Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
1 “Iweni Watu Wafundishwao na Yehova” ndicho kichwa cha programu ya siku ya kusanyiko la pekee. (Yn. 6:45) Ufundishaji wa kimungu kutoka kwa Yehova hutusaidia kuishi maisha yenye kuridhisha. Husitawisha ndani yetu uthamini wenye kina wa urithi wetu wa kiroho. Jitihada zetu za kusaidia wengine wasikie habari njema hutufanya tuwe washiriki wafaao wa jamii. Siku hii ya kusanyiko la pekee itakazia baraka zinazofurahiwa na watu wanaofundishwa na Yehova.
2 Programu hiyo itatofautisha manufaa za ufundishaji wa kimungu na hatari za ufundishaji wa kilimwengu. Tutaona kwa uwazi zaidi jinsi Yehova aandaavyo elimu ya hali ya juu zaidi—elimu inayotegemea Neno lake, Biblia. Maneno matatu ya ibada yatakaziwa ambayo katika hayo sisi hufurahia kufundishwa na Mungu. Kwa kuongezea, vijana watatiwa moyo kuiga vielelezo vyenye kutokeza vya Biblia kama Daudi na Timotheo na kujenga maisha zao kwenye utendaji mwingi wa kiroho. Imani yetu itatiwa nguvu kwa kuwa uaminifu-mshikamanifu wa walio na umri mkubwa pia unakaziwa. Wapya waliojiweka wakfu wanaostahili watabatizwa. Mapema kabla ya siku hiyo ya kusanyiko, wanapaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi kuhusu tamaa hiyo.
3 Hotuba kuu ya siku ya kusanyiko la pekee ni yenye kichwa “Twafundishwa na Yehova Kufanya Mapenzi Yake.” Itakazia sababu sisi sote twahitaji kuendelea kujifunza, ili tuimarishwe katika imani, na kuendelea kufanya maendeleo. Tutasihiwa kumwiga Yehova kwa kufundisha wengine kweli iongozayo kwenye uhai udumuo milele. Mambo yaliyoonwa yenye kujenga yatatiwa ndani kuonyesha jinsi vichapo vya Sosaiti vimesaidia wengi kufundishwa na Yehova. Matimizo yenye manufaa ya programu ya Yehova ya ufundishaji wa tufeni pote yatakaziwa.
4 Fanya mipango hususa ya kuhudhuria. Tia moyo wenye kupendezwa wote wahudhurie. Tazamia kwa hamu kufundishwa mambo mengi mazuri na Mfunzi wetu Mtukufu.—Isa. 30:20.