Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/05 uku. 5
  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2005
Huduma ya Ufalme—2005
km 12/05 uku. 5

Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 26, 2005. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Novemba 7 hadi Desemba 26, 2005. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba tunatoa himizo “juu ya msingi wa upendo”? (Flm. 9) [be uku. 266]

2. Tunaweza “kuhimiza kwa fundisho lenye afya” katika njia zipi? (Tito 1:9) [be uku. 267 fu. 1-2]

3. Kwa nini ni muhimu kutoa hotuba zenye kutia moyo, na tunawezaje kufanya hivyo? [be uku. 268 fu. 1-3, sanduku]

4. Kama Musa, kuwasaidia wengine wakumbuke mambo ambayo Yehova amewafanyia watu wake kunawezaje kuwachochea wawe jasiri? (Kum. 3:28; 31:1-8) [be uku. 268 fu. 5–uku. 269 fu. 2]

5. Kwa nini kuzungumzia kwa furaha mambo ambayo Yehova anafanya sasa na yale atakayofanya wakati ujao huwatia moyo wasikilizaji? [be uku. 270-271]

HOTUBA NA. 1

6. Septuagint ni nini, na kwa nini iwapendeze Wakristo? [si uku. 307 fu. 12–uku. 310 fu. 14]

7. Wamasora walikuwa nani, nao walichangia katika njia zipi muhimu kutafsiriwa kwa Biblia? [si uku. 310 fu. 18; uku. 311 fu. 20-21]

8. Ni maandishi gani yaliyotumiwa zaidi kutafsiri Maandiko ya Kiebrania katika New World Translation, na kwa nini inaweza kusemwa kwamba tafsiri hiyo ni sahihi na yenye kutegemeka? [si uku. 312 fu. 28, 30]

9. Wakristo wa mapema walionyeshaje tamaa kubwa ya kuhubiri Neno la Mungu? [si uku. 315 fu. 1-5]

10. Uchunguzi wa hati zilizopo na maandishi ya awali ya Maandiko Matakatifu unafunua nini kuihusu Biblia? [si uku. 320 fu. 32]

USOMAJI WA BIBLIA KILA JUMA

11. Kwa kuwa Daudi hakuruhusiwa kujenga hekalu, je, hiyo inamaanisha kwamba Yehova hakuvikubali vita ambavyo Daudi alipigana? (1 Nya. 22:6-10)

12. Katika sala yake ya kuweka hekalu wakfu, Sulemani alionyeshaje kwamba Yehova huhangaikia mahitaji ya watumishi wake wakiwa kikundi na kwamba anajua hali hususa ya kila mmoja anayemwogopa? (2 Nya. 6:29, 30)

13. Wale “roho waovu wenye umbo la mbuzi” wanaotajwa kwenye 2 Mambo ya Nyakati 11:15 ni nini?

14. Kwa kuwa utawala wa Baasha ulianza “katika mwaka wa tatu wa Asa” na kudumu kwa miaka 24 tu, tunawezaje kusema kwamba Baasha “alikuja kupigana na Yuda” katika “mwaka wa 36 wa utawala wa Asa”? (1 Fal. 15:33; 2 Nya. 16:1)

15. Andiko la 2 Mambo ya Nyakati 20:22, 23 linaonyeshaje waziwazi jambo ambalo litaupata ulimwengu wa Shetani hivi karibuni?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki