Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/05 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 8
  • Juma Linaloanza Agosti 15
  • Juma Linaloanza Agosti 22
  • Juma Linaloanza Agosti 29
  • Juma Linaloanza Septemba 5
Huduma ya Ufalme—2005
km 8/05 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

TAARIFA: Mwezi mmoja au miwili baada ya kutaniko kuhudhuria Kusanyiko la Wilaya la “Utii wa Kimungu,” mnapaswa kutenga dakika 15 hadi 20 katika Mkutano wa Utumishi (mnaweza kutumia sehemu ya mahitaji ya kwenu) ili kupitia mambo mliyojifunza kusanyikoni, ambayo yamewasaidia wahubiri katika utumishi wa shambani. Sehemu hiyo ya pekee ya Mkutano wa Utumishi itatupa nafasi ya kueleza jinsi tunavyotumia mambo tuliyojifunza kusanyikoni na jinsi ambavyo yameboresha huduma yetu.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2005, uku. 2.

Juma Linaloanza Agosti 8

Wimbo 125

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Wakumbushe wahubiri kuhusu tarehe za programu ya kusanyiko la mzunguko na kusanyiko la Pekee la mwaka wa utumishi wa 2006 iwapo zinajulikana. Panga kuwe na onyesho moja au mawili ya mapendekezo ya kuwarudia wale walioachiwa broshua. Mapendekezo hayo yamo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 2005.

Dak. 10: “Je, Unatumia Vikaratasi vya Mwaliko?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Waalike wasikilizaji waeleze matokeo mazuri ambayo wamepata kwa kutumia vikaratasi vya mwaliko. Tia ndani onyesho fupi la mhubiri akitumia kikaratasi cha mwaliko kumwalika mtu anayependezwa kwenye mkutano.

Dak. 25: “Sasa Ndio Wakati wa Kuhubiri!”a Panga mapema painia wa kawaida mmoja au wawili waeleze walifanya marekebisho gani ili wawe mapainia na baraka ambazo wamepata.

Wimbo 197 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 15

Wimbo 11

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu) kuonyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Julai 15 na Amkeni! la Julai 22. Panga onyesho la mzee na mhubiri aliye dhaifu kimwili wakihubiri kwa simu ikiwa inafaa eneo lenu. Ikiwa hamhubiri kupitia simu, panga onyesho la njia tofauti ya kuhubiri, kama vile mzee na mhubiri aliye dhaifu kimwili wakijifunza Biblia na mwanafunzi anayekuja nyumbani kwa mhubiri huyo aliye dhaifu, au wakitoa magazeti mhubiri huyo akiwa ameketi mahali wanapopita watu wengi.

Dak. 15: Je, Unakumbuka? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 2005, ukurasa 30. Waalike wasikilizaji wajibu kila swali. Kazia jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa. Watie moyo wote wasome kwa makini kila nakala ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

Dak. 20: “Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Mlangoni na Kupitia Simu Inapowezekana au Kupitia Barua.”b Tia ndani onyesho fupi la jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa katika ziara ya kwanza kwa kutumia fungu moja au mawili katika broshua Anataka. Simulia jambo moja au mawili yenye kutia moyo kuhusu kuanzisha funzo la Biblia kupitia simu au kwa barua.

Wimbo 30 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 22

Wimbo 161

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Zungumzia Habari za Kitheokrasi na utaje kwamba kiasi fulani cha michango ya hiari hutumiwa kwa ajili ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Kuhubiri Kuhusu Ufalme Ni Pendeleo la Pekee.”c Unapozungumzia fungu la 4, pitia mpango wa pekee wa kuripoti vipindi vya dakika 15 kwa ajili ya walio wazee au wenye afya mbaya.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme, Oktoba 2002, uku. 8, fu. 6.

Wimbo 204 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 29

Wimbo 45

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Agosti. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu), onyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na Amkeni la Agosti 8. Katika onyesho moja, mhubiri anamrudia mtu ambaye hupelekewa magazeti kwa ukawaida.

Dak. 15: “Kutoa Ushahidi Bila Kusema Neno Lolote.”d Waalike wahubiri waeleze jinsi mwenendo mzuri wa watu wa Mungu ulivyowasaidia kuwa watumishi wa Yehova.

Dak. 20: Kutumia Biblia Katika Ziara ya Kwanza. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Pitia mapendekezo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2004, ukurasa 6, fungu 2, kuhusu kutumia Neno la Mungu katika ziara za kwanza. Onyesha jinsi pendekezo moja au mawili yanavyoweza kutumiwa kutoa toleo la vichapo la mwezi wa Septemba. Wakati ukiruhusu, mnaweza kuzungumzia mapendekezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005 na mfanye maonyesho ya kutoa toleo hilo.

Wimbo 71 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 5

Wimbo 98

Dak. 10: Matangazo ya kwenu.

Dak. 15: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 12.”e Panga mapema mhubiri mmoja au wawili waeleze kilichowasaidia kufanya maendeleo katika kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia.

Dak. 20: Kufanya Mpango wa Kuwasaidia Wazee-Wazee. Hotuba hii inapaswa kutolewa na mzee, nayo inategemea habari iliyo katika Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 1993, ukurasa 28-29, chini ya kichwa kidogo “Kupanga Mambo Ni Jambo la Thamani.” Taja mipango ambayo kutaniko limefanya ili kuwasaidia wagonjwa na wale walio wazee-wazee.

Wimbo 164 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki