Habari za Kitheokrasi
◼ Hivi majuzi Jumba la Ufalme la Mbeya-Iyunga liliwekwa wakfu.
◼ Mashahidi wa Yehova walisajiliwa kisheria katika Bulgaria mnamo Oktoba 7, 1998. Twashiriki pamoja na wahubiri 946 huko kumpa Yehova shukrani kwa jambo hilo.
◼ Mnamo Oktoba 12, 1998, serikali ya Latvia iliidhinisha kusajiliwa kwa makutaniko 2 ya kwanza kati ya yale 21 yaliyo katika nchi hiyo.
◼ Kujapokuwa upinzani, ndugu katika Ufaransa wanavumilia katika kazi yao ya kuhubiri Ufalme. Katika Novemba na Desemba, kampeni ya kuvuta uangalifu wa nchi hiyo kwenye Biblia ilikazia ugawanyaji wa pekee wa broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote. Wanabetheli 50 hivi walihama kutoka Ufaransa hadi Uingereza kusaidia katika kazi za uchapaji na upakizi kwenye ofisi ya tawi, huku washiriki wale wengine 250 wa Betheli ya Ufaransa na ndugu walioko shambani wakiendelea kutumikia kwa shangwe chini ya hali za kawaida.