Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 1999
Maagizo
Wakati wa 1999, ifuatayo itakuwa ndiyo mipango wakati wa kuongoza Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.
VYANZO VYA HABARI: Migawo itategemea Biblia, Mnara wa Mlinzi [w-SW], Amkeni! [g-SW], “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Chapa ya 1990) [si-SW], Siri ya Kupata Furaha ya Familia [fy-SW], na “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vipatikanavyo katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya [td-SW].
Shule yapaswa kuanza KWA WAKATI kwa wimbo, sala, na maneno ya kukaribisha kisha kuendelea kama ifuatavyo:
MGAWO NA. 1: Dakika 15. Huu wapasa ushughulikiwe na mzee au mtumishi wa huduma, nao utategemea Mnara wa Mlinzi, Amkeni!, au “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Unapotegemea Mnara wa Mlinzi au Amkeni!, mgawo huu wapasa kutolewa ukiwa hotuba ya maagizo ya dakika 15 bila pitio la mdomo; unapotegemea kitabu “Kila Andiko,” wapasa kutolewa ukiwa hotuba ya maagizo ya dakika 10 hadi 12 kukiwa na pitio la mdomo la dakika 3 hadi 5, kwa kutumia maswali yaliyochapwa katika kichapo hicho. Lengo lapaswa kuwa si kuzungumza juu ya habari hiyo tu bali pia kuvuta fikira kwenye thamani inayotumika ya habari inayozungumziwa, ukikazia yale yatakayokuwa yenye msaada zaidi kwa kutaniko. Kichwa kilichoonyeshwa chapasa kitumiwe.
Ndugu wanaogawiwa hotuba hii wapaswa kuwa waangalifu wasipite wakati uliowekwa. Shauri la faragha likitolewa, maandishi yafaayo yapaswa kuandikwa kwenye kikaratasi cha shauri.
MAMBO MAKUU KUTOKANA NA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 6. Huu wapasa ushughulikiwe na mzee au mtumishi wa huduma atakayeitumia habari vya kufaa kuhusu mahitaji ya kwao. Huu haupaswi kuwa muhtasari tu wa usomaji uliogawiwa. Pitio la ujumla la sekunde 30 hadi 60 la sura ambazo zimegawiwa laweza kutiwa ndani. Hata hivyo, lengo hasa ni kuwasaidia wasikilizaji wathamini ni kwa nini na ni jinsi gani hiyo habari ni yenye thamani kwetu. Ndipo wanafunzi watakaporuhusiwa na mwangalizi wa shule waende kwenye madarasa yao mbalimbali.
MGAWO NA. 2: Dakika 5. Huu ni usomaji wa Biblia wa habari iliyo mgawo utakaotolewa na ndugu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa katika shule kuu na pia katika shule mbalimbali. Kwa kawaida migawo ya kusoma ni mifupi vya kutosha kuruhusu wanafunzi watoe habari yenye maelezo mafupi katika utangulizi na maelezo yake ya kumalizia. Mandhari-nyuma ya kihistoria, maana ya kiunabii au ya kimafundisho, na matumizi ya kanuni yaweza kutiwa ndani. Mistari yote iliyogawiwa yapasa isomwe bila kukatizwa. Bila shaka, wakati mistari inayopasa kusomwa haifuatani mfululizo, mwanafunzi aweza kutaja mstari ambao usomaji waendelea.
MGAWO NA. 3: Dakika 5. Dada atagawiwa mgawo huu. Habari za utoaji huu zitategemea kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia au “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vipatikanavyo katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Kikao chaweza kuwa utoaji wa ushahidi wa vivi hivi, ziara ya kurudia, funzo la Biblia nyumbani, au sehemu nyingineyo ya utumishi wa shambani. Katika visa vingine, kikao chaweza kutia ndani mzazi anayeshiriki habari fulani na mtoto mdogo. Wenye kushiriki wanaweza wakawa ama wameketi ama wamesimama. Mwangalizi wa shule atapendezwa hasa na vile mwanafunzi amsaidiavyo mwenye nyumba au mtoto asababu kuhusu habari hiyo na kuelewa jinsi maandiko yanavyotumiwa. Mwanafunzi aliyegawiwa sehemu hii apaswa awe anajua kusoma. Msaidizi mmoja ataratibiwa na mwangalizi wa shule, lakini msaidizi wa ziada aweza kutumiwa. Mwanafunzi anaweza kuamua kama mwenye nyumba atasoma mafungu kadhaa wanapochunguza kitabu Furaha ya Familia. Si kikao kinachopasa kupewa uangalifu mkuu, bali ni matumizi ya habari yenye matokeo.
MGAWO NA. 4: Dakika 5. Mgawo huu unapotegemea habari katika “Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo” kama vipatikanavyo katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, utagawiwa ndugu au dada. Unapotegemea kitabu Furaha ya Familia, utagawiwa ndugu. Kwa kila mgawo kumewekwa kichwa katika ratiba. Unapogawiwa ndugu, huu wapaswa uwe hotuba kwa wasikilizaji wote. Kwa kawaida itafaa zaidi kwa huyo ndugu kutayarisha hotuba yake akifikiria wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme ili iwe yenye kuarifu na kunufaisha kikweli wale wanaoisikia hasa. Dada anapopewa sehemu hii, yapasa itolewe kama vile ilivyoonyeshwa kwa Mgawo Na. 3.
*RATIBA YA KUONGEZEA YA USOMAJI WA BIBLIA: Hii imeongezwa katika mabano baada ya namba ya wimbo ya kila juma. Kwa kufuata ratiba hii, kusoma karibu kurasa kumi kila juma, Biblia yote nzima yaweza kusomwa kwa miaka mitatu. Sehemu katika programu ya shule au pitio la kuandika hazitegemei ratiba ya kuongezea ya usomaji.
TAARIFA: Kwa habari ya kuongezea na maagizo kuhusu shauri, wakati, mapitio ya kuandika, na utayarishaji wa migawo, tafadhali ona ukurasa wa 3 wa Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1996.
RATIBA
Jan. 4 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 16-18
Wimbo Na. 23 [*2 Wafalme 16-19]
Na. 1: Jinsi Ambavyo Mungu Alipulizia Biblia (w97-SW 6/15 uku. 4-8)
Na. 2: Ufunuo 16:1-16
Na. 3: Mlinde Mtoto Wako Dhidi ya Madhara (fy-SW uku. 61-63 fu. 24-28)
Na. 4: td-SW 17A Wakristo wa Kweli Ni Lazima Watoe Ushahidi
Jan. 11 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 19-22
Wimbo Na. 126 [*2 Wafalme 20-25]
Na. 1: Ufunuo—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW uku. 268-269 fu. 28-34)
Na. 2: Ufunuo 22:1-15
Na. 3: Wazazi—Dumisheni Njia za Uwasiliano Zikiwa Wazi (fy-SW uku. 64-66 fu. 1-7)
Na. 4: td-SW 17B Sababu Ambayo Hutufanya Tuendelee Kutembelea Watu
Jan. 18 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 1-3
Wimbo Na. 84 [*1 Mambo ya Nyakati 1-6]
Na. 1: Utangulizi kwa Mwanzo (si-SW uku. 13-14 fu. 1-8)
Na. 2: Mwanzo 1:1-13
Na. 3: Fundisha Watoto Kanuni za Kiadili na za Kiroho (fy-SW uku. 67-70 fu. 8-14)
Na. 4: td-SW 26B Lazima Wakristo Waheshimu Kanuni ya Ukichwa
Jan. 25 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 4-6
Wimbo Na. 66 [*1 Mambo ya Nyakati 7-13]
Na. 1: Jihadhari na Kuhesabia Nia Mbaya (w97-SW 5/15 uku. 26-29)
Na. 2: Mwanzo 4:1-16
Na. 3: Umuhimu wa Nidhamu na Staha (fy-SW uku. 71-72 fu. 15-18)
Na. 4: td-SW 3A Dhambi Ni Nini?
Feb. 1 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 7-9
Wimbo Na. 108 [*1 Mambo ya Nyakati 14-21]
Na. 1: Simulizi la Biblia Kuhusu Furiko Ni la Kweli (g97-SW 2/8 uku. 26-27)
Na. 2: Mwanzo 7:1-16
Na. 3: Fundisha Watoto Maoni ya Kimungu Kuhusu Kazi na Mchezo (fy-SW uku. 72-75 fu. 19-25)
Na. 4: td-SW 2B Kumtii Mungu Ni Muhimu
Feb. 8 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 10-12
Wimbo Na. 132 [*1 Mambo ya Nyakati 22-29]
Na. 1: Kweli Kuhusu Kusema Uwongo (g97-SW 2/22 uku. 17-19)
Na. 2: Mwanzo 12:1-20
Na. 3: Uasi wa Mtoto na Mambo Yanayousababisha (fy-SW uku. 76-79 fu. 1-8)
Na. 4: td-SW 30A Maana ya “Mwisho wa Ulimwengu”
Feb. 15 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 13-15
Wimbo Na. 49 [*2 Mambo ya Nyakati 1-8]
Na. 1: Udhaifu wa Kibinadamu Hutukuza Nguvu za Yehova (w97-SW 6/1 uku. 24-27)
Na. 2: Mwanzo 14:8-20
Na. 3: td-SW 38A Taabu za Ulimwengu Haziletwi na Mungu
Na. 4: Usiwe Mwenye Uendekevu au Mwenye Uzuifu Kupita Kiasi (fy-SW uku. 80-82 fu. 9-13)
Feb. 22 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 16-19
Wimbo Na. 188 [*2 Mambo ya Nyakati 9-17]
Na. 1: Kinachofunuliwa na Sala Zako (w97-SW 7/1 uku. 27-30)
Na. 2: Mwanzo 18:1-15
Na. 3: Kutimiza Mahitaji ya Msingi ya Mtoto Wako Kwaweza Kuzuia Uasi (fy-SW uku. 82-85 fu. 14-18)
Na. 4: td-SW 38B Sababu ya Mungu Kuruhusu Uovu
Mac. 1 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 20-23
Wimbo Na. 54 [*2 Mambo ya Nyakati 18-24]
Na. 1: Jinsi ya Kuizoeza Dhamiri Yako (w97-SW 8/1 uku. 4-6)
Na. 2: Mwanzo 23:1-13
Na. 3: td-SW 43C Sifa Nzuri Ajabu za Yehova
Na. 4: Njia za Kusaidia Mtoto Anayekosea (fy-SW uku. 85-87 fu. 19-23)
Mac. 8 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 24-25
Wimbo Na. 121 [*2 Mambo ya Nyakati 25-31]
Na. 1: Kweli Hutuweka Huru na Nini? (w97-SW 2/1 uku. 4-7)
Na. 2: Mwanzo 24:1-4, 10-21
Na. 3: td-SW 43D Si Wote Wanaotumikia Mungu Yuleyule
Na. 4: Kushughulika na Mwasi Aliyeazimia (fy-SW uku. 87-89 fu. 24-27)
Mac. 15 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 26-28
Wimbo Na. 197 [*2 Mambo ya Nyakati 32-36]
Na. 1: Mahali pa Muziki Katika Ibada ya Kisasa (w97-SW 2/1 uku. 24-28)
Na. 2: Mwanzo 26:1-14
Na. 3: Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu (fy-SW uku. 90-92 fu. 1-7)
Na. 4: td-SW 10A Ibilisi Ni Mtu Halisi
Mac. 22 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 29-31
Na. 1: Dunia Haitachomwa Moto (g97-SW 1/8 uku. 26-27)
Na. 2: Mwanzo 31:1-18
Na. 3: td-SW 13A Sababu ya Wanadamu Kufa
Na. 4: Maoni ya Mungu Juu ya Ngono (fy-SW uku. 92-94 fu. 8-13)
Mac. 29 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 32-35
Wimbo Na. 143 [*Ezra 8–Nehemia 4]
Na. 1: Maponyo ya Kimuujiza Kutoka kwa Mungu—Lini? (w97-SW 7/1 uku. 4-7)
Na. 2: Mwanzo 35:1-15
Na. 3: Saidia Watoto Wako Wachague Marafiki Wema (fy-SW uku. 95-97 fu. 14-18)
Na. 4: td-SW 6A Kifo cha Yesu Kilitimiza Nini?
Apr. 5 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 36-38
Na. 1: Wokovu—Unachomaanisha kwa Kweli (w97-SW 8/15 uku. 4-7)
Na. 2: Mwanzo 38:6-19, 24-26
Na. 3: td-SW 37A Ukumbusho wa Mlo wa Jioni wa Bwana
Na. 4: Kuchagua Tafrija Ifaayo ya Familia (fy-SW uku. 97-102 fu. 19-27)
Apr. 12 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 39-41
Wimbo Na. 34 [*Nehemia 12–Esta 5]
Na. 1: Kwa Nini Lililo Baya Liripotiwe? (w97-SW 8/15 uku. 26-29)
Na. 2: Mwanzo 40:1-15
Na. 3: Ufahamu wa Kimaandiko Kuhusu Familia za Mzazi Aliye Pekee (fy-SW uku. 103-105 fu. 1-8)
Na. 4: td-SW 44C Lazima Kuamini Kristo Kuandamane na Matendo
Apr. 19 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 42-44
Wimbo Na. 124 [*Esta 6–Ayubu 5]
Na. 1: Sababu Ambayo Hufanya Iwe Lazima Hasira Idhibitiwe (g97-SW 6/8 uku. 18-19)
Na. 2: Mwanzo 42:1-17
Na. 3: Ugumu wa Kupata Riziki Ukiwa Mzazi Aliye Pekee (fy-SW uku. 105-107 fu. 9-12)
Na. 4: td-SW 7A Vita ya Mungu ya Kukomesha Uovu
Apr. 26 Pitio la Kuandika. Kamilisha Ufunuo 16–Mwanzo 44
Mei 3 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 45-47
Na. 1: Je, Misherehekeo ya Mavuno Humpendeza Mungu? (w97-SW 9/15 uku. 8-9)
Na. 2: Mwanzo 45:16–46:4
Na. 3: Kudumisha Nidhamu Katika Nyumba ya Mzazi Aliye Pekee (fy-SW uku. 108-110 fu. 13-17)
Na. 4: td-SW 21A Kujiunga na Dini Nyingine Si Njia ya Mungu
Mei 10 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 48-50
Na. 1: Mwanzo—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW uku. 17-19 fu. 30-35)
Na. 2: Mwanzo 49:13-28
Na. 3: Kushinda Vita Dhidi ya Upweke (fy-SW uku. 110-113 fu. 18-22)
Na. 4: td-SW 21B Je, Dini Zote Ni Sawa Mbele za Mungu?
Mei 17 Usomaji wa Biblia: Kutoka 1-4
Na. 1: Utangulizi kwa Kutoka (si-SW uku. 19-20 fu. 1-8)
Na. 2: Kutoka 4:1-17
Na. 3: td-SW 15C Je, Maponyo ya Imani ya Kisasa Yana Uthibitisho wa Kukubaliwa na Mungu?
Na. 4: Jinsi ya Kusaidia Familia za Mzazi Aliye Pekee (fy-SW uku. 113-115 fu. 23-27)
Mei 24 Usomaji wa Biblia: Kutoka 5-8
Na. 1: Tajiri Ingawa Maskini—Yawezekanaje? (w97-SW 9/15 uku. 3-7)
Na. 2: Kutoka 7:1-13
Na. 3: td-SW 12B Kanisa Halikujengwa Juu ya Petro
Na. 4: Manufaa za Kukabili Ugonjwa kwa Mtazamo wa Kimungu (fy-SW uku. 116-120 fu. 1-9)
Mei 31 Usomaji wa Biblia: Kutoka 9-12
Na. 1: Kinachomaanishwa na Kutokuwa Sehemu ya Ulimwengu (g97-SW 9/8 uku. 12-13)
Na. 2: Kutoka 12:21-36
Na. 3: Thamani ya Roho Yenye Kuponya (fy-SW uku. 120-121 fu. 10-13)
Na. 4: td-SW 28A Siku ya Sabato Si Takwa kwa Wakristo
Juni 7 Usomaji wa Biblia: Kutoka 13-16
Na. 1: Jinsi ya Kupata Tumaini Katikati ya Hali ya Kukata Tumaini (w97-SW 5/15 uku. 22-25)
Na. 2: Kutoka 15:1-13
Na. 3: Weka Mambo ya Kutangulizwa na Usaidie Watoto Wakabiliane na Ugonjwa Katika Familia (fy-SW uku. 122-123 fu. 14-18)
Na. 4: td-SW 25A Nafsi Ni Nini?
Juni 14 Usomaji wa Biblia: Kutoka 17-20
Na. 1: Jinsi Ambavyo Wakristo Huheshimu Wazazi Wazee-Wazee (w97-SW 9/1 uku. 4-7)
Na. 2: Kutoka 17:1-13
Na. 3: td-SW 35A Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?
Na. 4: Jinsi ya Kuona Matibabu (fy-SW uku. 124-127 fu. 19-23)
Juni 21 Usomaji wa Biblia: Kutoka 21-24
Na. 1: Sayansi ya Kweli na Biblia Zaafikiana (g97-SW 7/8 uku. 26-27)
Na. 2: Kutoka 21:1-15
Na. 3: Mke Mwamini Anaweza Kudumishaje Amani Katika Nyumba Iliyogawanyika? (fy-SW uku. 128-132 fu. 1-9)
Na. 4: td-SW 39C Mume Hapaswi Kuruhusu Mke Amzuie Asitumikie Mungu
Juni 28 Usomaji wa Biblia: Kutoka 25-28
Na. 1: Mjue Yehova, Yule Mungu Mwenye Utu (w97-SW 10/1 uku. 4-8)
Na. 2: Kutoka 25:17-30
Na. 3: td-SW 39A Sababu ya Upinzani Kuelekea Wakristo
Na. 4: Mume Mwamini Anaweza Kudumishaje Amani Katika Nyumba Iliyogawanyika? (fy-SW uku. 132-133 fu. 10-11)
Jul. 5 Usomaji wa Biblia: Kutoka 29-32
Na. 1: Usiruhusu Roho ya Ulimwengu Ikutie Sumu (w97-SW 10/1 uku. 25-29)
Na. 2: Kutoka 29:1-14
Na. 3: Kuzoeza Watoto Kimaandiko Katika Nyumba Iliyogawanyika (fy-SW uku. 133-134 fu. 12-15)
Na. 4: td-SW 22A Lazima Wakristo Wote Wawe Wahudumu
Jul. 12 Usomaji wa Biblia: Kutoka 33-36
Na. 1: Uwe Mwenye Kutumainika na Ushikilie Uaminifu-Maadili Wako (w97-SW 5/1 uku. 4-7)
Na. 2: Kutoka 34:17-28
Na. 3: Kuendeleza Uhusiano Wenye Amani na Wazazi Wako Ambao Ni wa Dini Tofauti (fy-SW uku. 134-135 fu. 16-19)
Na. 4: td-SW 4A Kuna Dini Moja Tu ya Kweli
Jul. 19 Usomaji wa Biblia: Kutoka 37-40
Na. 1: Kutoka—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW uku. 24 fu. 26-31)
Na. 2: Kutoka 40:1-16
Na. 3: Ugumu wa Kuwa Mzazi wa Kambo (fy-SW uku. 136-139 fu. 20-25)
Na. 4: td-SW 4C Je, Ni Makosa Kubadili Dini ya Mtu?
Jul. 26 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 1-4
Wimbo Na. 26 [*Zaburi 107-118]
Na. 1: Utangulizi kwa Mambo ya Walawi (si-SW uku. 25-26 fu. 1-10)
Na. 2: Mambo ya Walawi 2:1-13
Na. 3: Usiruhusu Vifuatio vya Kimwili Vigawanye Nyumba Yako (fy-SW uku. 140-141 fu. 26-28)
Na. 4: td-SW 23A Utumizi wa Sanamu Katika Ibada Haumpendezi Mungu
Ago. 2 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 5-7
Na. 1: Ufunguo wa Furaha Halisi (w97-SW 10/15 uku. 5-7)
Na. 2: Mambo ya Walawi 6:1-13
Na. 3: Madhara Yanayosababishwa na Uraibu wa Alkoholi (fy-SW uku. 142-143 fu. 1-4)
Na. 4: td-SW 23B Ibada ya Mifano Ilikuwa Mtego kwa Waisraeli
Ago. 9 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 8-10
Wimbo Na. 210 [*Zaburi 126-143]
Na. 1: Kufahamu Kanuni Hudhihirisha Ukomavu (w97-SW 10/15 uku. 28-30)
Na. 2: Mambo ya Walawi 10:12-20
Na. 3: Kusaidia Mshiriki wa Familia Aliye na Uraibu wa Alkoholi (fy-SW uku. 143-147 fu. 5-13)
Na. 4: td-SW 27A Roho Takatifu Ni Nini?
Ago. 16 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 11-13
Wimbo Na. 80 [*Zaburi 144–Mithali 5]
Na. 1: Jihadhari na “Waepikurea” (w97-SW 11/1 uku. 23-25)
Na. 2: Mambo ya Walawi 13:1-17
Na. 3: Ujeuri wa Nyumbani na Njia za Kuuepuka (fy-SW uku. 147-149 fu. 14-22)
Na. 4: td-SW 36A Uhai Udumuo Milele Umehakikishiwa Wanadamu Watiifu
Ago. 23 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 14-15
Na. 1: Hizi Ndizo Siku za Mwisho Kwelikweli (w97-SW 4/1 uku. 4-8)
Na. 2: Mambo ya Walawi 14:33-47
Na. 3: td-SW 36C Uhai wa Kidunia Umeahidiwa Hesabu Isiyo na Mpaka
Na. 4: Je, Kutengana Ndilo Suluhisho? (fy-SW uku. 150-152 fu. 23-26)
Ago. 30 Pitio la Kuandika. Kamilisha Mwanzo 45-Mambo ya Walawi 15
Wimbo Na. 145 [*Mithali 15-22]
Sept. 6 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 16-18
Wimbo Na. 222 [*Mithali 23-31]
Na. 1: Kuteseka Kutakapokuwa Hakupo Tena (w97-SW 2/15 uku. 4-7)
Na. 2: Mambo ya Walawi 16:20-31
Na. 3: td-SW 43A Lazima Wakristo wa Kweli Walitambue na Kulitumia Jina la Mungu
Na. 4: Njia ya Kimaandiko ya Kutatua Matatizo ya Ndoa (fy-SW uku. 153-156 fu. 1-9)
Sept. 13 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 19-21
Na. 1: Sababu Ambayo Hufanya Kujinyima Sana Raha na Anasa Kusiwe Ufunguo wa Kupata Hekima (g97-SW 10/8 uku. 20-21)
Na. 2: Mambo ya Walawi 19:16-18, 26-37
Na. 3: td-SW 42B “Ukiisha Okolewa, Umeokolewa Sikuzote” Si Wazo la Kimaandiko
Na. 4: Kutoa Haki ya Ndoa (fy-SW uku. 156-158 fu. 10-13)
Sept. 20 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 22-24
Wimbo Na. 8 [*Wimbo Ulio Bora 1–Isaya 5]
Na. 1: Je, Kulalamika kwa Namna Zote Ni Kubaya? (w97-SW 12/1 uku. 29-31)
Na. 2: Mambo ya Walawi 23:15-25
Na. 3: td-SW 14B Ni Mungu Tu Apasaye Kuabudiwa
Na. 4: Misingi ya Kibiblia ya Talaka (fy-SW uku. 158-159 fu. 14-16)
Sept. 27 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 25-27
Na. 1: Mambo ya Walawi—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW uku. 28-30 fu. 28-39)
Na. 2: Mambo ya Walawi 25:13-28
Na. 3: td-SW 2A Sababu Ambayo Huwafanya Mashahidi wa Yehova Wasikubali Kutiwa Damu Mishipani
Na. 4: Kile Ambacho Maandiko Husema Juu ya Kutengana (fy-SW uku. 159-162 fu. 17-22)
Okt. 4 Usomaji wa Biblia: Hesabu 1-3
Na. 1: Utangulizi kwa Hesabu (si-SW uku. 30-31 fu. 1-10)
Na. 2: Hesabu 1:44-54
Na. 3: Kuzeeka Mkiwa Pamoja (fy-SW uku. 163-165 fu. 1-9)
Na. 4: td-SW 3C Tunda Lililokatazwa Lilikuwa Nini?
Okt. 11 Usomaji wa Biblia: Hesabu 4-6
Na. 1: Yehova Hutawala kwa Huruma (w97-SW 12/15 uku. 28-29)
Na. 2: Hesabu 4:17-33
Na. 3: Kuimarisha Tena Vifungo vya Ndoa (fy-SW uku. 166-167 fu. 10-13)
Na. 4: td-SW 10B Ni Nani Anayeutawala Ulimwengu?
Okt. 18 Usomaji wa Biblia: Hesabu 7-9
Na. 1: Mahali Ambako Furaha ya Kweli Yaweza Kupatikana (w97-SW 3/15 uku. 23)
Na. 2: Hesabu 9:1-14
Na. 3: Furahieni Wajukuu Wenu na Mfanye Marekebisho Kadiri Mzeekavyo (fy-SW uku. 168-170 fu. 14-19)
Na. 4: td-SW 8B Moto Ni Mfano wa Maangamizo ya Daima
Okt. 25 Usomaji wa Biblia: Hesabu 10-12
Na. 1: Yehova Huwajali Wenye Taabu (w97-SW 4/15 uku. 4-7)
Na. 2: Hesabu 10:11-13, 29-36
Na. 3: Kukabiliana na Hali ya Kumpoteza Mwenzi (fy-SW uku. 170-172 fu. 20-25)
Na. 4: td-SW 5B Dunia Itakaliwa Sikuzote
Nov. 1 Usomaji wa Biblia: Hesabu 13-15
Na. 1: Sababu Inayofanya Miujiza Peke Yayo Isijenge Imani (w97-SW 3/15 uku. 4-7)
Na. 2: Hesabu 14:13-25
Na. 3: td-SW 19A Asili ya Mashahidi wa Yehova
Na. 4: Njia za Kikristo za Kuwaheshimu Wazazi Wazee-Wazee (fy-SW uku. 173-175 fu. 1-5)
Nov. 8 Usomaji wa Biblia: Hesabu 16-19
Na. 1: Sababu Inayofanya Umaskini Usiwe Sababu Halali ya Kuiba (g97-SW 11/8 uku. 18-19)
Na. 2: Hesabu 18:1-14
Na. 3: Onyesha Upendo na Hisia-Mwenzi (fy-SW uku. 175-178 fu. 6-14)
Na. 4: td-SW 26D Wakristo Wapaswa Kufunga Ndoa na Wakristo Wenzao Tu
Nov. 15 Usomaji wa Biblia: Hesabu 20-22
Na. 1: Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Kwanza (w97-SW 8/15 uku. 8-11)
Na. 2: Hesabu 20:14-26
Na. 3: Mtegemee Yehova Sikuzote Ili Upate Nguvu (fy-SW uku. 179-182 fu. 15-21)
Na. 4: td-SW 33B Ubatizo Hauoshei Mbali Dhambi
Nov. 22 Usomaji wa Biblia: Hesabu 23-26
Na. 1: Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Pili (w97-SW 9/15 uku. 25-29)
Na. 2: Hesabu 23:1-12
Na. 3: Sitawisha Ujitoaji-Kimungu na Kujidhibiti (fy-SW uku. 183-184 fu. 1-5)
Na. 4: td-SW 9A Maria Mama ya Yesu, Si “Mama ya Mungu”
Nov. 29 Usomaji wa Biblia: Hesabu 27-30
Wimbo Na. 180 [*Yeremia 14-21]
Na. 1: Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Tatu (w97-SW 10/15 uku. 8-12)
Na. 2: Hesabu 27:1-11
Na. 3: Maoni Yafaayo Juu ya Ukichwa (fy-SW uku. 185-186 fu. 6-9)
Na. 4: td-SW 40A Kwa Nini Yehova Hawezi Kuwa Sehemu ya Utatu
Des. 6 Usomaji wa Biblia: Hesabu 31-32
Wimbo Na. 170 [*Yeremia 22-28]
Na. 1: Mizizi ya Krismasi ya Kisasa (w97-SW 12/15 uku. 4-7)
Na. 2: Hesabu 31:13-24
Na. 3: Fungu Muhimu la Upendo Katika Familia (fy-SW uku. 186-187 fu. 10-12)
Na. 4: td-SW 40B Mwana Si Sawa na Baba
Des. 13 Usomaji wa Biblia: Hesabu 33-36
Na. 1: Hesabu—Kwa Nini Ni Chenye Mafaa (si-SW uku. 35 fu. 32-38)
Na. 2: Hesabu 36:1-13
Na. 3: td-SW 31A Wakristo wa Mapema Hawakuadhimisha Siku za Kuzaliwa Wala Krismasi
Na. 4: Kufanya Mapenzi ya Mungu Mkiwa Familia (fy-SW uku. 188-189 fu. 13-15)
Des. 20 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 1-3
Wimbo Na. 159 [*Yeremia 35-41]
Na. 1: Utangulizi kwa Kumbukumbu la Torati (si-SW uku. 36-37 fu. 1-9)
Na. 2: Kumbukumbu la Torati 2:1-15
Na. 3: td-SW 44A Yesu Ni Mwana wa Mungu na Mfalme Aliyewekwa Rasmi
Na. 4: Familia na Wakati Wako Ujao (fy-SW uku. 190-191 fu. 16-18)
Des. 27 Pitio la Kuandika. Kamilisha Mambo ya Walawi 16–Kumbukumbu la Torati 3
Wimbo Na. 192 [*Yeremia 42-48]