Mikutano Ya Utumishi Kwa Oktoba
TAARIFA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mkutano wa Utumishi kwa kila juma wakati wa miezi ya mkusanyiko. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho yahitajiwayo ili kuruhusu uhudhuriaji wa Mkusanyiko “Njia ya Mungu ya Maisha” na kwa ajili ya pitio la dakika 30 la mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma lifuatalo. Pitio la siku kwa siku la programu ya mkusanyiko wa wilaya lapasa kugawiwa mapema ndugu watatu wenye sifa za ustahili ambao wataweza kukazia mambo makuu yenye kutokeza. Pitio hili lililotayarishwa vizuri litasaidia kutaniko likumbuke mambo makuu ya kutumia kibinafsi na shambani. Maelezo kutoka kwa wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yaliyosimuliwa yapaswa yawe mafupi na ya moja kwa moja.
Juma Linaloanza Oktoba 5
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 10: Wana Roho Changamfu ya Upainia. Hotuba yenye kutia moyo ikitegemea kichapo 1998 Yearbook, ukurasa wa 104-107. Eleza ni kwa nini kuna mapainia wengi sana Japani, kile ambacho hufanya wake huko watangulize masilahi ya kiroho, kile ambacho huchochea upainia, na ni nani walio wengi kati ya mapainia hao. Toa kielezi cha uvutano unaodhihirishwa na wazazi walio mapainia. Kazia ni usadikisho gani ambao huhitajika ili kufanya marekebisho ya lazima katika maisha ya mtu ili kupainia. Watie moyo wote wafikirie kwa uzito, kwa njia ya sala nao wachunguze matarajio yao ya kupainia.
Dak. 15: “Je, Wewe Huyasoma Magazeti?” Maswali na majibu. Pitia madokezo yatumikayo ya kuratibu wakati wa kusoma kibinafsi yanayopatikana katika kitabu Kiongozi cha Shule, somo la 4, fungu la 5-6.
Dak. 15: “‘Kupanda Mbegu za Ufalme’ kwa Kupelekea Watu Magazeti kwa Ukawaida.” Mazungumzo na wasikilizaji. Panga wahubiri kadhaa waeleze jinsi walivyoanza na walivyodumisha kupelekea watu magazeti kwa ukawaida. Kisha toa wonyesho wa utoaji wa gazeti mahali ambapo mipango imefanywa ya kurudi ukiwa na matoleo yafuatayo. Kazia uhitaji wa wahubiri wote kuwa na agizo hususa la magazeti ili wawe na ugavi wa kutosha.
Wimbo 133 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 12
Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 13: “Waangalizi Wanaoongoza—Mwandishi.” Hotuba itolewe na mwandishi wa kutaniko, akipitia wajibu wake mbalimbali aliogawiwa. Akazia kwamba wote wanaweza kushirikiana naye kwa kutoa ripoti za utumishi wa shambani bila kukawia.
Dak. 25: “‘Njia ya Mungu ya Maisha’ Mkusanyiko wa Wilaya na wa Kimataifa wa 1998.” (Fungu la 1-17) Maswali na majibu. Soma fungu la 11 na 12. Kazia umaana wa Kimaandiko wa kudumisha kwa uangalifu sura yetu ya kiasi ya Kikristo na mwenendo na kusimamia vizuri watoto wetu.
Wimbo 107 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 19
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo ya kuzungumziwa katika matoleo ya karibuni ya magazeti. Simulia mambo yaliyoonwa yaliyo katika kichapo 1997 Yearbook, ukurasa wa 45, na Amkeni!, Oktoba 22, 1996, ukurasa wa 32. Watie moyo wote washiriki kugawanya magazeti mwisho-juma huu.
Dak. 15: Jinsi ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Funzo la Mnara wa Mlinzi. Mazungumzo na wasikilizaji yakiongozwa na kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi, yakitegemea Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1986, ukurasa wa 19-20, fungu la 16-18 na kitabu Kiongozi cha Shule, somo la 7, fungu la 11, na somo la 18, fungu la 4-6. Omba maelezo juu ya maswali yafuatayo: (1) Kwa nini ni muhimu kupata manufaa nyingi kutokana na kila toleo la Mnara wa Mlinzi? (2) Tufanye nini tupokeapo toleo jipya? (3) Ni njia gani nzuri ya kujitayarisha kwa ajili ya Funzo la Mnara wa Mlinzi? (4) Maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa yapaswa kupewa uangalifu gani? (5) Twaweza kupitiaje yale ambayo tumejifunza? (6) Twapaswa kutafakari mambo gani makuu tunapomalizia funzo letu la kibinafsi juu ya somo fulani? (7) Tutayarishe maelezo namna gani? (8) Maelezo mbalimbali yaweza kutolewaje kwa swali moja? Panga wengine wasimulie yale ambayo wao binafsi wamefanya yawasaidie kupata manufaa nyingi zaidi kutokana na Funzo la Mnara wa Mlinzi.—Ona pia kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, ukurasa wa 65-67.
Dak. 22: “‘Njia ya Mungu ya Maisha’ Mkusanyiko wa Wilaya na wa Kimataifa wa 1998.” (Fungu la 18-24) Maswali na majibu. Soma fungu la 18 na maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa. Kazia uhitaji wa utaratibu na kuwafikiria wengine, hasa inapohusu kuketi. Malizia kwa hotuba fupi inayopitia “Vikumbusho vya Mkusanyiko.”
Wimbo 95 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 26
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Orodhesha vichapo vya zamani ambavyo viko akibani kwenu na ambavyo vyaweza kutolewa katika huduma fursa itokeapo. Kwa kuwa kuna vipindi vya likizo vinavyokuja Desemba, huu ungekuwa wakati mzuri kwa vijana waliobatizwa na wengine kufikiria kufanya upainia-msaidizi.
Dak. 20: Utii wa Kimungu Katika Familia Iliyogawanyika Kidini. Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Juni 1, 1995, ukurasa wa 26-29. Toa kitia-moyo chenye fadhili na onyo la upole ambalo litasaidia wale walio na wenzi wasioamini wadumishe mtazamo unaofaa na kushirikiana kwa ukawaida na kutaniko.
Dak. 15: Kufika Mikutanoni kwa Wakati. Mazungumzo na viongozi wawili au watatu wa Funzo la Kitabu la Kutaniko au watumishi wa huduma kuhusu tatizo la kuchelewa kwenye mikutano. Wanakiri kwamba hali zisizo za kawaida, kutia ndani dharura, hali za hewa, msongamano wa magari, na kadhalika, zaweza kumfanya mtu yeyote achelewe. Hata hivyo, wengine huwa na mazoea ya kuchelewa. Kwa njia yenye kujenga, kikundi hicho chazungumza na kutoa vielezi kuhusu kinachohitajiwa ili kuwahi: (1) uthamini wa moyo wote wa pendeleo la kuhudhuria mikutano na wa chakula cha kiroho na ushirika unaopatikana huko, (2) mpango mzuri wa mapema wa mambo ya kibinafsi, (3) nia ya kushirikiana miongoni mwa washiriki wa familia, (4) kuondoka mapema na kuruhusu wakati wa matatizo yasiyotazamiwa, na (5) kujali kikweli kutosababisha vikengeusha-fikira kwa wale wengine wanaohudhuria. Wote wakubali kwamba tatizo hili la kuchelewa laweza kumalizwa kwa kuendelea kujitahidi kufanya maendeleo.
Wimbo 86 na sala ya kumalizia.