Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
Juma Linaloanza Novemba 6
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak 15: Pitia Barua ya Tawi pamoja na ushiriki wa wasikilizaji. Kazia uhitaji wa kuwa na wajitoleaji zaidi. Zungumzia azimio lolote ambalo kutaniko huenda likataka kufanya kwa habari ya michango ikiwa hilo halijafanywa bado.
Dak 20: “Kila Andiko Ni Lenye Manufaa kwa Kufundisha.” Zungumza juu ya sehemu za Biblia New World Translation, ukionyesha ni kwa nini hiyo ni bora kuliko nyinginezo. Eleza faida kwa sababu imefasiriwa katika lugha ya kisasa. (Ona kitabu “Kila Andiko,” ukurasa 328, mafungu 4-6.) Uwe na maonyesho ya utoaji mbili.
Wimbo 2 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 13
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Pitia mipango ya utendaji wa utumishi wa shambani katika juma linalokuja.
Dak 15: “Kuhudhuria Mikutano kwa Ukawaida—Muhimu kwa Kusimama Kwetu Imara.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji.
Dak 20: “Jiendesheni kwa Namna Yenye Kustahiki Habari Njema.” Maswali na majibu. Toa maelezo ya ziada yanayotegemea Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1989, kurasa 16-17, mafungu 5-9.
Wimbo 23 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 20
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Mazungumzo mafupi juu ya andiko la siku. Taja manufaa zinazopatikana katika kuzungumza juu ya andiko la siku kila siku na uwatie moyo wote wazungumze juu ya andiko kila siku.
Dak 15: Mahitaji ya kwenu. (Au utoe hotuba “Je! Wewe Hufurahia Funzo la Kibinafsi?” inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1994, kurasa 8-11.)
Dak 20: “Saidia Wengine Watambue Thamani ya Biblia.” Mzee azungumza pamoja na wahubiri wawili au watatu juu ya sababu kwa nini twapaswa kufanya ziara za kurudia tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitia, kisha uwe na maonyesho ya utoaji mbalimbali uliodokezwa, kama vile katika pindi ya mazoezi.
Wimbo 8 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 27
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia andiko la siku na maelezo. Tia moyo ushiriki katika utendaji wa magazeti mwisho-juma huu.
Dak 15: “Weka Akili Yako Ikiwa Imekazwa juu ya Mambo Yaliyo Juu.” Maswali na majibu.
Dak 20: Kutoa Kitabu Mtu Mkuu Zaidi Wakati wa Desemba. Kuna uhitaji mkubwa sana wa kitabu hiki. Mamia ya mamilioni ya watu wanakiri kuwa wafuasi wa Yesu nao wadai kuamini aliyofundisha. Watu wanahitaji kujua ni nini kilichomtofautisha na wanaume wengine wote—wokovu wao wakitegemea. Kitabu Mtu Mkuu Zaidi, sura 133, husema: “Mioyo yetu inasukumwa wakati tunapofikiria ujasiri wake mwingi sana na sifa zake za kiume, hekima yake isiyolinganika, uwezo wake mwingi sana akiwa mwalimu, uongozi wake wa ujasiri, na huruma zake nyororo na hisia zenye kusikitikia wengine.” Biblia humtambulisha waziwazi kuwa (1) Shahidi (Yn. 18:37), (2) Mwokozi (Mdo. 4:12), na (3) Mfalme (Ufu. 11:15). Panga uwe na mhubiri aliye na ustadi atoe wonyesho wa utoaji akitumia baadhi ya mambo haya. Watie moyo wote washiriki katika kugawanya kitabu hiki katika Desemba.
Wimbo 78 na sala ya kumalizia.