Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/00 uku. 3
  • Chunguza Neno la Yehova Kila Siku!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Chunguza Neno la Yehova Kila Siku!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Ratiba ya Familia—Andiko la Siku
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Jinsi Yehova Anavyotusaidia Kuvumilia kwa Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Je, Uko Tayari Kurudi Shuleni?
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 1/00 uku. 3

Chunguza Neno la Yehova Kila Siku!

1 Kila siku imani yetu hupatwa na magumu mapya. Labda mjuani mlimwengu hukusonga mfanye miadi pamoja. Mwalimu wako akutaka ufuatie kazi-maisha ya kimwili, au mwajiri wako akutaka ufanye kazi kwa muda wa saa nyingi zaidi. Afya yako ya kimwili huenda ikawa inazorota. Hata ingawa majaribu kama hayo yaweza kukukabili wakati wowote, hauko peke yako. Yehova yuko tayari kukupa hekima unayohitaji ili uweze kukabiliana nayo. Kuchunguza andiko la Biblia na maelezo katika Kuyachunguza Maandiko ni njia moja ambayo waweza kutwaa Neno la Yehova kwa ukawaida. Je, wewe hutumia kwa manufaa uandalizi huu?

2 Msaada Wapatikana: Isaya 30:20, Biblia Habari Njema, humweleza Yehova kuwa “Mwalimu” ambaye watu wa Mungu hutafuta msaada kutoka kwake. Yeye hukupa yale unayohitaji ili uweze kukabiliana na magumu ya imani yako. Jinsi gani? Mstari unaofuata hueleza hivi: “Mtasikia sauti nyuma yenu ikisema, ‘Njia ni hii; ifuateni.’” Leo, Yehova hupeleka “neno” lake kupitia Maandiko na vichapo vya ‘mtumwa mwaminifu na mwenye busara.’ (Mt. 24:45) Kuna hekima nyingi katika makala za Mnara wa Mlinzi za wakati uliopita, zinazozungumzia karibu kila sehemu ya maisha ya Kikristo. Kupitia makala zilizoonyeshwa katika Kuyachunguza Maandiko husaidia kujenga ghala la ujuzi ambalo litasaidia sana katika kukabiliana na matatizo ya kila aina.— Isa. 48:17.

3 Ratibu Wakati: Hata ingawa asubuhi ulikuwa wakati wenye shughuli nyingi, mama mmoja alihakikisha kwamba alisoma na kuzungumzia andiko na maelezo pamoja na mwana wake alipokuwa akila kiamsha kinywa. Maneno hayo pamoja na sala ndiyo yalikuwa maneno ya mwisho aliyosikia kila asubuhi kabla hajaondoka kwenda shuleni. Yalimwimarisha kukinza msongo wa kufanya ngono, kuchukua msimamo thabiti alipokabiliwa na suala la utukuzo wa taifa na kutoa ushahidi kwa ujasiri kwa wanafunzi na walimu pia. Hata ingawa alikuwa ndiye Shahidi pekee shuleni, hakujihisi akiwa peke yake.

4 Mtegemee Yehova na Neno lake ili kupata mwelekezo na ushauri. Ukifanya hivyo, atakuwa halisi kwako kama rafiki mwenye kutumainiwa. Mwendee kila siku! Pamoja na mamilioni ya wengine ulimwenguni pote ambao huchunguza Neno la Mungu kila siku, utapata kwamba macho yako yatakuwa “macho yaonayo Mwalimu wako.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki