“Watasikiaje?”
1 Yesu alisema hivi kwa mkazo: “Katika mataifa yote lazima habari njema ihubiriwe kwanza.” (Mr. 13:10) Zijapokuwa jitihada zetu nyingi, bado kuna mamia ya mamilioni ya watu ambao hawajahubiriwa. Serikali fulani zinazuia kazi yetu. Idadi ya watu katika nchi nyingi inazidi kuongezeka haraka. Hivyo basi, “watasikiaje?”—Rom. 10:14.
2 Mtumaini Yehova: Lazima tukumbuke kwamba Yehova anajua mioyo ya watu wote. Hata mtu awe na hali gani, akitafuta kweli kumhusu Mungu kwa unyofu, ataipata.—1 Nya. 28:9.
3 Abrahamu alihangaikia sana wakazi wa Sodoma na Gomora. Lakini Mungu alimhakikishia kwamba hangeharibu Sodoma hata kama kungepatikana watu kumi waadilifu huko. (Mwa. 18:20, 23, 25, 32) Yehova hajawahi kamwe kuharibu watu waadilifu pamoja na watu waovu, na jambo hilo linathibitishwa na jinsi alivyowakomboa Loti na binti zake.—2 Pet. 2:6-9.
4 Wakati mmoja Eliya alifikiri kwamba alikuwa akimtumikia Mungu wa kweli akiwa peke yake. Hata hivyo, Yehova alimhakikishia kwamba hakuwa peke yake na kwamba kazi aliyoianza ingekamilika. (1 Fal. 19:14-18) Hali ikoje leo?
5 Na Uwe na Shughuli Nyingi Katika Utumishi wa Mungu: Hatujui ni muda gani umebaki ili kazi ya kuhubiri imalizwe. Yehova ndiye anayeongoza kazi hii na anatumia malaika zake kuisimamia. (Ufu. 14:6, 7) Yeye ndiye atakayeamua kazi hiyo itafanywa kwa kadiri gani katika mataifa yote. Yehova mwenyewe akipenda, anaweza kufanya ujumbe wa Ufalme uenezwe kwa njia ambazo hatuwezi kuwazia ili watu wengi zaidi “wasikie neno la habari njema na kuamini.” (Mdo. 15:7) Kile ambacho Yehova atafanya kitapatana kabisa na utu wake—Mungu mwenye upendo, hekima, na haki.
6 Tuna pendeleo kutenda kupatana na mapenzi ya Yehova, tukifanya yote tuwezayo kujulisha kila mtu habari njema.—1 Kor. 9:16.