Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Wengi wetu tutatumia sehemu kubwa ya maisha yetu kufanya kazi. Watu fulani huona kazi kuwa baraka huku wengine wakiiona kuwa laana. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mhubiri 2:24.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia kuwa na maoni yanayofaa kuhusu kazi. Pia linazungumzia jinsi ya kukabiliana na mfadhaiko unaosababishwa na kazi.”
Amkeni! Juni 22
“Je unafikiri kwamba jamii yetu ingekuwa bora ikiwa kila mmoja wetu angeishi kupatana na maneno haya? [Soma Waefeso 4:28, kisha umruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia hasara kubwa ambayo sisi sote hupata kutokana na wizi wa dukani. Pia linaonyesha jinsi wizi wa dukani na aina nyingine zote za uhalifu zitakavyokomeshwa hivi karibuni.”
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Sisi sote tunajua watu fulani ambao wanaonekana wamefanikiwa lakini bado hawaridhiki na maisha yao. Unafikiri wanatafuta nini? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mathayo 5:3.] Gazeti hili linazungumzia njia muhimu ya kupata amani ya akili, yaani, kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho.”
Amkeni! Julai 8
“Ukosefu wa kazi ni tatizo kubwa katika ulimwengu huu ambamo watu wengi wanang’ang’ania nafasi za kazi. Gazeti hili linaorodhesha mbinu tano za kupata kazi. [Mwonyeshe vichwa vyenye herufi nzito katika makala “Mbinu Tano za Kupata Kazi.”] Pia linatoa mapendekezo mazuri kuhusu jinsi ya kudumisha kazi.” Soma andiko la Methali 22:29, ambalo limenukuliwa katika ukurasa wa 10.