Kwa Kufanyiza Fursa za Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi
1 Yesu aliagiza wanafunzi wake waache nuru yao ing’ae. (Mt. 5:14-16) Yeye aliwataka waambie wengine juu ya habari njema za Ufalme wa Mungu kwenye kila pindi iliyofaa. Katika habari hii, Yesu alikuwa kiolezo. Kielelezo cha hilo ni wakati alipotumia fursa ya kunena ukweli kwa mwanamke Msamaria kwenye kisima kimoja katika Sikari. (Yn. 4:5-30) Namna gani sisi? Je! sisi hufanyiza fursa hizo tutoe ushahidi?
2 Si sisi sote tunaoweza kushiriki katika utumishi wa shambani kila siku. Lakini huenda kukawapo pindi karibu kila siku tunapoweza kutoa ushahidi. Kwa njia gani? Kwa kutoa ushahidi wa vivi hivi. Maelfu wengi wamefahamikiana na ukweli katika njia hiyo. Tukiwa chonjo kutambua fursa na kutia jitihada, watu wengi zaidi waweza kufikiwa.
TWAWEZA KUHUBIRI NANI?
3 Kuongezea utoaji wa ushahidi rasmi wa nyumba kwa nyumba, ziara za kurudia, na mafunzo ya Biblia, twaweza kutolea ushahidi wa vivi hivi wafanya kazi wenzi, wanashule wenzi, washiriki wa biashara, watu wa ukoo, na wengine tunaofahamikiana nao. Tunaposafiri kwa basi, gari-moshi, au eropleni, huenda tukaweza kuanzisha mazungumzo pamoja na abiria wenzetu. Tunapokuwa likizoni, huenda tukashiriki habari njema na wafanya kazi wa hoteli na moteli, wafanya kazi wa vituo vya petroli, wafanya kazi wa mkahawa, na madereva wa teksi. Twaweza kuongea na wengine tunaposubiri kwenye ofisi ya daktari au dobi. Tunapokuwa nyumbani, labda twaweza kutolea ushahidi majirani, wauzaji, au matarishi. Hata tukiwa tumelazwa hospitali, twaweza kutolea ushahidi madaktari, wauguzi, na wagonjwa wengine.
JINSI YA KUANZA
4 Tukiwa na miadi nasi tujue tutatumia wakati fulani tukisubiri, twaweza kwenda na magazeti ya karibuni zaidi na kuwa tayari kuzungumza makala fulani yenye upendezi pamoja na mtu tunayekutana naye. Au tungeweza kutumia trakti au broshua kuwa msingi wa kuanzisha mazungumzo. Katika kikao hicho, wengine wameona kuna mafanikio kuanza mazungumzo kwa kutoa taarifa yenye kutazamisha juu ya tukio fulani la wakati huu na kisha kuuliza itikio-tendo la mtu huyo. Wengine wameona kwamba kuuliza swali lenye kuamsha kufikiri kuhusu tukio fulani la wakati huu kwaweza kuongoza kwenye utoaji ushahidi mzuri. Katika visa vyote, uanzilishaji ndio unaohitajiwa ili kuanzisha mambo.
KUTOA USHAHIDI KAZINI
5 Wale wenye kazi za kimwili waweza kufanyiza fursa za kutoa ushahidi kwa wafanya kazi wenzi. Dada wawili katika Georgia walitengeneza orodha ya wafanya kazi wenzao ambao walidhani wangeweza kupendezwa na ukweli. Kwa kuongea na wale waliokuwa kwenye orodha na wengine wachache, waliweza kuangusha vitabu Ufunuo Upeo zaidi ya 65 na kusitawisha upendezi mwingi.
6 Katika kisa kingine, ndugu mmoja aliazimia kwamba angetoa ushahidi kwa mtu wa kwanza ambaye angeketi kando yake wakati wa pumziko lake la dakika 15 kazini. Mwanamume aliyesema naye alijua juu ya ukweli lakini akasema hakutaka kufuatia jambo hilo. Hata hivyo, ndugu yetu aliacha fasihi mahali ambapo mwanamume huyo angeweza kuichukua kwa urahisi. Katika muda wa miezi sita mwanamume huyo na familia yake walikuwa wamebatizwa.
7 Akiwa “nuru ya ulimwengu,” Yesu alifanyiza fursa za kutoa ushahidi wa vivi hivi. (Yn. 8:12) Tukiwa chonjo na wenye nia ya kushiriki tumaini letu lenye msingi wa Biblia, sisi pia hatutakosa fursa za kutoa ushahidi. Kwa hiyo, kama vile wanafunzi wa Yesu, sisi ‘tutang’aa kama wamulikaji katika ulimwengu.’—Flp. 2:15, 16, NW.