Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Kwa kuwa kuna ufisadi mwingi duniani, watu wengine hujiuliza hivi, ‘Kuna haja gani ya kujitahidi kufanya yaliyo sawa?’ Je, umewahi kuhisi hivyo? [Mruhusu ajibu.] Ona maneno haya yenye kutia moyo. [Soma Methali 2:21, 22.] Gazeti hili linatoa sababu muhimu za kuwa wanyoofu.”
Amkeni! Nov.
“Watu wengine hufikiri kwamba Mungu ndiye husababisha kila kitu kinachotokea. Msiba fulani unapotokea, wanasema Mungu ana sababu nzuri za kuusababisha. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Yakobo 1:13.] Gazeti hili linaonyesha kile ambacho Biblia inasema kuhusu chanzo cha kuteseka na kile ambacho Mungu anafanya kukomesha hali hizo.”
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Je, unafikiri kwamba unabii huu wa Biblia unatimia leo? [Soma Mathayo 24:11. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia baadhi ya mafundisho ambayo yamekuwa maarufu. Pia linaonyesha jinsi tunavyoweza kujilinda tusidanganywe na watu wanaofundisha uwongo.”
Amkeni! Des.
“Ungesema ni nani mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi? [Mruhusu ajibu.] Wengi humwona Yesu kuwa mtu mkuu zaidi. Ona kile atakachofanya kuelekea dunia akiwa Mtawala wa Ufalme wa Mungu. [Mwonyeshe picha kwenye ukurasa wa 8-9, na usome moja kati ya maandiko yaliyoonyeshwa.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Yesu atatimiza hilo na ni wakati gani atafanya hivyo.”