Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/98 uku. 1
  • Mashahidi wa Yehova —Waeneza-Evanjeli wa Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova —Waeneza-Evanjeli wa Kweli
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • “Fanya Kazi ya Mweneza-injili”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Je! Wewe Unayo Roho ya Kueneza Injili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Uenezaji wa Evanjeli—Mahali Pao Katika Ibada ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Ni Nani Ambao Ndio Waeneza-Evanjeli wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 2/98 uku. 1

Mashahidi wa Yehova —Waeneza-Evanjeli wa Kweli

1 Yesu Kristo aliwekea wanafunzi wake wote daraka la kueneza evanjeli, akiwaelekeza kihususa wahubiri habari njema za Ufalme. (Mt. 24:14; Mdo. 10:42) Wanafunzi wake wa mapema waliweka kiolezo katika jambo hili waliposema juu ya Ufalme bila kuacha—si katika mahali pa ibada tu bali popote walipokuta watu hadharani na wakienda nyumba hadi nyumba. (Mdo. 5:42; 20:20) Tukiwa Mashahidi wa Yehova leo, tumejithibitisha kuwa Wakristo waeneza-evanjeli wa kweli, tukihubiri ujumbe wa Ufalme katika nchi 232 na kubatiza wanafunzi wapya zaidi ya milioni moja kwa miaka mitatu tu iliyopita! Kwa nini kazi yetu ya kueneza evanjeli imekuwa yenye mafanikio sana?

2 Habari Njema Hutusisimua: Waeneza-evanjeli ni wahubiri, au wajumbe, wa habari njema. Tukiwa hivyo, tuna pendeleo lenye kusisimua la kutangaza Ufalme wa Yehova—habari njema halisi pekee iwezayo kutolewa jamii ya binadamu yenye msononeko. Twachangamkia ujuzi wa mapema ambao tumepata juu ya mbingu mpya ambazo zitatawala kwa uadilifu dunia mpya inayofanyizwa na wanadamu waaminifu, katika Paradiso ijayo. (2 Pet. 3:13, 17) Ni sisi tu ambao tumelikubali tumaini hili, nasi tuna hamu ya kulishiriki na wengine.

3 Upendo wa Kweli Hutuchochea: Kazi ya kueneza evanjeli ni ya kuokoa uhai. (Rom. 1:16) Ndiyo sababu sisi huona shangwe kubwa katika kueneza ujumbe wa Ufalme. Tukiwa waeneza-evanjeli wa kweli, twawapenda watu, na hilo hutuchochea kushiriki habari njema nao—familia zetu, jirani zetu, wajuani wetu, na wengine wengi iwezekanavyo. Kufanya kazi hiyo kwa nafsi yote ni mojawapo ya wonyesho mzuri zaidi tuwezao kutoa wa upendo wetu kwa wengine.—1 The. 2:8.

4 Roho ya Mungu Hututegemeza: Neno la Mungu hutuhakikishia kwamba tufanyapo kazi yetu ya kupanda na kutia maji mbegu ya Ufalme, Yehova ndiye “aikuzaye.” Hilo hasa ndilo jambo tuonalo likitukia katika tengenezo letu leo. (1 Kor. 3:5-7) Roho ya Mungu ndiyo hututegemeza katika utendaji wetu wa kueneza evanjeli nayo hutupa mafanikio makubwa.—Yoe. 2:28, 29.

5 Kwa kufikiria kitia-moyo kilicho kwenye 2 Timotheo 4:5 cha “[ku]fanya kazi ya mweneza-evanjeli,” na kwa sababu ya upendo wetu kwa watu wote, na tuchochewe kushiriki habari njema ya Ufalme yenye kusisimua kwenye kila fursa, tukiwa na uhakika wa kwamba Yehova ataendelea kubariki kazi yetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki