Twapaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu
1 Imeonwa kwamba “Mashahidi wa Yehova wameeneza kihalisi dunia yote wakitoa ushahidi wao.” Hili limewezekanaje? Si kwa uweza au nguvu ya binadamu, bali kwa roho ya Mungu inayofanya kazi juu ya watumishi wake wanapotumia uandalizi wake mbalimbali wa kutimiza utume wao wa kuhubiri na kufundisha.—Zek. 4:6; Mdo. 1:8.
2 Vichapo ni njia moja yenye matokeo ya kutimiza kazi yetu ya kuhubiri. Kwa miaka kadhaa, mabilioni ya vitabu, vijitabu, broshua, magazeti, na trakti zimechapwa na kugawanywa na Mashahidi wa Yehova ili kusaidia kujulisha habari njema ya Ufalme. Ripoti katika 1997 Yearbook zaonyesha kwamba kutokezwa kwa fasihi kumefikia kiwango kisicho cha kawaida. Hadi sasa, zaidi ya nakala milioni 91 za Biblia New World Translation zimechapwa. Kwa mwaka mmoja hesabu ya magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yaliyochapwa Marekani ilipanda kwa asilimia 7.1. Katika Ujerumani, kutokezwa kwa magazeti kulipanda hadi asilimia 35. Zaidi ya thuluthi moja ya magazeti yaliyotokezwa huko yalikuwa ya shamba la Urusi.
3 Kwa nini fasihi nyingi hivyo zahitajiwa? Ulimwenguni pote, kumekuwa na itikio kubwa zaidi la kitia-moyo tulichopewa cha kutoa ushahidi popote watu wawezapo kupatikana. Wengi wetu tukiongeza kazi yetu ya kutoa ushahidi—hadharani, barabarani, na eneo la biashara—watu wanaoonyesha kupendezwa wanaangushiwa kiasi kikubwa zaidi cha fasihi. Wengi wao walipata fursa mara chache au hawakupata fursa ya kusikia ujumbe wa Ufalme hapo awali. Ili kutimiza uhitaji huu, makutaniko huwa na vichapo mbalimbali vya kutumia katika kila sehemu ya huduma.
4 Mradi Wetu wa Kugawanya Fasihi Ni Nini? Mradi wetu si kuangusha fasihi tu. Utume wa kufanya wanafunzi huhusisha pande mbili—kuhubiri na kufundisha. Kwanza, tuna pendeleo la kuhubiri habari njema ya Ufalme, tukiwajulisha watu kwamba ndiyo tumaini pekee kwa wanadamu. (Mt. 10:7; 24:14) Kulingana na muda ulivyothibitisha, fasihi zetu zenye kutegemea Biblia ni njia yenye matokeo ya kuchochea kupendezwa na kupatia wengine ujuzi juu ya Ufalme.
5 Pili, ikiwa tutafanya wanafunzi, lazima tufundishe mambo yote ambayo Yesu aliamuru. (Mt. 11:1; 28:19, 20) Tena, fasihi hutimiza fungu la maana katika kukaza kikiki ndani ya mioyo ya wanafunzi, kuwasaidia wawe wanafunzi.
6 Wale wanaokubali fasihi wanaweza kuwa ‘wasikiaji wa neno,’ lakini haielekei kwamba watakuwa watekelezaji walo wakiachwa bila kusaidiwa. (Yak. 1:22-25) Isipokuwa waongozwa na mtu, ni wachache watakaopata kuwa wanafunzi. (Mdo. 8:30, 31) Wanahitaji mwalimu wa kuwasaidia wajithibitishe kweli inayopatikana katika Maandiko. (Mdo. 17:2, 3) Mradi wetu ni kuwasaidia wafanye maendeleo kufikia hatua ya wakfu na ubatizo na kuwazoeza wawe na sifa ya ustahili ili wafundishe wengine.—2 Tim. 2:2.
7 Uhitaji Mkubwa Zaidi Ni wa Walimu Zaidi: Tunapohubiri, twatangaza habari njema hadharani. Hata hivyo, kufundisha, huhusisha kuagiza mtu hatua kwa hatua. Ijapokuwa kuhubiri hufanya wengine wajue ujumbe wa Ufalme, kufundisha husaidia watu wakubali habari njema na kutenda kulingana nazo. (Luka 8:15) Mwalimu hufanya mengi zaidi ya kutangaza; yeye hufafanua, husababu kwa hoja nzuri, hutoa ithibati, na husadikisha.
8 Wengi wetu twapaswa kuwa walimu, si wahubiri tu. (Ebr. 5:12a) Kugawanya fasihi ni sehemu muhimu ya kazi yetu, lakini kufikia lengo la pili la huduma yetu mwishowe hutegemea tufanyayo tukiwa walimu. Ijapokuwa huenda tukapendezwa tunapoweza kuangusha fasihi, ili kutimiza huduma yetu kikamili hatupaswi kuona angusho kuwa mradi wetu wa mwisho. (2 Tim. 4:5) Maangusho ni njia yenye matokeo ya kufungua mlango kwenye fursa za kufundisha wengine kweli.
9 Fanya Ziara za Kurudia Ili Kuanzisha Mafunzo ya Biblia: Sisi sote yaelekea tumeangusha vitabu, broshua, na magazeti kadhaa, yakikusanya orodha ya ziara za kurudia. Twapaswa kuratibu wakati wa kawaida wa kurudia ili tuchochee kupendezwa. Kusudi letu kubwa la kurudia si kuangusha fasihi zaidi tu bali kutia moyo watu wasome na kunufaika na kile walicho nacho. Tungefanya maendeleo gani sisi wenyewe ikiwa mtu fulani hangalikuwa amerudia mara kwa mara ili kutusaidia tujipatie ujuzi sahihi?—Yn. 17:3.
10 Fuatia kupendezwa kote ukiwa na maoni ya kuanzisha funzo la Biblia ama katika broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? au katika kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Vichapo hivi viwili hutoa ujumbe wa Ufalme katika namna ambayo ni rahisi kuuelewa. Broshua Anataka ina mtaala mpana wa funzo, ikishughulikia mafundisho ya msingi ya Biblia. Kitabu Ujuzi humwezesha mtu kufundisha kweli kwa kina kikubwa, hata hivyo kwa urahisi, uwazi, na ufupi.
11 Programu iliyofanywa sahili ya kufundisha, kama ilivyoelezwa katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996, hufanya iwe rahisi mwalimu kufundisha na mwanafunzi kujifunza. Weka nakala ya nyongeza yako tayari ili kupitia njia na ufundi wa kufundisha ambao umethibitika kuwa wenye matokeo. Baadhi ya madokezo ambayo hutoa huhusisha jinsi ya kupendezwa kibinafsi na mwanafunzi, kiasi cha habari cha kujifunza katika kipindi kimoja, jinsi ya kushughulika na maswali yasiyohusu somo lenyewe, jinsi mwalimu na mwanafunzi wanavyoweza kujitayarisha mapema kwa ajili ya funzo, na jinsi ya kuelekeza mwanafunzi kwenye tengenezo la Yehova. Kwa kufuata madokezo hayo, wengi wetu, kutia na walio wapya, tutaweza kuongoza mafunzo yenye kufanya maendeleo.
12 Ripoti za Mafanikio Mazuri Kutoka Shambani: Broshua Anataka na kitabu Ujuzi vimethibitika kuwa visaidizi vyenye kuharakisha utaratibu wa kufanya wanafunzi. Alipopata broshua Anataka, ndugu mmoja katika Bolivia mara moja aliitumia kuanzisha funzo na mwanamume mmoja. Miezi minne baadaye kwenye mkusanyiko wa wilaya, mwanafunzi huyu alikuwa miongoni mwa wataka-kubatizwa wenye furaha! Tulisikia mambo kama hayo yaliyoonwa kwenye makusanyiko yaliyofanywa Bukoba, Tanzania; Mombasa, Kenya na sehemu nyinginezo.
13 Wengi wanachochewa kuweka maisha zao wakfu kwa Yehova baada ya kumaliza funzo la kitabu Ujuzi. Katika kutaniko moja Angola, idadi ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa na wanafunzi iliongezeka kutoka 190 hadi 260 na hudhurio la mikutano likawa maradufu katika hesabu kutoka 180 hadi 360 kwa miezi minne tu baada ya kitabu Ujuzi kuanza kutumiwa katika eneo hilo. Muda mfupi baada ya hapo, ililazimu kuanzisha kutaniko jingine.
14 Baada ya kuanzisha funzo lake katika kitabu Ujuzi, ndugu mmoja alisema kwamba kuliongoza ni “sahili ikiwa mwenye kuongoza auliza tu maswali, kusoma maandiko kadhaa yatumikayo, na kuhakikisha kwamba mwanafunzi anaelewa.” Ijapokuwa sikuzote alifikiri kwamba ni wahubiri wenye sifa ya ustahili tu ndio wangeweza kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo na kwamba hangeweza kamwe kufanya hivyo, alitambua kwamba angeweza, akisema: “Ikiwa naweza, mtu yeyote anaweza.”
15 Ni kwa kuongoza mafunzo ya Biblia yakiwa sehemu ya huduma yetu kwamba twatimiza lengo la kufanya wanafunzi. Wale ambao wamesitawisha uwezo wa kushiriki sehemu hii ya huduma wanaiona kuwa yenye kutosheleza na yenye kuthawabisha sana. Na isemwe juu yetu kwamba sisi pia “[twa]hubiri ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yahusuyo Bwana Yesu Kristo kwa uhuru wa usemi ulio mkubwa zaidi sana.”—Mdo. 28:31.