Bidii Inayochochea Walio Wengi
Mtume Paulo alipongeza Wakorintho kwa sababu bidii yao kwa kazi nzuri ilikuwa “imechochea walio wengi” kati ya Wakristo wenzao. (2 Kor. 9:2) Mara nyingi, watu mmoja-mmoja, familia, kikundi cha funzo la kitabu, au kutaniko zima laweza kuwa na matokeo hayohayo kwa kushiriki kwa bidii kazi ya kueneza evanjeli. Zifuatazo ni njia kadhaa ambazo unaweza kuonyesha bidii katika huduma.
◼ Pangia Jumamosi zako kwa ajili ya utendaji wa Siku ya Magazeti.
◼ Shiriki katika utumishi wa shambani Jumapili.
◼ Hubiri jioni iwezekanapo.
◼ Nenda mahubiri siku zozote za pekee zilizopangwa.
◼ Tumia likizo kutoka kazini au shuleni ili kwenda katika utumishi.
◼ Unga mkono huduma wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko.
◼ Fanya upainia-msaidizi mwezi mmoja au zaidi katika mwaka.
◼ Rekebisha hali zako ili ufanye upainia wa kawaida ikiwezekana.
Ona 2000 Yearbook of Jehovah’s Witnesses, ukurasa wa 17-19.