Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Je, unafikiri waume na wake wakitii shauri hili la Biblia, ndoa zitaimarika? [Soma Ayubu 31:1. Mruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia kanuni za Biblia zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kuendelea kuwajibika katika ndoa.” Kazia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Nov.
“Watu wengi wanakubali kwamba rasilimali za bahari zinaendelea kumalizika haraka sana. Je, unafikiri kwamba serikali za wanadamu zitatatua tatizo hilo? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Mathayo 6:10.] Makala hii inazungumzia sababu za kuhangaikia jambo hilo na inakazia suluhisho ambalo Mungu anatoa.” Kazia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Wakati huu wa mwaka, watu wengi wanamfikiria Yesu. Unafikiri Yesu ana uvutano gani maishani mwako? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatuhimiza tufuate mfano wa Yesu. [Soma 1 Petro 2:21.] Tukifanya hivyo tunaweza kuboresha utu wetu na kuwa wenye furaha zaidi. Gazeti hili linaeleza sababu.”
Amkeni! Des.
“Watu fulani wamekuwa wakifikiria swali hili kwa karne nyingi. [Onyesha swali kwenye jalada.] Unafikiri tunaweza kupata wapi jibu lenye kuridhisha? [Mruhusu ajibu.] Ona kwa nini tunaweza kumtegemea Mungu atupe jibu. [Soma Zaburi 100:3.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo.”