Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/03 uku. 8
  • Wasaidie Wale ‘Walio na Mwelekeo Unaofaa’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Wale ‘Walio na Mwelekeo Unaofaa’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kubali Daraka la Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kujitayarisha—Siri ya Kufanya Ziara za Kurudia Zenye Manufaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Hakikisha Kwamba Unarudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 12/03 uku. 8

Wasaidie Wale ‘Walio na Mwelekeo Unaofaa’

1 Kila mtu ana mwelekeo fulani wenye nguvu katika moyo wake wa mfano. (Mt. 12:35) Biblia inasema kwamba watu fulani wana ‘moyo ulio na mwelekeo wa kupigana.’ (Zab. 55:21) Wengine wana “mwelekeo wa ghadhabu.” (Met. 29:22) Lakini pia kuna wale ‘walio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.’ (Mdo. 13:48) Leo, Yehova anawakusanya watu hao wenye mwelekeo unaofaa. (Hag. 2:7) Tunawezaje kuwasaidia wawe waabudu wa Yehova?

2 Fanya Ziara za Kurudia kwa Bidii: Ili tutimize kazi yetu ya kufanya wanafunzi, ni muhimu tuwe na maoni yanayofaa kuhusu ziara za kurudia. (Mt. 28:19, 20) Je, sisi huwarudia haraka wale wanaopendezwa? Je, sisi huwarudia wote wanaokubali vichapo au wale wanaopendezwa na habari njema? Je, tunajitahidi kuwasaidia wakue kiroho? Kwa kuwa uhai unahusika, tunapaswa kujitahidi kuwarudia watu wote wanaopendezwa.

3 Andika jina na mahali anapoishi mtu anayependezwa kabla hujasahau mambo mliyozungumzia. Andika mambo mliyozungumzia, maandiko yoyote mliyosoma, na kichapo alichochukua. Kisha, hakikisha umerudi haraka iwezekanavyo.

4 Kufanya Ziara ya Kurudia: Unapofanya ziara ya kurudia, ni muhimu uwe mchangamfu, mwenye urafiki na upendezwe kikweli na mwenye nyumba. Fanya mazungumzo yawe sahili na yategemee Maandiko. Tayarisha habari yenye kusisimua kutoka katika Biblia, na baada ya mazungumzo uliza swali ambalo utajibu kwenye ziara itakayofuata. Epuka kubishana na mwenye nyumba kuhusu maoni yake yasiyo ya Kimaandiko. Jitahidi kuendeleza mazungumzo kwa kutumia mambo ambayo mnakubaliana.—Kol. 4:6.

5 Jitihada zinahitajiwa ili kufanya ziara za kurudia, lakini matokeo huridhisha. Painia mmoja huko Japani aliweka mradi wa kufanya ziara nyingi kila mwezi. Alianza kuandika majina ya watu wote aliowapata alipokuwa akihubiri nyumba kwa nyumba, kisha akawatembelea tena kabla ya juma kwisha. Alitayarisha vizuri habari ambayo angezungumzia na akahubiri kwa usadikisho kabisa. Alipokuwa akifanya ziara moja ya kurudia, alianzisha funzo na mtu mmoja aliyemwambia hivi: “Sikuzote mimi huwafukuza. Hii ndiyo mara yangu ya kwanza kuwasikiliza.” Uvumilivu wa painia huyo ulikuwa na matokeo mazuri. Kufikia mwisho wa mwezi wa kwanza, alikuwa akiripoti mafunzo kumi ya Biblia.

6 Hali za watu hubadilika-badilika daima. (1 Kor. 7:31) Ili kumpata tena mtu mwenye kupendezwa nyumbani kwake, mara nyingi itakubidi kumtembelea mara kadhaa. Tukifanya ziara za kurudia kwa bidii, tunaweza kuwasaidia wale walio na mwelekeo unaofaa kuifuata barabara inayoongoza kwenye uzima wa milele.—Mt. 7:13, 14.

[Maswali ya Funzo]

1. Yehova anawakusanya nani leo?

2. Kazi yetu ya kufanya wanafunzi inahusisha nini?

3. Tufanye nini baada ya kuzungumza na mtu katika huduma?

4. Tunawezaje kufanya ziara za kurudia zenye matokeo?

5. Painia mmoja alifanya jitihada gani, naye alipata matokeo gani?

6. Kwa nini tuendelee kufanya ziara za kurudia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki