Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mac. 15
“Wengi wetu tumekabili huzuni ya kufiwa na mpendwa wetu. Je, umewahi kusikia ahadi hii yenye kufariji? [Soma Matendo 24:15. Mruhusu ajibu.] Hata hivyo, watu wengi hujiuliza, Ni nani watakaofufuliwa? Ufufuo utatukia lini? Utatukia wapi? Gazeti hili linatoa majibu ya Biblia kwa maswali hayo.”
Amkeni! Mac.
“Watu wengi wanaamini kwamba Yesu ni Mungu. Jambo la kupendeza ni kwamba Petro, aliyekuwa mwanafunzi wa Yesu alimtambulisha kuwa Mwana wa Mungu. [Soma Mathayo 16:16.] Je, unafikiri Yesu anaweza kuwa Mungu na tena awe Mwana wa Mungu? [Mruhusu ajibu.] Makala hii kwenye ukurasa wa 12-13 inazungumzia swali hilo, ikitoa maoni ya Biblia.”
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Maneno haya yanayojulikana sana hukazia umuhimu wa kupata ujuzi kumhusu Mungu. [Soma Mathayo 4:4.] Hata hivyo, watu wengi huona kwamba ni vigumu kuelewa Neno la Mungu. Je, unakubaliana na jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yanayofaa ambayo yanaweza kukusaidia kuielewa Biblia.”
Amkeni! Apr.
“Watu wengi hujitahidi kupata furaha, lakini inaonekana kwamba ni wachache wanaoipata. Je, unafikiri mojawapo ya mambo yaliyoonyeshwa hapa yanaweza kuwasaidia watu wawe na maisha yenye furaha zaidi? [Mwonyeshe sanduku kwenye ukurasa wa 9. Kisha soma mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa.] Gazeti hili la Amkeni! huzungumzia mambo yanayotajwa katika Biblia ambayo yanaweza kuchangia furaha ya kweli.”