Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/00 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Januari 10
  • Juma Linaloanza Januari 17
  • Juma Linaloanza Januari 24
  • Juma Linaloanza Januari 31
  • Juma Linaloanza Februari 7
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 1/00 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Januari 10

Wimbo 107

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 15: “Kujulisha Jina la Yehova Katika Dunia Yote.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani maelezo kuhusu ushahidi wa vivi hivi kutoka katika kitabu Huduma Yetu ukurasa wa 93 na 94.

Dak. 20: Kufanya Uchaguzi wa Kisheria wa Kutotiwa Damu Kuhusu Mambo ya Kitiba. (Mdo. 15: 28, 29) Hotuba itolewe na mzee mwenye kustahili, inayotegemea barua ya Februari 15, 1997, na Desemba 1, 1998. Baada ya mkutano huu, Mashahidi waliobatizwa wanaweza kupata kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia mpya, na wale walio na watoto wadogo wasiobatizwa wanaweza kupokea Kadi ya Utambulishi kwa kila mtoto. Kadi hizi hazitajazwa usiku huu. Zapaswa kujazwa kwa uangalifu nyumbani lakini ZISITIWE sahihi. Kutia sahihi, kushuhudia, na kuandika tarehe katika kadi zote kutafanywa baada ya Funzo la Kitabu la Kutaniko linalofuata, chini ya usimamizi wa kiongozi wa funzo la kitabu. Kabla ya kutia sahihi, hakikisha kwamba kadi zimejazwa kikamili. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi wanapaswa kuona mwenye kadi akitia sahihi kadi hiyo. Kwa kugeuza usemi ulio katika kadi hii kulingana na hali zao na masadikisho yao wenyewe, wahubiri wasiobatizwa wanaweza kuandika mwelekezo wao wenyewe wa kutumia na wa watoto wao. Viongozi wa funzo la kitabu wapaswa kuhakikisha kwamba wote walio katika kikundi chao wanapata msaada wanaohitaji kujaza kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia.

Wimbo 155 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 17

Wimbo 12

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Usafi wa Kiafya wa Kibinafsi. Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Amkeni! Novemba 22, 1998, ukurasa wa 31, “Nawa Mikono na Uipanguse!,” Amkeni! Novemba 22, 1997, ukurasa wa 11 “Nawa Mikono kwa Sabuni,” na Amkeni! Novemba 8, 1997 ukurasa wa 28, “Nawa Mikono.” Taja kwamba baada ya kusalimiana kwa mikono likiwa jambo la utunzaji wa afya wa kibinafsi, unapaswa kunawa mikono kabla ya kugusa chakula. Hiki ni kikumbusha kizuri hasa wakati wa makusanyiko na mikusanyiko.

Dak. 20: “Tumia Trakti Kuanzisha Mazungumzo.” Pitia trakti zozote nne zinazotumika sana katika eneo lenu. Tokeza swali linalojibiwa na kila trakti. Wakaribishe wasikilizaji kutoa mapendekezo ya jinsi swali hilo linavyoweza kutumiwa kuanzisha mazungumzo na labda kuongoza kwenye funzo la Biblia. Toa wonyesho wa jinsi ambavyo hilo laweza kufanywa ukitumia mbili za trakti hizo.

Wimbo 57 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 24

Wimbo 110

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na mambo yaliyoonwa shambani.

Dak.15: “Chunguza Neno la Yehova Kila Siku!” Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Tia moyo kila mmoja atumie vizuri Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2000. Tia ndani maelezo kutoka kwenye utangulizi katika ukurasa wa 3-4. Ikiwa kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2000 hakipatikani kwenye kutaniko lenu, tumia habari iliyoko kwenye Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1999, ukurasa wa 3-4. Waalike wasikilizaji wasimulie jinsi wanavyofanya jitihada ya pekee ili kuchunguza andiko na maelezo kila siku.

Dak. 20: “Je, Utakuwapo?” Hotuba na mambo yaliyoonwa, ikiongozwa na mzee. Mikusanyiko mikubwa imechangia sehemu kubwa katika kuwatia nguvu watu wa Mungu kuanzia nyakati za Biblia kufikia siku yetu. (Ona kitabu Wapiga-Mbiu ukurasa wa 254 fungu la 1-3, na Insight, Buku la 1 ukurasa 821 fungu la 5.) Watie wote moyo waanze kufanya mipango sasa ya kuhudhuria siku zote tatu za kusanyiko la wilaya la mwaka huu. Waalike wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa yakionyesha kwamba bidii yao nyendelevu ili waweze kuwepo katika siku zilizopita zilithawabishwa kiroho.

Wimbo 157 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 31

Wimbo 16

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Januari. Taja toleo la mwezi wa Februari: kitabu Furaha ya Familia. Toa wonyesho wa jinsi yale maswali matatu katika kisanduku kwenye ukurasa wa 12 wa kitabu hicho yanavyoweza kutumiwa kumhusisha mtu katika mazungumzo.

Dak. 15: Jibu kwa Swali Kuhusu ‘Kutia Alama.’ Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1999, ukurasa wa 29-31.

Dak. 18: Jinsi ya Kuwasaidia Wengine Watambue Dini ya Kweli. Mazungumzo kati ya mtumishi wa huduma anayestahili na wahubiri wawili au watatu wenye uwezo kuhusu jinsi watu wanavyoweza kuvutiwa na Mashahidi wa Yehova lakini hawaelewi vizuri tofauti kati ya dini nyingine na yetu. Pitia zile hoja kumi zilizo kwenye ukurasa wa 20 wa Amkeni! Mei 8, 1995. Eleza jinsi ambavyo kujua habari hizo kwaweza kusaidia mtu mwenye moyo mnyofu aone tofauti kati ya ibada ya kweli na isiyo ya kweli na uhitaji wa kujifunza kutokana na watu wa Yehova na kushirikiana nasi.

Wimbo 60 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 7

Wimbo 113

Dak. 8: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 17: Pitia Kitabu Unabii wa Danieli. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Pitia mambo makuu ya kitabu hiki kipya: ukikazia vichwa vya sura, picha zilizo dhahiri visanduku vilivyo na maswali yenye kuamsha fikira mwishoni mwa kila sura, ramani na chati zinazoelezea vizuri mambo makuu. Chunguza yale maelezo yenye kutia moyo kuhusu jinsi Mikaeli “atakavyosimama” katika njia ya pekee (ukurasa wa 288-290). Zungumzia umuhimu wa kuendelea kuvumilia tukiwa walimu wa Neno la Mungu (Ukurasa wa 311-312). Sisi sote twapaswa kusoma kitabu hicho kwa makini na kuwatia moyo wenye kupendezwa kufanya hivyo pia.

Dak. 20: Walifanya Uamuzi Wenye Hekima. Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi Oktoba 15, 1997, ukurasa wa 19-21, mafungu 3-16. Simulia maelezo ya mapainia, ukionyesha kwa nini wanahisi kwamba maisha ambayo wameishi yamekuwa yenye kuthawabisha sana, na yenye kunufaisha. Watie moyo wote waliohudhuria kufikiria uwezekano wa kuwa mapainia.

Wimbo 182 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki