Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Zamani, watu wengi waliamini kwamba siku moja dunia itakuwa paradiso. Watu fulani leo hawadhani kwamba dunia itaokoka. Una maoni gani kuhusu wakati ujao wa dunia yetu? [Ngojea jibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo. [Soma Zaburi 37:11.] Gazeti hili linafafanua zaidi yale ambayo Biblia inatabiri kuhusu dunia.”
Amkeni! Nov. 22
Watu wengine wanahofia kwamba mazingira yetu yameharibiwa sana hivi kwamba hayawezi kurekebishwa. Je, unakubaliana nao? [Ngojea jibu.] Muumba hakukusudia dunia iwe pipa la takataka lisiloweza kukaliwa. [Soma Isaya 45:18.] Gazeti hili linaonyesha jinsi dunia itakavyookolewa.”
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Watu fulani leo hawamwamini Mungu. Sababu moja ni kwamba hawapati majibu yenye kuridhisha kwa maswali yanayotatanisha kama haya. [Chagua swali moja katika sanduku kwenye ukurasa wa 6.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jambo moja linaloweza kutusaidia kusitawisha imani ya kweli katika Mungu.” Soma Wafilipi 1:9.
Amkeni! Des. 8
“Je, unafikiri wanadamu watafurahia hali zinazoelezwa katika andiko hili? [Soma Isaya 14:7. Kisha ngojea jibu.] Gazeti hili lina habari inayoweza kutusaidia tunapongojea ahadi za Mungu zitimie.” Mwonyeshe makala “Unawezaje Kushinda Tamaa Mbaya?”