Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Taarifa: Huduma Yetu ya Ufalme itapanga Mkutano wa Utumishi wa kila juma wakati wa miezi ya kusanyiko la wilaya. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho yanayohitajiwa ili kuwaruhusu watu wahudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Tembea Pamoja na Mungu.” Pale inapofaa, tumieni dakika 15 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalotangulia kusanyiko ili kurudia shauri linalofaa kwenu lililoonyeshwa katika nyongeza ya mwezi huu. Katika mwezi wa Oktoba, Mkutano mmoja mzima wa Utumishi utatumiwa kupitia mambo makuu ya programu ya kusanyiko. Tukiwa kusanyikoni, sisi sote tunaweza kuandika mambo yatakayotusaidia katika mazungumzo hayo kutia ndani orodha ya mambo hususa tunayotaka kutumia maishani mwetu na katika huduma ya shambani. Kisha tunaweza kuwatia wengine moyo kwa kueleza jinsi ambavyo tumetumia madokezo hayo.
Juma Linaloanza Juni 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 (ikiwa yanafaa eneo la kutaniko lenu) kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 15 na Amkeni! la Mei 22. Katika onyesho moja, panga mhubiri akitoa ushahidi kwenye eneo la biashara. Maonyesho mengine yanayofaa yanaweza kutumiwa.
Dak. 15: “Yehova Huwasaidia Wale Wanaomtegemea.”a Mnapozungumzia fungu la 4, tia ndani maelezo kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 1999, ukurasa wa 4, fungu la 8-9, na kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 67, fungu la 2.
Dak. 20: “Na Tulikweze Jina Lake Pamoja.”b Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko, akitumia maswali yaliyopo. Taja kusanyiko ambalo kutaniko limegawiwa. Saa za programu zimeorodheshwa kwenye nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 2003. Mambo mengine katika nyongeza hiyo yanaweza kukaziwa kulingana na uhitaji. Malizia kwa kuuliza maswali mawili au matatu kutoka katika makala “Chakula cha Kiroho kwa Wakati Unaofaa,” ambayo itazungumziwa kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalofuata.
Wimbo 179 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Malaika Wanatusaidia.”c Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyotajwa wakati ukiruhusu.
Dak. 20: “Chakula cha Kiroho kwa Wakati Unaofaa.”d Tumia maswali yaliyopo. Mnapozungumzia fungu la 2, panga msikilizaji mmoja au wawili waeleze juu ya kusanyiko walilohudhuria ambalo halisahauliki. Malizia kwa kuuliza maswali mawili au matatu kutoka katika makala “Uwe Mtakatifu Katika Mwenendo Wako Wote,” ambayo itazungumziwa katika Mkutano wa Utumishi juma linalofuata.
Wimbo 53 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 28
Dak. 9: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya Hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Juni. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 (ikiwa yanafaa eneo lenu) onyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni 8. Katika kila onyesho, panga mhubiri atoe maelezo mafupi ya kirafiki katika utangulizi wake. Taja kwamba kufanya hivyo kunaweza kumsaidia mwenye nyumba astarehe.
Dak. 18: “Uwe Mtakatifu Katika Mwenendo Wako Wote.”e Tumia maswali yaliyopo. Omba wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wameona mwenendo mzuri kusanyikoni humletea Yehova sifa. Malizia kwa kuuliza maswali mawili au matatu kutoka katika makala “Uwe na Mwonekano Safi Kiadili, Wenye Kustahili Sifa,” ambayo itazungumziwa kwenye Mkutano wa Utumishi juma linalofuata.
Dak. 18: “Kwa Nini Funzo la Kitabu la Kutaniko Ni Muhimu?”f Tumia maswali yaliyopo. Tia ndani maelezo kutoka kwenye makala “Msaidie Mwangalizi Wenu wa Funzo la Kitabu la Kutaniko,” iliyo kwenye ukurasa wa 1 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2002.
Wimbo 20 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 5
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: “Uwe na Mwonekano Safi Kiadili, Wenye Kustahili Sifa.”g Tumia maswali yaliyopo. Wakati ukiruhusu, soma na uzungumzie maandiko yaliyotajwa.
Dak. 20: Kile Ambacho Watoto Wanahitaji Kutoka kwa Wazazi. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji kwa kutegemea kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, ukurasa wa 6-7. Ni muhimu watoto wajifunze kanuni za Biblia zinazoongoza ibada ya kweli na kuelewa daraka muhimu ambalo wazazi hutimiza katika kuwazoeza watoto. Zungumzieni madokezo yaliyotolewa ya kujifunza kitabu hicho. Waombe wazazi watoe maelezo ya jinsi ambavyo wametumia kitabu hicho cha funzo. Panga mtoto mmoja au wawili waeleze kwa nini wanathamini kitabu hicho.
Wimbo 65 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
f Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
g Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.