Mambo ya Kukumbuka Wakati wa Ukumbusho
Siku ya Ukumbusho mwaka huu ni Alhamisi, Machi 24. Wazee wanapaswa kukumbuka mambo yafuatayo:
◼ Mnapopanga saa ya mkutano huo, hakikisheni kwamba mkate na divai havitapitishwa kabla ya jua kushuka.
◼ Wote, kutia ndani msemaji, wanapaswa kujulishwa saa na mahali pa mwadhimisho.
◼ Fanyeni mipango mapema ili kuwe na mkate na divai inayofaa.—Ona toleo la Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 2003, ukurasa wa 14-15.
◼ Sahani, glasi, meza na kitambaa cha meza vinavyofaa vinapaswa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine ambapo mwadhimisho huo utafanywa panapaswa kusafishwa vizuri mapema.
◼ Wakaribishaji na wale watakaopitisha mkate na divai wanapaswa kuteuliwa na kuelezwa mapema juu ya wajibu wao, utaratibu unaofaa kufuatwa, na umuhimu wa kuwa nadhifu na kuvalia mavazi yenye kuheshimika.
◼ Pangeni kuandaa mkate na divai kwa ajili ya watiwa mafuta walio wagonjwa na wasioweza kuhudhuria.
◼ Ikiwa makutaniko zaidi ya moja yatatumia Jumba la Ufalme, mipango mizuri inahitajika ili kusiwe na msongamano usio wa lazima kwenye Jumba, milangoni, barabarani, au kwenye maegesho ya magari.