimbo 122 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 19
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Toa maonyesho mawili au matatu mafupi ya utoaji wa magazeti yanayoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak 18: Shughulikia Barua ya Tawi kukiwa na ushiriki wa wasikilizaji. Wasaidie wote waone majengo mbalimbali mahali pa ujenzi. Tia moyo ndugu vijana walio waseja wajitolee kwa pendeleo hili zuri ajabu. Fikiria azimio lolote ambalo kutaniko huenda likataka kufanya kuhusu michango.
Dak 17: “Tumia Vizuri Wakati Wako.” Maswali na majibu. Kuhusu wakati unaotumiwa kutazama televisheni, pitia madokezo yaliyo chini ya kichwa kidogo “Kuidhibiti,” ukurasa 11 wa Amkeni! la Desemba 8, 1991.
Wimbo 208 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 26
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Zungumzia kifupi umaana wa kufanya ziara za kurudia. Sehemu kubwa ya kufundisha kwetu yafanywa tunaporudi ili kusitawisha kupendezwa. Watu wachache wanaweza kufanya maendeleo ya kiroho kwa fasihi pekee. Tunapokosa kufanya ziara za kurudia, tunakosa fursa yetu bora zaidi ya kuwasaidia. Ziara za kurudia hutokeza mafunzo ya Biblia. Wahubiri wengi wamepata matokeo mazuri zaidi kwa kurudi baada ya siku moja au mbili badala ya kungoja juma moja.—Ona kitabu Huduma Yetu, kurasa 88-89.
Dak 15: Sanduku la Swali. Maswali na majibu ikishughulikiwa na kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi. Toa maelezo zaidi yakitegemea kitabu Kiongozi cha Shule, kurasa 91-92.
Dak 15: Pitia toleo la fasihi la Julai. Zungumzia mambo yenye kutokeza ya broshua ambazo kutaniko linazo akibani. Panga wahubiri watoe onyesho la jinsi zinavyoweza kutolewa mlangoni. Vielelezo: Je! Kweli Mungu Anatujali (Fungua kurasa 26-27, onyesha vielezi, na uzungumzie mojapo maandiko kuhusu Paradiso ijayo.) Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje? (Fungua kurasa 30-31, fikiria mojapo maandiko yaliyonukuliwa, na uzungumzie kielezi.) Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. (Kazia fikira maswali yaliyotokezwa kwenye ukurasa 2, kisha ueleze wazo moja au mawili ya Kimaandiko yenye kufariji yapatikanayo kwenye ukurasa 31.) Acha kutaniko lijue ni broshua zipi zipatikanazo sasa akibani. Pia, pitia mipango ya kushughulikia eneo lililo pekee na lisilohubiriwa mara nyingi.
Wimbo 225 na sala ya kumalizia.