Iweni Wenye Kujitoa kwa Nafsi Yote!
1 Tuna sababu nyingi za kuwa wenye shukrani kwa Yehova. Hizi zatia ndani mambo ambayo ametufanyia wakati uliopita, anayotufanyia sasa, na atakayotufanyia wakati ujao. Shukrani zetu zapasa kutuchochea tufanye nini? Zaburi ya Daudi yajibu hivi: “Nitamhimidi BWANA kila wakati, sifa zake zi kinywani mwangu daima.”—Zab. 34:1.
2 Biblia yaonyesha wazi kwamba twaamuriwa kuhubiri. Hii ni kazi tunayofanya “kwa moyo, [“nafsi yote,” NW] kama kwa Bwana.” (Kol. 3:23) Tutafanya kadiri gani katika huduma ikiwa kwelikweli tunajitoa kwa nafsi yote? Tunapofikiria upendo wa Yehova kwetu, hakika mioyo yetu hutuchochea kushiriki kwa kujitoa katika kuwaambia wengine juu yake na makusudi yake yenye thamani! Twachochewa kufanya yale tuwezayo.
3 Lingekuwa jambo lenye kufikiri kuzuri kutazamia mtu anayejitoa kwa nafsi yote atake kukazia uangalifu utumishi mtakatifu. Mtunga-zaburi, ambaye kwa wazi alihisi hivyo, alitangaza: “Mara saba kila siku nakusifu.” (Zab. 119:164) Wale wanaoshiriki hisia za mtunga-zaburi hutafuta fursa za kumtukuza Yehova. Hali zao zinaporuhusu, wao hutumikia kadiri wawezavyo.
4 Tumezungukwa na Fursa za Kumtukuza Yehova: Si lazima tungoje hadi tushiriki katika kazi ya nyumba kwa nyumba ili kuhubiri habari njema. Wafanyakazi wenzetu, wanashule wenzetu, watu wa ukoo, na watu tunaowafahamu wote wanahitaji kusikia ujumbe wa Ufalme. Tunaposafiri, tunaweza kuanzisha mazungumzo yanayoweza kuongoza kwenye kutoa ushahidi kwa wafanyakazi wa hoteli, wafanyakazi wa mkahawa, watumishi wa kituo cha petroli, au madereva wa teksi. Tunapokuwa nyumbani, tunaweza kutolea ushahidi jirani au watu wenye kuleta mizigo. Ikiwa tumelazwa hospitalini, kuna wauguzi, madaktari, na wagonjwa wengine ambao twaweza kuwahubiria kivivi hivi.
5 Ushahidi wa Vivi Hivi Wapata Matokeo: Mashahidi wawili walikuwa wakitembea kwenye bustani siku moja nao wakaanzisha mazungumzo na mwanamume mchanga aliyekuwa akitembea na mtoto wake. Hatimaye yeye na mke wake waliikubali kweli. Huyo mwanamume mchanga baadaye alikiri kwamba muda mfupi tu kabla ya kukutana na Mashahidi hao wawili, alikuwa amesali kwa Mungu, akimwomba, ‘Ikiwa wewe upo, tafadhali uniruhusu kukujua.’ Yeye huona kukutana huko katika bustani kuwa jibu la Yehova kwa sala yake.
6 Wale ambao ni wenye kujitoa kwa nafsi yote katika tamaa yao ya kusaidia wengine kiroho hupata shangwe kubwa zaidi. Wao wanajua kwamba utumishi wa aina hiyo, ‘wa moyo mkamilifu,’ humpendeza Yehova.—1 Nya. 28:9.