Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Februari 2
  • Juma Linaloanza Februari 9
  • Juma Linaloanza Februari 16
  • Juma Linaloanza Februari 23
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 2/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari

Juma Linaloanza Februari 2

Wimbo 166

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: “Mashahidi wa Yehova—Waeneza-Evanjeli wa Kweli.” Maswali na majibu. Pitia sanduku lililo kwenye ukurasa wa 19 katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1992.

Dak. 20: “Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na Kiu.” Pitia makala, ukionyesha jinsi ambavyo madokezo ya utoaji mbalimbali yamekusudiwa kuchochea upendezi na kuwachochea wasikilizaji. Panga mtu mzima atoe wonyesho wa fungu la 2-3 au la 4-5 na kijana atoe wonyesho wa fungu la 6.

Wimbo 208 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 9

Wimbo 96

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini Zote.” (Fungu la 1-10) Maswali na majibu. Orodhesha lugha zisemwazo na wengi katika eneo lenu, na uonyeshe ni fasihi gani za lugha hizo ambazo kutaniko linazo akibani. Kama ilivyoelezwa katika fungu la 10, panga mtu atoe wonyesho wa kutumia kijitabu Good News for All Nations.

Wimbo 220 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 16

Wimbo 75

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 12: Sababu kwa Nini Wahitaji Kuhudhuria Mikutano ya Kutaniko. Mzee azungumzia mambo makuu yaliyo katika Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1993, ukurasa wa 8-11, akikazia umaana wa kuhudhuria mikutano yote kwa ukawaida.

Dak. 18: “Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini Zote.” (Fungu la 11-28) Maswali na majibu. Orodhesha ni dini zipi zisizo za Kikristo zilizo katika eneo lenu. Panga mhubiri mwenye uzoefu atoe wonyesho wa jinsi ya kutoa ushahidi mara ya kwanza kwa mtu ambaye ni Mbuddha, Mhindu, Myahudi, au Mwislamu—yoyote iliyoenea sana kwenu.

Dak. 10: “Yehova Ni Msaidiaji Wangu.” Hotuba changamfu, yenye kutia moyo itolewe na mzee.

Wimbo 15 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 23

Wimbo 4

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia toleo la fasihi la Machi. Taja wazo moja au mawili ya kutoa kitabu Ujuzi, ukitumia mambo kadhaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1996, ukurasa wa 4. Kazia mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani.

Dak. 15: “Ukipata Matokeo, Utumie!” Maswali na majibu. Panga mhubiri mmoja au wawili wazoefu kutoka kwa wasikilizaji watoe maelezo kifupi juu ya utoaji mbalimbali ambao wameendelea kuutumia kwa sababu ya usahili wa utoaji huo mbalimbali na matokeo yake. Kisha wengine washiriki mifikio iliyodokezwa hivi karibuni ambayo ilikuwa katika Huduma ya Ufalme Yetu na ambayo imethibitika kuwa yenye matokeo.

Dak. 20: Jizoeze Utoaji Wako Mbalimbali. Hotuba fupi ikitegemea kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 98-99, fungu la 8-9. Kazia uhitaji wa kuchanganua utoaji wetu mbalimbali na kutafuta njia za kuwa wenye matokeo zaidi. Panga dada wawili watoe wonyesho wa jinsi wao huchanganua walilofanya mlangoni, wakizungumza juu ya jinsi wanavyoweza kufanyia maendeleo jambo hilo. Pia wanakuwa na kipindi kifupi cha mazoezi kujaribu utoaji mmoja wanaopanga kuutumia wakati ufuatao, wakipeana madokezo yenye kusaidia. Mwenyekiti amalizia kwa kutia wote moyo wachanganue na kujizoeza utoaji wao mbalimbali.

Wimbo 103 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki