Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Watu wengi hutamani kuwa na afya nzuri na maisha marefu. Lakini, kama ingewezekana, je ungependa kuishi milele? [Ngoja jibu. Kisha usome Yohana 17:3.] Gazeti hili linazungumzia ahadi ya Biblia ya uzima wa milele. Pia, linazungumzia jinsi maisha yatakavyokuwa wakati ahadi hiyo itakapotimizwa.”
Amkeni! Nov. 22
“Katika miaka 20 iliyopita, watu wamefahamu mambo mengi kuhusu UKIMWI na matibabu yake. Lakini wengi bado wamepotoshwa. [Onyesha sanduku “Uwongo Kuhusu UKIMWI,” na ungoje maelezo.] Gazeti hili linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kuwalinda watoto wao.” Soma Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Sifa moja inayowatofautisha wanadamu na wanyama ni ule uwezo wao wa kupambanua yaliyo sawa na yaliyo makosa. Kwa kusikitisha, watu wengi hufanya mambo mabaya. Unafikiri ni kwa nini? [Ngoja jibu. Kisha usome Yeremia 17:9 au Ufunuo 12:9.] Gazeti hili linazungumzia jambo linaloweza kutusaidia kujua na kufanya yaliyo sawa.”
Amkeni! Des. 8
“Maendeleo ya kiteknolojia hayajabadili uhitaji wa msingi wa wanadamu wa kuwa na marafiki. Lakini je, umetambua kwamba mabadiliko katika jamii hufanya iwe vigumu leo kusitawisha urafiki wa karibu pamoja na wengine? [Ngoja jibu. Kisha usome Methali 18:24.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kufanya na kudumisha urafiki.”