Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/99 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Mei 3
  • Juma Linaloanza Mei 10
  • Juma Linaloanza Mei 17
  • Juma Linaloanza Mei 24
  • Juma Linaloanza Mei 31
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 5/99 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Juma Linaloanza Mei 3

Wimbo 7

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 17: “Fundisha Wengine ili Wajinufaishe.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe na mazungumzo ya maswali na majibu. Ukitumia sura ya 13 ya kitabu Ujuzi, toa kielezi cha jinsi ambavyo watu wananufaika kwa njia yenye kutumika wanapojifunza, wanapoelewa, na kutumia kanuni za Biblia.

Dak. 20: “Njia za Kupanua Huduma Yako.” Wazee wawili wazungumzia makala hii kwa kujibu maswali yaliyotokezwa na wasikilizaji tofauti-tofauti. Mhubiri tineja, wenzi wa ndoa, na ndugu mwenye umri wa kustaafu wanauliza njia ambazo wanaweza kutumia ili kupanua huduma yao. Madokezo yenye kutumika yanatolewa kutoka katika makala hiyo na sura ya 9 ya kitabu Huduma Yetu, ikikazia “Miradi Yako ya Kiroho kwa Wakati Ujao Ni Nini?,” kwenye ukurasa wa 116-118. Wahubiri wanaeleza uthamini wao kwa habari hiyo yenye msaada ambayo Sosaiti huandaa inayoonyesha jinsi ya kupanga utumishi uliopanuliwa wakati ujao wa karibuni.

Wimbo 11 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 10

Wimbo 15

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 12: Una Mipango Gani ya Likizo? Familia yapitia mipango yao ya kuhudhuria mkusanyiko, kufanya upainia-msaidizi, kwenda likizo, na tafrija. (Ona Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1998, ukurasa wa 3.) Wanazungumzia jinsi ya kupanga na kutoa ushahidi wa vivi hivi, na wanatoa wonyesho wa jinsi ya kuanzisha mazungumzo. Kazia uhitaji wa kuendelea na funzo la kibinafsi na funzo la Biblia la familia, kufika kwenye mikutano ya kutaniko mnaposafiri kwingineko, na kupeleka ripoti ya utumishi wa shambani kwenye kutaniko la nyumbani. Familia yajikumbusha mambo mazuri yaliyoonwa walipotembelea makutaniko mengine na shangwe waliyohisi. Wanachunguza njia ambazo wanaweza kuonyesha ukaribishaji-wageni kwa wageni wowote wanaokuja kutanikoni.

Dak. 25: “Mikusanyiko ya Wilaya ya 1999 ya ‘Neno la Mungu la Kiunabii.’” (Fungu la 1-16) Maswali na majibu. Soma fungu la 6, 8, 11, na 16. Kazia sababu ambazo twapaswa kuhudhuria mkusanyiko wote, kutia ndani vipindi vya Ijumaa. Kazia umuhimu wa kufuata mwelekezo wa Sosaiti wa kuleta chakula chetu cha mchana mkusanyikoni kila siku.

Wimbo 19 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 17

Wimbo 27

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Chunguzeni “Je, Utahudhuria?”

Dak. 15: “Panga Kimbele.” Hotuba inayopitia utendaji wote wa kitheokrasi uliopangwa kwenu kwa miezi kadhaa ijayo. Tia moyo kila mtu atie alama tarehe kwenye kalenda yake na asiruhusu mambo mengine yavuruge.

Dak. 20: “Mikusanyiko ya Wilaya ya 1999 ya ‘Neno la Mungu la Kiunabii.’” (Fungu la 17-24) Maswali na majibu. Soma fungu la 18-21. Tumia maandiko yaliyonukuliwa na yaliyotajwa bila kunukuliwa kukazia sababu ambazo mavazi, mapambo, na mwenendo wapasa kukaziwa uangalifu.

Wimbo 29 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 24

Wimbo 41

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Pitia barua ya Sosaiti ya Oktoba 15, 1998, inayohusu fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43-SW). Eleza jinsi hiyo iwezavyo kusaidia kufuatia upendezi uliopatikana wakati wa kutoa ushahidi wa vivi hivi na unapokutana na watu wanaosema lugha nyingine. Tia moyo wahubiri watumie vizuri fomu hizi.

Dak. 12: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.

Dak. 18: Je, Tunashiriki Kazi ya Kutenganisha? Hotuba yenye kuchochea itolewe na mwangalizi wa utumishi, ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1997, ukurasa wa 30-31.

Wimbo 32 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 31

Wimbo 43

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Mei. Pitia toleo la fasihi la Juni. Unapotoa kitabu Ujuzi, waweza kuongezea nakala ya kitabu cha zamani chenye kurasa 192 ambacho kiko kwa wingi akibani katika kutaniko. Toa wonyesho wa utoaji huo.

Dak. 15: “Fedha za Kuendesha Kazi Yao Zinatokana na Michango ya Kujitolea.” Mwandishi azungumzia habari iliyo katika broshua, Mashahidi wa Yehova Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote, ukurasa wa 28. Soma na ukazie 2 Wakorintho 8:12; 9:7. Taja kwamba kama ilivyoandikwa katika maandiko kila mtu anaweza kutoa mchango kama alivyonuia moyoni mwake. Si vizuri kufanya mtu yeyote ahisi anasukumwa kutoa mchango. Haingefaa kuweka vikapu au vyombo vinginevyo katika Jumba la Ufalme na kuomba akina ndugu watumbukize fedha wanapopita. Wala si jambo la kimaandiko kuwekea mtu yeyote masharti ya kiwango fulani cha mchango atakachotoa. Iwe kutaniko lahitaji fedha za kujenga Jumba la Ufalme au gharama nyinginezo, Mashahidi wa Yehova hufuata kanuni za Biblia na kutoa kwa hiari wanachoweza ili kutegemeza ibada safi. Wanafurahi kutoa upaji kwa hiari bila kusukumwa na mtu yeyote au bila kufuata njia zozote za kilimwengu za kukusanya fedha. Taja kwamba nyakati nyingine inakuwa lazima kuazimia kile ambacho kutaniko litalipia mkopo wa Jumba la Ufalme. Vikaratasi visivyotiwa sahihi vyenye kiwango fulani vitatosha tu kutoa kadirio hilo. Baada ya hapo, wazee hawangemlazimisha mtu yeyote kulipa kile ambacho mtu alikuwa ameazimia. Hali hutofautiana na tena akina ndugu wanafurahi kutoa kile wanachoweza. Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni, 1976, kwenye kichwa kidogo, “Kutoa Pesa za Kuendesha Jumba la Ufalme.” Ona pia kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, ukurasa wa 121 na 122.

Dak. 15: Dini Yangu Ina Kasoro Gani? Mazungumzo kati ya watumishi wa huduma wawili. Twakabiliana na watu wengi ambao wanapendelea kweli na kupendezwa na Mashahidi wa Yehova. Hata hivyo, vifungo wanavyodumisha katika kanisa lao huwazuia. Wao huona likiwa jambo gumu kuamini kwamba tuna dini moja tu ya kweli na kwamba ibada yao si ya kweli. Hicho huwa kizuizi kikubwa cha maendeleo yao ya kiroho. Akina ndugu hao wanapitia mambo sita yanayotajwa kwenye ukurasa wa 183-184, wa kitabu Kutoa Sababu, ambayo yanaonyesha wazi kwamba dini nyingine hazifuati Biblia. Tia moyo wasikilizaji watumie mambo haya kwa busara kusaidia watu wenye moyo mnyofu wachanganue itikadi zao za kidini.

Wimbo 50 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki