Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Watu wengi hujiuliza sababu inayofanya matatizo yanayowakabili wanadamu yazidi kuwa mabaya. Je, umewahi kufikiri kwamba mambo hayo husababishwa na jambo linalotajwa katika mstari huu? [Soma Ufunuo 12:9. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mbinu ambazo Shetani hutumia kuwapotosha watu na jinsi tunavyoweza kupinga uvutano wake.”
Amkeni! Nov. 22
“Ingawa kuna chakula cha kutosha kuwalisha watu wote duniani, watu milioni 800 hivi hawana chakula cha kutosha. Je, hilo si jambo la kusikitisha? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia ugumu unaozidi kuongezeka wa kulisha majiji. Pia linazungumzia ahadi ya Biblia ya ulimwengu usio na njaa.” Soma Zaburi 72:16a.
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Watu wanaposikia neno ‘Har-magedoni,’ wengi wao huwazia uharibifu mkubwa wenye kutisha. [Mwonyeshe sanduku kwenye ukurasa wa 3.] Je, ungeshangaa kujifunza kwamba Har-magedoni ni mojawapo ya mambo mazuri zaidi ambayo yatawahi kutupata? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza sababu.” Soma 2 Petro 3:13.
Amkeni! Des. 8
“Ningependa kukueleza kuhusu wakati ambapo kila mtu atakuwa na makao yanayofaa. Je, si jambo la kusikitisha kwamba watu wengi sana hawana makao? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Isaya 65:21, 22.] Gazeti hili linazungumzia mambo yanayosababisha ukosefu wa makao. Pia linaeleza jinsi ambavyo Mungu atatimiza ahadi ambayo tumesoma.”