Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 3
  • Juma Linaloanza Agosti 10
  • Juma Linaloanza Agosti 17
  • Juma Linaloanza Agosti 24
  • Juma Linaloanza Agosti 31
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 8/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Juma Linaloanza Agosti 3

Wimbo 216

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Eleza ripoti ya utumishi wa shambani ya Aprili ya nchi na ya kutaniko la kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: “Je, Agosti Utakuwa Mwezi Muhimu?” Maswali na majibu. Tia moyo kila mtu ashiriki katika huduma mwezi wa Agosti na kila mwezi wa mwaka mpya wa utumishi.

Dak. 20: “Tumia Broshua Uvutie Akili na Moyo.” Mazungumzo na wasikilizaji. Pitia kifupi broshua ambazo zimechapishwa kwa miaka kadhaa kujulisha watu mambo ya maana ya Kimaandiko. (Ona Watch Tower Publications Index 1986-1995, ukurasa wa 652-653.) Kazia broshua za karibuni, na uzungumzie ni nani ambaye huenda akapendezwa kupata moja ya hizo. Toa wonyesho mmoja au mawili.

Wimbo 191 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 10

Wimbo 127

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Taja mradi wa wahubiri wote kushiriki katika huduma ya shambani katika Agosti.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Vijana—Tumieni kwa Manufaa Masomo Yenu.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo yanayofaa kutoka Amkeni!, Aprili 8, 1992, (Kiingereza) ukurasa wa 17-19, na Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1991, ukurasa wa 23-26.

Wimbo 37 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 17

Wimbo 163

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Alika watu watoe maelezo mafupi juu ya jinsi ya kupata jina na anwani ya mtu ambaye ametolewa ushahidi barabarani, bustanini, au penginepo ili kufuatia kupendezwa alikoonyesha.

Dak. 35: “Uchunguzi Wenye Kuendelea wa Kazi Yenye Uharaka ya Kufanya Wanafunzi.” Maswali na majibu. Soma fungu la 5, 10, na 11. Pitia jinsi kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia inavyoendelea kwenu. Watie moyo wote wanaoongoza mafunzo ya Biblia wasome nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996 tena ili kuboresha stadi zao za kufundisha. Chunguzeni fungu la 5 na la 25 la nyongeza hiyo.

Wimbo 108 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 24

Wimbo 213

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Chunguzeni sanduku lenye kichwa “28,500!” katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1998. Kukiwa na mwisho-juma mmoja tu uliobaki katika Agosti, tia moyo kila mtu ashiriki katika huduma kabla ya mwezi kwisha. Pitia “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.”

Dak. 18: Jinsi ya Kudumu Katika Utumishi wa Painia. Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1993, ukurasa wa 28-31. Hoji painia ambaye amejifunza kukabiliana na matatizo makubwa naye aendelea kupainia.

Dak. 15: Tumia Vizuri Huduma ya Ufalme Yetu. Mazungumzo na wasikilizaji. Ukitumia mifano ya karibuni, toa kielezi cha habari ya wakati ufaao inayopatikana katika kurasa za Huduma ya Ufalme Yetu na manufaa tupatazo kutokana nayo: (1) makala zituchocheazo kushiriki kwa ukawaida katika huduma; (2) mambo yaliyoonwa ambayo hutusaidia katika utumishi mtakatifu; (3) madokezo ambayo hutusaidia kutoa habari njema kwa matokeo; (4) matangazo ya vichapo vipya vinavyopatikana ambavyo ni vyenye mafaa katika eneo la kwetu; (5) ripoti za utumishi, ambazo huonyesha mwendo wa utendaji wa Ufalme; (6) Habari za Kitheokrasi, ambazo huripoti maendeleo ya kazi ya ulimwenguni pote; (7) matangazo na ratiba ambazo hutujulisha juu ya matukio ya karibuni; (8) Masanduku ya Maswali ambayo hujibu mambo ya kuhangaikiwa kwa uzito; na (9) nyongeza ambazo hutuambia juu ya mikusanyiko, kampeni za pekee, na mambo mengine yanayotufanya tukazie fikira mahitaji yetu ya kiroho. Watie moyo wote wasome kila toleo, watumie madokezo yake, na kuileta kwenye Mikutano ya Utumishi na mikutano ya utumishi wa shambani, na kuiweka katika faili ya kibinafsi ili kuirejezea wakati ujao.

Wimbo 210 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 31

Wimbo 65

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti ya utumishi ya Agosti. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wapaswa kuuliza kila mmoja katika kikundi chao ili ripoti zote ziweze kuhesabiwa Septemba 6. Chunguzeni toleo la fasihi la Septemba. Toa wonyesho kifupi unaotokeza swali hili, “Kwa nini tutumie jina la Mungu?” Lijibu ukitumia kitabu Ujuzi, sura ya 3, fungu la 6.

Dak. 15: “Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi-Msimamizi.” Hotuba itolewe na mwangalizi-msimamizi. Baada ya kupitia wajibu wake, aeleza uthamini wake kwa kutaniko kwa kushirikiana na wazee wanapochunga kundi.

Dak. 18: Saidia Mtoto Wako Akabili Matatizo ya Shuleni. Mzee awa na mazungumzo na wazazi wawili au watatu ambao wana watoto shuleni. Taja kifupi baadhi ya matatizo ya kawaida zaidi ambayo watoto hukabili, kama ionyeshwavyo katika Amkeni!, Agosti 8, 1994, ukurasa wa 5-7. Kisha ukirejezea ukurasa wa 8-10, zungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kulinda watoto wao na kudumisha mahusiano mazuri kati ya wazazi na walimu.

Wimbo 24 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki