Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/96 uku. 1
  • Hatujapata Kamwe Kuwa na Hali Nzuri Hivi ya Kiroho!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hatujapata Kamwe Kuwa na Hali Nzuri Hivi ya Kiroho!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Baraka ya Yehova Hututajirisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Kusitawisha Urafiki na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Kujitolea Wenyewe kwa Hiari kwa Kila Kazi Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Jitayarishe Sasa Kuishi Katika Ulimwengu Mpya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 5/96 uku. 1

Hatujapata Kamwe Kuwa na Hali Nzuri Hivi ya Kiroho!

1 Watu walio wengi wanatamani siku watakayoweza kusema, “Hatujapata kamwe kuwa na hali nzuri hivi!” Akilini mwao, siku hiyo itawajia wakiwa na vitu vingi vya kimwili, vikiwaruhusu ‘kupumzika, kula, kunywa, na kujifurahisha.’ (Luka 12:19) Kinyume na hilo, sasa hivi twaweza kusema kwamba kwa njia ya kiroho, hatukosi kitu chochote chema. (Zab. 34:10) Hilo lawezekanaje?

2 Mithali 10:22 hutangaza kwamba “baraka ya BWANA hutajirisha.” Sisi tunaopata upendeleo huo wa kimungu kwa kweli twaweza kusema kwamba Mungu ‘atupa vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha.’ (1 Tim. 6:17) Hili hutufanya kuwa watu matajiri zaidi duniani!

3 Kutambua Baraka Tulizo Nazo: Ni wachache kati yetu tulio na wingi wa vitu vya kimwili. Hata hivyo, tumebarikiwa kwa sababu hatuhangaiki sana kuhusu mahitaji yetu ya kila siku. Yehova ajua twahitaji vitu gani, naye aahidi kutuandalia. (Mt. 6:31-33) Uhakikishio wake hutupa amani ya akili ambayo kwa kweli ni yenye thamani.

4 Hata hivyo, baraka zetu za kiroho ni nyingi hata zaidi. Maisha zetu hutegemea chakula cha kiroho kutoka kwa Yehova. (Mt. 4:4) Wale ambao hutegemea vyanzo vya kilimwengu ili wapate chakula cha kiroho hupata njaa ilhali sisi hula na kunywa mpaka tushibe. (Isa. 65:13) “Mtumwa mwaminifu” hutugawia kwa wingi ujuzi uongozao kwenye uhai udumuo milele.—Mt. 24:45; Yn. 17:3.

5 Udugu wetu wenye thamani wa ulimwenguni pote hutuandalia ushirika wenye shauku wa ndugu na dada wenye upendo wanaoishi kila sehemu ya dunia. (Yn. 13:35) Kutaniko la kwetu ni mahali pa amani, tunapoweza kupata faraja na burudisho. Wazee wanachunga nafsi zetu wakitusaidia kukabiliana na aina nyingi za matatizo. (Ebr. 13:17) Kuwa na uhusiano wa karibu na ndugu na dada zetu hutokeza badilishano la kitia-moyo, likituimarisha kuvumilia.—Rum. 1:11, 12.

6 Hata kazi yetu ni baraka. Kazi nyingi za kimwili ni zenye kuchosha na zisizoridhisha. Kushiriki habari njema huletea wengine shangwe na kutuletea furaha. (Mdo. 20:35) Kwa kweli twaweza kuona mema kwa kazi yetu yote ya bidii.—Mhu. 2:24.

7 Zaidi ya yote, tuna tumaini zuri ajabu la wakati ujao. (Rum. 12:12) Twatazamia ulimwengu mpya mkamilifu wa uadilifu, ambamo tutaishi na wapendwa wetu kwa furaha na amani milele! Tumaini hili ni hazina inayoshinda chochote ambacho ulimwengu huu waweza kutoa.—1 Tim. 6:19.

8 Twaweza Kuonyeshaje Uthamini Wetu? Hatuwezi kumlipa Yehova kwa yale ambayo ametufanyia. Twaweza tu kuonyesha uthamini wetu kwa (1) kumshukuru kila siku kwa fadhili zake zisizostahiliwa (Efe. 5:20), (2) kuonyesha upendo wetu kwa kuwa watiifu (1 Yoh. 5:3), (3) kutakasa jina lake kwa kuhubiri habari njema (Zab. 83:18), na (4) kuunga mkono kutaniko la Kikristo kwa ushirikiano wetu wa moyo wote.—1 Tim. 3:15.

9 Tuna sababu nyingi za kuwa watu wenye furaha zaidi duniani. (Zab. 144:15b) Mtazamo, mwenendo, na utumishi wetu na uonyeshe shangwe tunayohisi katika paradiso yetu ya kiroho. Hatujapata kamwe kuwa na hali nzuri hivi!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki