Ukipata Matokeo, Utumie!
1 Huduma ya Ufalme Yetu hutuandalia kwa kuendelea utoaji mbalimbali uliopendekezwa tutumie katika huduma. Huo hutupa mawazo mapya ya jinsi ya kutokeza kupendezwa katika ujumbe wa Ufalme. Huenda ukawa unafanya jitihada kila mwezi ujifunze utoaji mmoja au zaidi kati ya hizo. Hata hivyo, baadhi ya wahubiri huenda wakaona kwamba wakati ambapo wametumia moja ya hizo mara chache, toleo jingine la Huduma ya Ufalme Yetu limeandaa utoaji mpya mbalimbali. Ni wazi huenda isiwezekane kwa kila mtu kujifunza utoaji mpya kabla ya kuwa stadi wa kutumia ule wa kwanza.
2 Bila shaka, kuna maelfu ya mapainia na wahubiri wengine ambao hutumia wakati mwingi katika utumishi wa shambani. Zaidi ya hayo, makutaniko mengi hufanya eneo lao lote kila baada ya majuma machache. Katika hali hizi, wahubiri huthamini kuwa na mifikio mipya na mawazo mapya ya kuutoa ujumbe. Hilo huwasaidia waboreshe stadi zao. Pia hufanya huduma yao ipendeze na iwe yenye matokeo zaidi na huwasaidia kutimiza magumu yanayokabiliwa.
3 Kwa vyovyote, ikiwa umetayarisha utoaji ulio na matokeo, katika kusitawisha kupendezwa, endelea kuutumia! Hakuna lazima ya kuacha kuendelea kutumia utoaji wenye matokeo unaokuwa na matokeo. Upatanishe tu na toleo la fasihi la mwezi wa wakati uliopo. Unapopitia madokezo yaliyotolewa katika Huduma ya Ufalme Yetu, tafuta mambo yenye kupendeza ambayo huenda ukataka kuyaingiza katika utoaji wako.
4 Kwa hiyo upokeapo toleo jipya la Huduma ya Ufalme Yetu, kumbuka kwamba utoaji mbalimbali uliomo ndani yake ni madokezo tu. Ukiweza kuyatumia, sawa. Lakini kama tayari umepata utoaji unaopata matokeo katika eneo lako, utumie! Jambo la maana ni “[ku]timiza kikamili huduma yako” kwa njia ifaayo, ukipata wenye kustahili na kuwasaidia wawe wanafunzi.—2 Tim. 4:5.