Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei
Juma Linaloanza Mei 6
Dak 10: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: “Iweni Wenye Kujitoa kwa Nafsi Yote!” Maswali na majibu. Wakati ukiruhusu, toa uangalifu kwa “Mambo Makuu ya Kuzungumza Mkiwa Jamaa,” katika Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1982, ukurasa 17.
Dak 20: “Sema Kweli na Jirani Yako.” Maswali na majibu. Pitia toaji zilizodokezwa. Tia moyo wote washiriki katika kampeni ya andikisho, wakitumia toaji zilizofupishwa ili kuanza. Uwe na maonyesho mawili.
Wimbo 148 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 13
Dak 7: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak 18: “Hatujapata Kamwe Kuwa na Hali Nzuri Hivi ya Kiroho!” Maswali na majibu. Uwe na watangazaji wawili au watatu, kutia ndani tineja, wakitaja baadhi ya baraka zao. Malizia kwa kuonyesha jinsi uthamini unaoongezeka unavyotuchochea kwa utendaji wa bidii katika utumishi mtakatifu.
Dak 20: “Nawezaje Kumfanya Mtu Anisikilize?” Maswali na majibu. Uwe na watangazaji wawili wazungumze jinsi wanavyoweza kujaribu kuonyesha uchangamfu zaidi wanapoongea milangoni, wakitumia baadhi ya madokezo yaliyotolewa katika kitabu Kiongozi cha Shule, kurasa 165-167, mafungu 10-21.
Wimbo 193 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 20
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Tia moyo wote washiriki katika ugawanyaji wa magazeti.
Dak 15: “Endelea Kusema Kweli.” Kazia uhitaji wa kufanya ziara za kurudia, mradi ukiwa kuanzisha mafunzo. Uwe na maonyesho mafupi mawili.
Dak 20: Mazungumzo kati ya mzee na mtumishi wa huduma juu ya makala “Familia za Kimungu za Wakati Uliopita—Kigezo cha Siku Zetu,” ipatikanayo kwenye kurasa 20-23 za toleo la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 1995. Kazia matumizi yafaayo ili kunufaisha familia za kwenu.
Wimbo 28 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 27
Dak 5: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: Kutoa Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele Katika Juni. Mwangalizi wa utumishi kwanza azungumza kwa sababu gani kitabu Ujuzi kilitangazwa. Kisha apitia baadhi ya mambo makuu akiwa na watangazaji wawili au watatu wenye uwezo. Kitabu chajibu maswali kuhusu wakati wetu ujao, kuteseka kwa wanadamu, Ufalme wa Mungu, mwenendo wa kimungu, maisha ya familia, na manufaa za sala. Wawili tofauti katika kikundi hicho waonyesha mfikio uwezao kutumiwa kuanzisha funzo katika ziara ya kwanza au ziara ya kurudia. Kisha mwangalizi wa utumishi azungumzia mambo yafuatayo. Kuna uhitaji wa kuongoza mafunzo ya Biblia mengi yenye matokeo kwa wakati mfupi. Kitabu hiki kimetayarishwa kwa kusudi hilo. Hicho hutoa kweli katika njia chanya, yenye usahihi. Maswali yaliyo katika kila fungu, pamoja na yaliyo katika mwisho wa kila sura, yatatusaidia kukazia mambo makuu. Kitabu hicho chatia ndani majibu kwa maswali waulizwayo wapya waliojiweka wakfu wanaotaka kubatizwa. Tia moyo wahubiri wote wawe na mradi wa kuanzisha mafunzo katika Juni.
Dak 10: Sanduku la Swali. Soma na uzungumze na wasikilizaji.
Dak 15: “Je, Una Shughuli Nyingi Mno?” Maswali na majibu. Wakati ukiruhusu, tia ndani maelezo kutoka Amkeni! la Januari 8, 1991, kurasa 14-16. Uwe na mtangazaji mmoja au wawili waeleze kifupi yale ambayo wamefanya ili kukabiliana kwa mafanikio na ratiba ya kitheokrasi yenye shughuli nyingi.
Wimbo 155 na sala ya kumalizia.