Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/00 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 12
  • Juma Linaloanza Juni 19
  • Juma Linaloanza Juni 26
  • Juma Linaloanza Julai 3
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 6/00 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Juni 12

Wimbo 136

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: “‘Kazi Yenu ya Jasho Si ya Bure.’” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani maelezo juu ya jambo lililoonwa lililosimuliwa katika Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1996, ukurasa wa 32.

Dak. 22: Kuanzisha Mafunzo kwa Broshua Anataka. Hotuba, itakayozungumzia makala iliyo katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1999, ukurasa wa 4. Toa onyesho la utoaji uliodokezwa katika fungu la 6. Panga mhubiri mmoja au wawili wasimulie kifupi mafanikio ambayo wamekuwa nayo katika kuanzisha mafunzo, wakieleza jinsi walivyoanzisha funzo na kile walichofanya ili kuendeleza funzo hilo juma baada ya juma.

Wimbo 209 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 19

Wimbo 14

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu na ukaguzi wa hesabu unaofanywa baada ya kila miezi mitatu. Kama kutaniko lina nakala za Vijana Huuliza au Ujana Wako akibani, toa onyesho la jinsi vinavyoweza kutumiwa kwa manufaa katika huduma wakati ambapo kuna uwezekano mkubwa wa kupata vijana nyumbani.

Dak. 8: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.

Dak. 25: “Ningewezaje . . . Isipokuwa Mtu Fulani Angeniongoza?” Mazungumzo ya maswali na majibu yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Panga kila fungu lisomwe kwa sauti ya juu, na usome maandiko yaliyo katika fungu la 3, 4, na 7. Unapozungumzia fungu la 6, eleza daraka la mwangalizi wa utumishi katika kuamua kama inafaa kuanzisha upya funzo la Biblia la kibinafsi na watu waliobatizwa.—Ona Sanduku la Swali katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1998.

Wimbo 89 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 26

Wimbo 39

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Juni. Zungumzia toleo la vichapo la Julai. Onyesha broshua za zamani ambazo zapatikana kwenu, na utaje kifupi kusudi la kila moja. Panga kuwe na onyesho lililotayarishwa vizuri kuonyesha jinsi ya kutoa moja ya hizo katika huduma. Eleza kwamba twaacha broshua bila malipo lakini twakubali michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ya ulimwenguni pote. Mwenye nyumba asema angependa kutoa mchango na mhubiri amshikia bahasha ili aweke mchango wake ndani.

Dak. 17: “‘Iweni Wakarimu, Tayari Kushiriki.’” Maswali na majibu. Tia ndani sababu nne zinazoonyeshwa kwenye kichwa “Sababu Inayotufanya Tutoe” katika Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 1996, ukurasa wa 29-30.

Dak. 18: Jua Jinsi ya Kutoa Jibu. (Kol. 4:6) Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Wewe hufanya nini unapokabili mtu ambaye hufanya mabishano yasiyo ya Kimaandiko? Kitabu Kutoa Sababu mara nyingi hutusaidia kwa kuandaa madokezo yenye kutumika ya jinsi ya kutoa jibu la busara. Kwa mfano, ijapokuwa twaona kifo kuwa adui atakayeshindwa kupitia fidia ya Kristo, wengine wanasadiki kwamba hakuna kitu kitakachoondoa kifo, wao hata huamini wazo lisilo la kweli la kuzaliwa upya katika mwili mwingine. Zungumzia maitikio yanayotolewa katika kitabu Kutoa Sababu katika sehemu “Mtu Akisema—” kwenye ukurasa wa 105-106 na 158. Tia moyo kila mtu abebe kitabu hiki katika huduma ya shambani.

Wimbo 44 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 3

Wimbo 213

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Mwombe mhubiri ambaye ameanzisha mafunzo kwa broshua Anataka asimulie jinsi alivyoweza kufanya hivyo. Panga mapainia wawili waeleze mambo yao yaliyoonwa katika kutoa vichapo kwa mpango wa mchango.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: Kutumia Kanuni za Biblia Huimarisha Maisha ya Familia. Mazungumzo kati ya ndugu wawili, yakitegemea mambo manane yaliyo katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 246. Eleza umuhimu wa kusaidia wanafunzi wa Biblia wajifunze kwamba siri ya kupata furaha ya familia inategemea kuelewa na kutumia kanuni za Neno la Mungu. Ukitumia somo la 8 katika broshua Anataka, toa onyesho jinsi hilo linavyoweza kutimizwa. Familia ambazo zinakubali shauri la Biblia huwa na uhusiano wa karibu na hupata shangwe nyingi katika vifungo vya upendo na muungano. Simulia jambo lililoonwa katika kitabu Furaha ya Familia, sura ya 13, fungu la 1, 21-22.

Wimbo 51 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki