Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Sisi sote tungependa kuwa na maisha yenye furaha na kusudi. Je, unakubaliana na maneno ya Yesu hapa kuhusu siri ya kupata furaha? [Soma Mathayo 5:3. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha jinsi ambavyo kutosheleza uhitaji wetu wa msingi wa kumwabudu Mungu unavyofanya maisha yetu yawe na kusudi.”
Amkeni! Nov.
“Katika siku hizi zetu za kisayansi na zenye wachambuzi wengi, watu wengi hufikiri kwamba Biblia imepitwa na wakati. Wewe una maoni gani kuhusu jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Je, ulijua kwamba mambo yote ya kisayansi ambayo Biblia inazungumzia ni sahihi? [Soma Ayubu 26:7.] Toleo hili la pekee la Amkeni! linatoa sababu zenye kusadikisha zinazoonyesha ni kwa nini Biblia inaweza kutegemeka.”
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Unaweza kujibuje swali hili? [Soma swali kwenye jalada. Kisha mruhusu ajibu.] Ni kusudi la Mungu kuwaunganisha wanadamu wote. [Soma Zaburi 46:8, 9.] Gazeti hili linaonyesha kile ambacho Biblia inasema kuhusu jinsi umoja utakavyopatikana.”
Amkeni! Des.
“Wengine huhisi kwamba kifo ni njia ya kuingia kwenye maisha baada ya kifo; nao wengine huamini kwamba kifo ndio mwisho. Je, wewe unafikiri kwamba kifo ni kitu tunachopaswa kuogopa? [Mruhusu ajibu.] Ona maoni ya Ayubu kuhusu taraja lake baada ya kifo. [Soma Ayubu 14:14, 15.] Gazeti hili linazungumzia maelezo ya wazi ya Biblia kuhusu kile kinachotupata tunapokufa.”