Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/04 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Februari 9
  • Juma Linaloanza Februari 16
  • Juma Linaloanza Februari 23
  • Juma Linaloanza Machi 1
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 2/04 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Februari 9

Wimbo 225

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 15 na Amkeni! la Januari 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja, onyesha jinsi ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Nina dini yangu mwenyewe.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 18-19.

Dak. 10: “Faidika kwa Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko ikitegemea makala hiyo. Katika fungu la 2, elekeza fikira kwenye ratiba ya funzo. Katika fungu la 3, soma na kuzungumzia fungu la 23 kwenye ukurasa wa 25 wa kitabu hicho.

Dak. 25: “Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova.”a (Fungu la 1-10) Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Tumia maswali yaliyopo. Wachochee wahubiri wawe na hamu ya kuongeza utendaji wa utumishi wa shambani wakati wa majira ya Ukumbusho.

Wimbo 90 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 16

Wimbo 41

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 15: “Kazi Inayotegemezwa na Mungu.”b Tia ndani maelezo kutoka katika kitabu Wapiga-Mbiu, ukurasa wa 547-548.

Dak. 20: “Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova.”c (Fungu la 11-17) Tumia maswali yaliyopo. Tia ndani onyesho fupi la mhubiri akimwalika rudio kwenye Ukumbusho.

Wimbo 75 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 23

Wimbo 118

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Mwishoni mwa onyesho moja, uliza swali lenye kuamsha fikira linaloweza kujibiwa katika ziara ifuatayo ukitumia broshua Anataka.

Dak. 15: “Tanguliza Uhudhuriaji wa Mikutano kwa Ukawaida.”d Panga mapema mtu mmoja au wawili watoe maelezo kuhusu hatua walizochukua ili wahudhurie kila mkutano.

Dak. 20: Msifu Yehova “Katikati ya Kutaniko.” Mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 2003, ukurasa wa 19-22. (1) Andiko la Zaburi 22:22, 25 hukaziaje sababu ya kutoa maelezo mikutanoni? (2) Kwa nini sala inasaidia? (3) Kwa nini tunahitaji kujitayarisha? (4) Sote tunapaswa kuwa na mradi gani kwenye mikutano? (5) Kwa nini kuketi mbele husaidia? (6) Kwa nini ni muhimu kusikiliza yale ambayo wengine wanasema? (7) Tunaweza kujibuje kwa maneno yetu wenyewe? (8) Tunawezaje kuwatia moyo wengine kwa maelezo yetu? (9) Mwenye kuongoza ana daraka gani?

Wimbo 81 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 1

Wimbo 156

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Februari. Taja toleo la vichapo la Machi, na uzungumzie kifupi mojawapo ya madokezo ya utoaji yaliyo kwenye nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Tia ndani uhitaji wa kutumia vichapo vya zamani ambavyo vinapatikana kutanikoni. Waombe wahubiri waagize vichapo vilivyopo kwa ajili ya maktaba zao na wavitumie katika huduma ya shambani.

Dak. 20: “Tunaweza Kufanya Matakwa ya Yehova.”e Tumia maswali yaliyopo. Wakati ukiruhusu, kazia maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa.

Wimbo 98 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki