Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Novemba 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kampeni ya pekee ya kugawanya broshua Endeleeni Kukesha! itamalizika Novemba 14. Siku zinazosalia za mwezi huo, tutatoa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Pitia kwa ufupi maonyesho yaliyodokezwa kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2004, ukurasa wa 3.
Dak. 15: Nufaika Kikamili na Mkutano wa Utumishi. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 71-72. Ni katika njia zipi tano Mkutano wa Utumishi hutusaidia kuwa wahudumu bora tukiwa Wakristo? Taja mifano kwenye ratiba ya mwezi huu. Unanufaikaje kwa kutayarisha mapema? Kwa nini uhudhurie kwa ukawaida? Kuna kielelezo gani cha Kimaandiko kinachoonyesha kwamba mkutano kama huo ulifanywa zamani?
Dak. 20: “Endelea Kutambua Uharaka wa Nyakati Hizi!”a Tia ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 2000, ukurasa wa 12-13.
Wimbo 19 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ikiwa madokezo kwenye ukurasa wa 4 yanafaa katika eneo la kutaniko lenu, yatumie kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15 na Amkeni! la Oktoba 22. Maonyesho mengine yanayofaa eneo lenu yanaweza kutolewa.
Dak. 15: Je, Unatambua Furaha Inayotokana na Kutoa? Hotuba ikitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2004, ukurasa wa 19-23. Ikiwa gazeti hilo halipatikani, tumia la Novemba 1, 2003, ukurasa wa 26-30.
Dak. 20: Sitawisha Upendezi kwa Kutumia Broshua Mpya. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakishughulikiwa na mwangalizi wa utumishi. Ni lazima tufanye ziara za kurudia ili kusitawisha upendezi wa kila mmoja aliyechukua nakala ya broshua Endeleeni Kukesha! Ukitumia ukurasa wa 2, taja kwa ufupi yaliyomo katika broshua hiyo, ukionyesha sehemu zilizoorodheshwa chini ya vichwa vilivyochapwa kwa herufi nzito, na ambazo zimekaziwa kwa rangi mbalimbali ndani ya broshua. Sehemu hizo zinaweza kutumiwa kwa mazungumzo mafupi na yenye kuelimisha unapofanya ziara ya kurudia. Kwa mfano, ikiwa ulizungumzia ukurasa wa 3-4 ulipomtembelea mtu mara ya kwanza, sehemu iliyokaziwa, “Je, Kweli Mungu Anajali?” kwenye ukurasa wa 5 inaweza kuzungumziwa katika ziara ya kurudia. Zungumzia jinsi ya kufanya hivyo. Pitia sehemu nyingine zilizokaziwa, kama zile zilizo kwenye ukurasa wa 6-8 na wa 17-18 au sehemu nyingine zinazofaa eneo lenu. Panga kuwe na onyesho la ziara ya kurudia, ukitumia mojawapo ya sehemu zilizokaziwa. Andiko moja au mawili kati ya yale yaliyotajwa bila kunukuliwa yanaweza kusomwa na kuzungumziwa. Mhubiri anamalizia kwa kutaja sehemu nyingine iliyokaziwa ambayo inaweza kuzungumziwa katika ziara inayofuata.
Wimbo 66 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya Hesabu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Pamoja na Wale Waliochukua Broshua Mpya. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakishughulikiwa na mwangalizi wa utumishi. Zungumzia kwa ufupi onyesho la ziara ya kurudia lililofanywa kwenye Mkutano wa Utumishi juma lililopita, ukitaja hasa sehemu iliyokaziwa ambayo ilitajwa kwenye umalizio wa onyesho hilo. Waombe wahubiri walewale (ikiwezekana), watumie sehemu hiyo iliyokaziwa ambayo ilitajwa ili kuonyesha jinsi ya kufanya ziara nyingine ya kurudia. Kisha, akitumia jalada la nyuma la broshua hiyo mhubiri anamwuliza mwenye nyumba kama angependa kujifunza Biblia. Mipango inafanywa kuzungumzia somo la 1 katika broshua Anataka katika ziara inayofuata. Watie moyo wote wazingatie kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na wale waliochukua broshua Endeleeni Kukesha!
Wimbo 58 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Novemba. Panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na Amkeni! la Novemba 8.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.
Dak. 25: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 3.”b Tumia maswali yaliyopo. Baada ya kuzungumzia fungu la 3, tia ndani onyesho fupi kuhusu kuongoza funzo la Biblia kwa kutumia broshua Anataka, somo la 5, fungu la 1. Fungu limekwisha somwa na swali kujibiwa. Mwenye kuongoza funzo na mwanafunzi wanasoma na kuzungumzia Isaya 45:18 na Mhubiri 1:4. Mwenye kuongoza anauliza maswali rahisi ili kumchochea mwanafunzi aeleze jinsi kila andiko linavyohusiana na jambo linalozungumziwa.
Wimbo 178 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja vichapo vitakavyotolewa Desemba. Panga kuwe na onyesho moja au mawili yanayoweza kutumiwa kutoa kitabu Mtu Mkuu Zaidi.
Dak. 20: “Je, Unaweza Kusaidia?”c Hoji mhubiri mmoja au wawili waliothamini msaada au kitia moyo kutoka kwa wengine.
Dak. 15: Mambo yaliyoonwa. Waombe wasikilizaji wasimulie mambo waliyoona walipowarudia watu ambao walichukua broshua Endeleeni Kukesha! Panga mapema kuwe na maigizo ya mambo yenye kutokeza yaliyoonwa. Wapongeze wote kwa kuunga mkono kampeni hiyo ya pekee.
Wimbo 101 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.