Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Januari 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Mzee atoa hotuba yenye kichwa: Unaionaje Migawo? Kuna orodha ndefu ya kazi zinazohitaji kufanywa ili kuendeleza kutaniko: kutayarisha migawo ya programu; kuwapeleka wengine mikutanoni au katika utumishi; kusaidia wazee-wazee; na kusafisha, kurekebisha, na kutunza Jumba la Ufalme, kutia ndani uwanja. Wewe huitikiaje unapoombwa usaidie? Onyesha ni kwa nini kukubali na kutimiza migawo ni pendeleo zuri. Tia moyo wote katika kutaniko waonyeshe roho ya kujitolea.—Zab. 110:3, kielezi chini katika New World Translation of the Holy Scriptures—With References; Isa. 6:8.
Dak. 20: Kunufaika na Maandalizi Yenye Fadhili. Hotuba itolewe na mzee mwenye uzoefu, akizungumzia maandalizi ambayo yamefanywa kutusaidia tunapofanya maamuzi kuhusu tiba. Maandalizi hayo yanatia ndani kadi za Mwelekezo kuhusu tiba na makala za “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2000 na Oktoba 15, 2000. Kutaniko lapaswa liwe na kadi za kutosha zifuatazo: Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia, na Kadi ya Utambulisho. Wahubiri waliobatizwa watapewa kadi hizo baada ya mkutano leo, lakini HAZIPASI kujazwa leo. Kutia sahihi, kushuhudia, na kuandika tarehe katika kadi zote kutafanywa baada ya Funzo la Kitabu la Kutaniko litakalofuata, na kiongozi wa funzo la kitabu anaweza kusaidia ikiwa lazima. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi wanapaswa kuona mwenye kadi akitia sahihi kadi hiyo. Kwa kugeuza maneno yaliyo katika kadi hii yafae hali zao na masadikisho yao wenyewe, wahubiri wasiobatizwa wanaweza kuandika mwelekezo wao wenyewe na wa watoto wao. Kazia umuhimu wa wao kufanya maamuzi mapema kwa kutegemea dhamiri yao iliyozoezwa na Biblia. (Mit. 27:12; 14:15) Ni muhimu kuzungumza mapema na wanatiba ukiwaeleza waziwazi matibabu na dawa utakazokubali. Kujifunza kwa makini kwahitajiwa ili kufanya maamuzi yanayofaa. Soma mafungu katika makala za Mnara wa Mlinzi zilizotajwa juu. Wazee wako tayari kusaidia, lakini hawawezi kuwafanyia wengine maamuzi. Eleza jinsi wanavyoweza kuandika hati za maamuzi yao.
Dak. 15: “Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti.” Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na gazeti la Amkeni! la Januari 8. Panga kijana atoe moja ya maonyesho hayo. Tia moyo wahubiri wote waunge mkono Siku ya Magazeti. Zungumzia Habari za Kitheokrasi. Taja kwamba michango kwa ajili ya Hazina ya Jumba la Ufalme inasaidia makutaniko mengi yawe na Majumba ya Ufalme yenye kupendeza.
Wimbo 55 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Zungumzia sanduku lenye kichwa ‘Weka Kando Kitu Fulani.’
Dak. 13: Je, Unayachunguza Maandiko Kila Siku? Mazungumzo ya familia. Ili kunufaika zaidi na mazungumzo yao ya andiko la kila siku, familia hiyo yazungumzia gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 15, 1996, ukurasa wa 18, fungu la 13-14. Zungumzia kifupi maandiko mawili au matatu ya siku yaliyozungumziwa hivi karibuni, na ueleze jinsi habari hiyo ilivyokuwa na manufaa. Kazia kwamba mpango huo unapaswa kuwa sehemu ya programu ya funzo la Biblia la familia lenye kusudi la kuwafanya waendelee kuwa na bidii kiroho.
Dak. 22: “Endelea Kutanguliza Ufalme.”a Tia ndani maswali machache kuhusu mambo makuu kutoka gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1998, ukurasa wa 19-21.
Wimbo 168 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Januari. Kwa kutumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, toa maonyesho mawili mafupi ya kutoa magazeti, moja ukitumia gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 15 na lingine ukitumia gazeti la Amkeni! la Januari 22, ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8. Taja toleo la vichapo la Februari, ukitaja vitabu ambavyo kutaniko linavyo akibani.
Dak. 20: “Wazazi—Wafundisheni Watoto Wenu Tangu Utotoni.”b Tia ndani maelezo kutoka katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1998, ukurasa wa 32. Alika wazazi wasimulie matokeo mazuri ambayo wamepata kwa kuanza kuwafundisha watoto wao mambo ya kiroho tangu utotoni.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Waombe wahubiri wasimulie mambo waliyoona walipokuwa wakitumia kitabu Kutoa Sababu, wakitoa broshua kadhaa kujibu maswali ya watu, au walipokuwa wakiwapa watu faraja ya Kimaandiko kwa kutumia broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Labda unaweza kuigiza jambo moja au mawili yaliyoonwa.
Wimbo 202 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 4
Dak. 8: Matangazo ya kwenu.
Dak. 17: “Watasikiaje?”c Acha wasikilizaji waeleze jinsi maandiko yaliyotajwa yanavyotumika. Tia ndani maswali ya fungu la 17-18 kwenye ukurasa wa 20 wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 1998.
Dak. 20: “Madokezo ya Utoaji wa Utumishi wa Shambani.” Mazungumzo na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Nyongeza hii ina madokezo ya utoaji ambao ulikuwa katika matoleo ya zamani ya Huduma Yetu ya Ufalme, pamoja na mengine ambayo ni mapya. Mistari iliyoachwa yaweza kutumiwa kuandika madokezo mengine ambayo yatatokea wakati ujao na yatakayofaa eneo lenu. Waombe wasikilizaji waseme madokezo wanayopenda sana na kwa nini. Toa onyesho la dokezo moja au mawili yanayoweza kutumiwa pamoja na toleo la vichapo la Februari. Waombe wahubiri wote waweke nyongeza hii vizuri na kuirudia mara nyingi wanapojitayarisha kwenda katika huduma.
Wimbo 224 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu