Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Watu fulani wamejiuliza kama tunahitaji makanisa na mahekalu ya kumwabudu Mungu. Wafikirije? [Ngoja jibu.] Ona vile Biblia inavyosema kuhusu jambo hilo. [Soma Matendo 17:24.] Basi, mahali pa ibada panapaswa kutumiwa kwa kusudi gani? Gazeti hili lina jibu la Kimaandiko la swali hilo.”
Amkeni! Nov. 22
“Je, wafikiri kwamba siku moja sayansi itakomesha magonjwa? [Ngoja jibu.] Toleo hili la Amkeni! lachunguza baadhi ya maendeleo ambayo sayansi imefanya. Pia laonyesha kwa nini Muumba ana nguvu za kuondoa magonjwa na kifo.” Soma Zaburi 146:3-5, na utoe magazeti.
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Siku hizi karibu kila mtu anaona ugumu wa kupata fedha za kutosheleza mahitaji ya kila siku. Ndivyo ilivyo pia kwa makanisa kupata fedha, na ndiyo sababu hata wanawaomba sana watu watoe fedha. Je, unaona hilo kuwa jambo lenye kuudhi? [Ngoja jibu. Kisha soma 1 Wathesalonike 2:9.] Mnara wa Mlinzi unachunguza kile ambacho Biblia husema kuhusu jambo hili.”
Amkeni! Des. 8
“Kwa sababu ya vitisho vya magaidi, watu wengi wanajiuliza kama kusafiri kwa ndege ni salama. Je, unahangaishwa na jambo hilo? [Ngoja jibu.] Biblia yakubali kwamba hakuna mtu asiyeweza kupatwa na jambo baya. [Soma Mhubiri 9:11.] Hata hivyo, toleo hili la Amkeni! lachunguza jinsi unavyoweza kuzidisha usalama wako na kustarehe unaposafiri kwa ndege.”