Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Aprili 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Usisahau hotuba ya pekee ya Aprili 16, yenye kichwa “Sababu Wanadamu Wanahitaji Fidia.” Tia moyo wote wafuate usomaji wa Biblia wa Ukumbusho ulioratibiwa Aprili 14-19, kama ilivyoonyeshwa kwenye Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2000. Chunguzeni “Vikumbusha vya Ukumbusho,” kwenye ukurasa wa 4 wa nyongeza.
Dak. 15: “Je, Waitikia Upendo wa Kristo?” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatie kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani mawazo yaliyo kwenye Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 1998, ukurasa wa 16-17, fungu la 12-13. Tia moyo kila mtu ajitahidi kwa njia ya pekee kualika watu kwenye Ukumbusho.
Dak. 20: “Aprili—Wakati wa Kuwa Wenye Bidii kwa Kazi Zilizo Bora!” Maswali na majibu. Mazungumzo yenye uchangamfu juu ya yale tunayotamani kutimiza katika Aprili. Tumia dakika tatu au nne za kumalizia kuchunguza “Bidii Inayochochea Walio Wengi.”
Wimbo 199 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 17
Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Ni miisho-juma miwili tu iliyobaki ya Aprili, kwa hiyo tia moyo kila mtu ashiriki katika huduma kabla ya mwezi kwisha. Toa onyesho fupi la utoaji wa magazeti ukitumia matoleo ya karibuni na ueleze vizuri mpango wa mchango. Mwache mtu aweke mchango wake katika bahasha ambayo mhubiri anayo. Ona onyesho katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1999. Kwa kuwa huenda tukawajibika kujibu watu ambao wanataka tushiriki katika desturi zao za Ista, soma yaliyoandikwa kwenye kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 293-294.
Dak. 16: “Je Una Roho ya Kujitolea?” Maswali na majibu. Twahitaji kupanga mambo ya kutangulizwa, tukiweka mambo ya muhimu yawe ya kwanza. Hutaka nia na kujidhibiti ili kuendelea kufanya yale yatakayotufaidi kiroho. Eleza tunayoweza kujifunza kutokana na kielelezo cha Yesu.—Ona Insight, Buku la 2, ukurasa wa 68, fungu la 3-5.
Dak. 16: Angusha Magazeti Pale Ambapo Yatapata Matokeo Zaidi. Hotuba, na wasikilizaji wakishiriki. Zungumzia madokezo yaliyo katika Amkeni!, Januari 8, 1995, ukurasa wa 22-24. Eleza uzuri wa kutafuta watu ambao wataelekea kukubali makala za pekee zilizo katika magazeti. Fikiria vielelezo vya matoleo yaliyopita na aina za watu, wafanya biashara, au mashirika ambayo yalivutiwa na makala katika eneo lenu. Alika wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa yanayoonyesha jinsi walivyopata matokeo kwa kutumia njia hii. Kama kikumbusha, tajia akina ndugu kwamba kuachia watu magazeti hakutegemei kama wanatoa mchango au hawatoi, bali kwategemea upendezi halisi wa kuyasoma.
Wimbo 71 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tangazia kutaniko hudhurio la Ukumbusho. Alika wasikilizaji wasimulie maelezo yaliyotolewa na wale waliohudhuria kwa mara ya kwanza.
Dak. 17: Saidia Wapya Wahudhurie Mikutano. Hotuba ikitegemea kitabu Ujuzi, ukurasa wa 162-163, fungu la 5-8. Baada ya kujifunza kwa muda fulani, ni muhimu wapya waanze kuja mikutanoni. Kuwafanya wahudhurie mikutano kwaweza kuwa jambo gumu. Unaweza kufanya nini ili uwachochee? Wale wanaoongoza mafunzo wapaswa kuchukua wakati wapitie habari iliyo katika kitabu Ujuzi pamoja na wanafunzi wao kisha wafanye mipango dhahiri ya kuwasaidia wajiunge nasi katika ibada ya kweli.
Dak. 18: “Je, Wewe Ni Mtangazaji wa Kawaida wa Ufalme?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakifanywa na mwandishi. Eleza ni kwa nini turipoti utumishi wetu wa shambani. (Ona Huduma Yetu, ukurasa wa 106-108.) Simulia baadhi ya matatizo ambayo hutokea tunapochelewa kutoa ripoti zetu. Alika wasikilizaji waeleze kile ambacho wao hufanya ili kutoa ripoti zao kwa wakati. Eleza jinsi ambavyo viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanavyoweza kusaidia. Ni mwisho-juma mmoja tu uliobaki katika Aprili, kwa hiyo kazia umuhimu wa kila mtu kwenda katika utumishi wa shambani na kuripoti utendaji wake mwishoni mwa mwezi.
Wimbo 200 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 1
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Aprili. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wapaswa kuuliza kila mtu katika kikundi chao ili ripoti zote zihesabiwe kufikia Mei 6. Zungumzieni Sanduku la Swali, ukihusisha matumizi ya kwenu.
Dak. 18: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 15: “Hakikisha Umerudi!” Mazungumzo na wasikilizaji. Zungumzieni sababu ambazo huenda tukakosa kufanya ziara za kurudia. Eleza kwa nini maandishi sahihi na utayari wa kurudi ni muhimu. Dokeza kutenga wakati fulani kila juma ili kufanya ziara za kurudia. Zungumzia yaliyo katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 88-89. Simulia jambo lililoonwa katika 1995 Yearbook, ukurasa wa 45.—1 Kor. 3:6, 7.
Wimbo 68 na sala ya kumalizia.