Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/02 uku. 1
  • Endelea Kutanguliza Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kutanguliza Ufalme
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • “Fulizeni Kutafuta Kwanza Ufalme”
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Watumishi wa Huduma Ni Baraka kwa Watu wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Kutanguliza Masilahi za Ufalme Kwanza
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Watumishi wa Huduma Dumisheni Msimamo Mzuri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 1/02 uku. 1

Endelea Kutanguliza Ufalme

1 Si rahisi kutanguliza Ufalme wa Mungu maishani na kuendelea kufanya hivyo tunapokabiliwa na hali ngumu za kiuchumi au matatizo mengine. Twawezaje kuendelea kutanguliza Ufalme matatizo yatokeapo? Vipi tukipata kazi ambayo itatulazimu tukose mikutano au kuvuruga utumishi wetu wa shambani? Je, itabidi tuweke Ufalme mahali pa pili maishani?

2 Ni Lazima Tuwe na Imani Yenye Nguvu: Imani yetu inapojaribiwa na hali hizo, hatupaswi kusahau ahadi ya Yehova na uhakikisho ambao Yesu ametupatia kwamba tutategemezwa na Mungu tukitafuta Ufalme kwanza. (Zab. 37:25; Mt. 6:31-34) Uvutano wa kilimwengu unaweza kutuzuia kuendelea kuona Ufalme kuwa jambo kuu. Wengine wameruhusu matazamio ya kupata cheo kazini au kuchuma fedha kuwa jambo la maana maishani mwao. Hata hivyo, kama Paulo, twahitaji kufikiria kwa uzito ni jambo gani la maana maishani.—Flp. 3:7, 8.

3 Je, Wahitaji Kufanya Marekebisho? Mhubiri mmoja alisema hivi: “Moyo wangu ulikuwa katika biashara yangu—niliipenda sana. Nilifikiri kwamba bado naweza kuwa Shahidi huku nikitumia wakati wangu mwingi katika biashara.” Lakini alihisi kuwa angeweza kufanya mengi zaidi ili amtumikie Yehova. Baada ya muda, aliacha biashara hiyo ambayo ilimzuia kufanya maendeleo ya kiroho. Alipojitoa kabisa kufanya kazi ya Ufalme, alisema hivi: “Sasa naona maisha yangu yana mafanikio machoni pa Yehova, na hilo ndilo jambo muhimu.”

4 Ni jambo lenye kupendeza kwamba, wengi wameacha kazi na matazamio ya kupata fedha nyingi, wakarahisisha maisha yao, na kuingia katika utumishi wa wakati wote. Vijana waseja walio watumishi wa huduma na wazee ambao wamehudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma wamefanya hivyo na wanafurahia mapendeleo ya utumishi. Wakiiga kielelezo bora cha Paulo, wanatosheka na mahitaji ya lazima ya maisha.—1 Kor. 11:1; 1 Tim. 6:6-8; Ebr. 13:5.

5 Ijapokuwa huenda watu katika ulimwengu wakadharau maoni yetu kuhusu maisha, Yehova anatubariki. (1 Kor. 1:26-31) Je, si jambo lenye kutia moyo kujua kwamba atatutumia kikamili iwezekanavyo na kutusaidia tutimize kazi yake? Hatutakuwa na fursa nyingine tena ya kutangaza Ufalme wa Mungu uliosimamishwa. Kwa hiyo, sasa ndio wakati wa kuendelea kutanguliza Ufalme maishani mwetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki