Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Oktoba 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Septemba 15 na Amkeni! la Septemba 22 kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu). Baada ya kila onyesho kazia mambo mazuri ya onyesho. Zaidi ya hayo, kazia makala za ziada ambazo huenda zikawavutia watu katika eneo lenu.
Dak. 15: Je, Una Mazoea Mazuri ya Kujifunza? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea sehemu zilizoteuliwa katika kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 21-26. Unaweza kutumia mapendekezo gani katika ratiba yako ya kusoma? (uku. 21, sanduku) Kwa nini ni muhimu kusoma vichapo vinavyoandaliwa? (uku. 23, fu. 2) Ni nini kinachoweza kutusaidia kudumisha ratiba nzuri ya kusoma? (uku. 26, fu. 3-4) Unafanya nini ili kutenga wakati wa kusoma magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!? Umenufaikaje kwa kufanya hivyo?
Dak. 20: “Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri.”a Waombe wasikilizaji waeleze ni hali gani ambazo zinaweza kufanya iwe vigumu kujipa ujasiri unaohitajika ili kutoa ushahidi. Ni nini ambacho kimewasaidia kujipa ujasiri?
Wimbo 78 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia jambo moja au mawili katika sehemu ya 3 ya nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2005, kuhusu jinsi tunavyoweza kutumia vizuri Maandiko tunapoongoza mafunzo ya Biblia.
Dak. 15: Epuka Hatari za Intaneti. Hotuba itakayotolewa na mzee inayotegemea Amkeni! la Desemba 8, 2004, ukurasa wa 18-21.
Dak. 20: “Onyesha Unawajali Watu Kikweli kwa Kuwatendea kwa Fadhili.”b Waombe wasikilizaji waeleze jinsi tunavyoweza kuwa wenye fadhili tunapowahubiria wengine. Matoleo yatakayofuata ya Huduma Yetu ya Ufalme yatazungumzia mambo mengine yanayohusu jinsi tunavyoweza kuwajali wale tunaowahubiria.
Wimbo 2 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Panga kuwe na onyesho la jinsi ya kutoa toleo la mwezi wa Novemba kwa kutumia pendekezo moja katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, au njia nyingine inayofaa eneo lenu.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, uku. 8, fu. 5.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Ikiwa mmekuwa na kusanyiko la wilaya, pitieni mambo makuu ya kusanyiko. Ona taarifa kwenye ukurasa wa 2 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2005.
Dak. 20: Mavazi na Mapambo Yanayopatana na Viwango vya Mungu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Mnara wa Mlinzi, la Agosti 1, 2002, ukurasa wa 17-19, ishughulikiwe na mzee. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi mavazi na mapambo yanayofaa yanavyotusaidia kupata fursa ya kutoa ushahidi.
Wimbo 153 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 31
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za mwezi wa Oktoba. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1 na Amkeni! la Oktoba 8 kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu). Katika onyesho moja mhubiri anakazia sanduku, “Katika Toleo Linalofuata,” ili kuweka msingi kwa ajili ya ziara ya kurudia.—Ona Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1998, uku. 12, fu. 7-8.
Dak. 15: Wapelekee Watu Magazeti kwa Ukawaida ili Kuwachochea Wapendezwe Zaidi. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2005, ukurasa wa 8. Tunawezaje kuwapata watu ambao tunaweza kuwapelekea magazeti kwa ukawaida? (fu. 1) Tunawezaje kutayarisha mfululizo wa mazungumzo yanayotegemea andiko moja? (fu. 3) Kwa nini haitoshi kusoma tu andiko tulilochagua? (fu. 4) Tunawezaje kuanzisha funzo la Biblia pamoja na mtu tunayempelekea magazeti kwa ukawaida? (fu. 5) Panga kuwe na onyesho la mhubiri anayezungumzia andiko moja na mtu fulani anayempelekea magazeti kwa ukawaida.
Dak. 20: Vijana Walio Thabiti na Wenye Heshima. Hotuba itakayotolewa na mzee inayotegemea kichwa kidogo “Jiepushe kwa Heshima” katika Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 2002, ukurasa wa 23-24. Panga mapema vijana wawili waeleze kuhusu matatizo ambayo wamekabili shuleni na yale ambayo yamewasaidia kuyashughulikia kwa mafanikio.
Wimbo 222 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 7
Dak. 5: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: Boresha Uwezo Wako wa Kuwa Makini Katika Mikutano. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 2002, ukurasa wa 12-14, fungu la 11-14. Pitia mapendekezo yaliyotolewa, na uwaombe wasikilizaji waeleze ni nini ambacho kimewasaidia kunufaika zaidi na mikutano ya kutaniko.
Dak. 20: “Sitawisha Ustadi wa Kujadiliana na Wengine.”c Panga mapema wahubiri kadhaa waeleze jinsi ambavyo wamejadiliana na watu wa malezi mbalimbali katika eneo lenu.
Wimbo 50 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.